Kisarawe tatizo wafugaji na wakulima

Kisarawe tatizo wafugaji na wakulima

wakurochi

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2017
Posts
2,647
Reaction score
2,957
Mimi kama mkulima namkaribisha kwa furaha Mkuu wa Wilaya aliyechaguliwa hivi karibuni. Wenzake wote hilo tatizo limewashinda ama walizembea. We fikiria umelima mahindi na mihogo unataka kuvuna ndio ng'ombe 100 wanaingia shamba na hata ukishitaki kwa mwenyekiti unaambiwa hana mamlaka ya kukamata mhalifu, ila wewe mkulima unatakiwa ugharimie usafiri wa askari haipungui elfu 40 (wa pikipiki). Ili mwenye mifugo akamatwe.

Cha kushangaza mapori ni mengi. Ila ni kama kwa hapa DSM mtu badala ya kuchunga jangwani apeleke punda, ng'ombe na kondoo fire halafu wakate waingie msimbazi watokee shule ya uhuru. Ndicho kinachofanyika kila siku mpaka tunachangia visima na mifugo.

Akiiweza changamoto hii Wakulima wengi watapona. Hili ni tatizo la muda mrefu na chanzo ni viongozi vijiji Matamko kibao yametolewa na wakuu wa Wilaya bila mafanikio.
 
Waf
Vip mashamba huko bei gani
Wafugaji wanatakiwa kubadilika, ardhi haiongezeki, watu wanaongezeka, wanatakiwa kufuga kisasa ili kuondoka na changamoto za magomvi na wakulima, kwani wakulima huona kama wanadharauliwa na wafugaji hii ni kutokana kwamba, wakulima bidhaa yao ni ya muda mfupi, sasa mifugo inapokula mazao ya mkulima inaonekana mfugaji anafanya makusudi, ingawa wanaofanya makusudi wapo pia.
 
Waf

Wafugaji wanatakiwa kubadilika, ardhi haiongezeki, watu wanaongezeka, wanatakiwa kufuga kisasa ili kuondoka na changamoto za magomvi na wakulima, kwani wakulima huona kama wanadharauliwa na wafugaji hii ni kutokana kwamba, wakulima bidhaa yao ni ya muda mfupi, sasa mifugo inapokula mazao ya mkulima inaonekana mfugaji anafanya makusudi, ingawa wanaofanya makusudi wapo pia.

Ni sawa Mkuu ni kwamba viongozi wanajua tatizo ni mfugaji. Ila wanaishia kutoa matamko tu. Mfugaji ana pesa kila wakati kwasababu hanunui majani ya kula mifugo na mara nyingine analisha na kwenye mahindi na maboga ya mkulima na, ng'ombe akikua na kupata uzito bora anawahi mnadani, mkulima hana uwezo wa kufanya chochote. Kwa kweli sina namna ya kuwafikishia ujumbe hawa viongozi. Yaani mkuu wa Wilaya. Ila hii ni kero kubwa.
 
Ni sawa Mkuu ni kwamba viongozi wanajua tatizo ni mfugaji. Ila wanaishia kutoa matamko tu. Mfugaji ana pesa kila wakati kwasababu hanunui majani ya kula mifugo na mara nyingine analisha na kwenye mahindi na maboga ya mkulima na, ng'ombe akikua na kupata uzito bora anawahi mnadani, mkulima hana uwezo wa kufanya chochote. Kwa kweli sina namna ya kuwafikishia ujumbe hawa viongozi. Yaani mkuu wa Wilaya. Ila hii ni kero kubwa.
Dawa ni kukamata mifugo yao mpaka kielewke lakini naona huyu mkuu wa wilaya kaonyesha njia, kweli wafugaji wanaona wana pesa sana kuliko mfugaji, wakikamatwa wa mfano wakafungwa na kulipa faini akili zitawakaa sawa.
 
sasa mkuu mnalima porini?
Mkuu umenifurahisha na swali lako Ili eneo liitwe shamba ni kwamba kuna kazi imefanyika hapo. Kazi hiyo ni pamoja na pori kukatwa miti,kuondoa visiki n.k.nadhani wengine watasaidia kukuelewesha, kama una nia kweli ya kuelewa na kupata shamba.

Kwa hiyo hakuna mtu anaefanya kazi hiyo halafu anatafuta wanunuzi, au labda kama kuna mtu alikuwa na shamba anataka kuuza,hao ni wachache. Mashamba mengi ni ya wazawa ya kurithi au wenyeji ambapo hayauzwi ovyo ovyo. Kama unataka Shamba kama uko makini hupati humu JF na kwenye keyboard nenda vijijini onana na viongozi wa vijiji watakupa tatatibu.
 
Mkuu umenifurahisha na swali lako Ili eneo liitwe shamba ni kwamba kuna kazi imefanyika hapo. Kazi hiyo ni pamoja na pori kukatwa miti,kuondoa visiki n.k.nadhani wengine watasaidia kukuelewesha, kama una nia kweli ya kuelewa na kupata shamba.

Kwa hiyo hakuna mtu anaefanya kazi hiyo halafu anatafuta wanunuzi, au labda kama kuna mtu alikuwa na shamba anataka kuuza,hao ni wachache. Mashamba mengi ni ya wazawa ya kurithi au wenyeji ambapo hayauzwi ovyo ovyo. Kama unataka Shamba kama uko makini hupati humu JF na kwenye keyboard nenda vijijini onana na viongozi wa vijiji watakupa tatatibu.
asante mkuu
 
Back
Top Bottom