Marashaaa95
JF-Expert Member
- Nov 9, 2015
- 842
- 709
Ume muelewesha Vizuri sana MkuuMkuu Wewe utakua ni mgeani katika safari za mwanza-dar, hiyo route ina bus nyingi sana hata 40 yanaweza timia, na kila kampuni ina abiria wake kabisa,
Kuna buss za starehe, yaani wala bata. Wenyewe hata bus itumie siku 3 kwenda dar hawana shida.
Kuna bus kwa ajili ya watu wa kazi, watu wa appointment na wafanyabiashara (wengi wao ni wasukuma wa mwanza na wanyantuzu wa simiyu ) hao watu hawataki kusikia bus inalala njiani, hapo Ndio utakutana na Kisbo na kibo
Ukijaribu kukumbuka vizuri kwa aliekua anaomba kujisaidia hata abiria tu walikua either wanamshangaa, ama wanamcheka.
Umezungumzia neno kutoboa
Kwa kifupi ni kwamba kwa route ya mwanza -dar, ikifika saa 4 kamili za usiku bus yenu haijafika morogoro ujue hamtaruhusiwa kuendelea na safari, lazima mtalala hapo na mtaendelea na safari yenu baadae alfajiri.
Na mwendo wa bus kumbuka uko limited siku hizi, ni 80 kph
Sasa kwa aina hiyo ya abiria niliokutajia, hawataki kusikia habari ya kulala njiani,
Utasikia Dereva usifanye masihara tunataka kutoboa sisi oohooo!
Na moja ya vitu vinavyochelewesha safari ni hiyo ya kukojoakojoa hovyo,
Kisbo kwa ku-serve muda wana vituo vyao maalum, wakitoka mwanza kituo ni shinyanga, wakitoka shinyanga ni singida, baada ya singida ni manyoni, na baada ya hapo ni dodoma, wakitoka dodoma chuma inatembea mpaka morogoro kabla ya saa 4 wanapita hapo, na kituo kinachofuata ni ubungo.
Hata ukitoa taarifa kituo cha polisi abiria karibu wote watakugeuka maana lengo lao ni kutoboa