KAHAMA MANISPAA
Member
- Jul 20, 2015
- 15
- 15
Mfanya biashara maarufu nchini Tanzania na nje ya nchi..Mzee kishimba,ameamua kurudi nyumbani kwao kahama kuwania ubunge jimbo la kahama mjini,ambalo liko ndani ya Manispaa ya kahama.Kishimba anasifika kwa umahiri mkubwa wa kufanya biashara ndani na nje ya nchi..jambo ambalo limewasitua wanakahama wengi ni pamoja na kishimba kuchukua form...wanasema,"hivi hawa wafanya biashara wameona siasa ndio kichaka cha kujifichia?"mmoja wazee alisema.Pia kishimba alishawahi kugombania jimbo Msalala na Emmanuel Kipole kushinda kinyang'anyiro hicho cha ubunge.Jambo jingine ambalo linamtia doa Kishimba ni kile kitendo alichokifanya kipindi cha ukame cha kuwazuia wanakijiji wa kata ya Nzongomera kuchota maji kwenye visima vyake.kitendo ambacho aliwanyanyasa akina Mama na watoto kutembea umbali mrefu kufaata maji..mzee mmoja ambaye ni Baba mdogo wa Mzee kishimba anasema," hatuwezi kumpa kura mtu ambaye alitunyima maji ya kunywa..yeye na hela zake aende zake".hiyo ni kauli ya wazee wenyeji wa hapa mjini.Hivyo kishimba tunaomba utafakari kwani huwezi kutuongoza!