GE2025 Kisaka: Mdahalo Wa Kisiasa Hauwezi Kufanyika Bila Usawa wa Vyama

GE2025 Kisaka: Mdahalo Wa Kisiasa Hauwezi Kufanyika Bila Usawa wa Vyama

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Meneja wa Huduma za Utangazaji katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mhandisi Andrew Kisaka, amesisitiza kuwa midahalo ya kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lazima izingatie usawa na weledi ili isiwe na kasoro zinazoweza kupotosha taswira ya uchaguzi.

Akizungumza Agosti 16, 2025 jijini Arusha katika Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji Kanda ya Kaskazini, Kisaka ameeleza kuwa midahalo yenye washiriki wachache au usiokuwa na uwiano wa vyeo vya chama inapoteza maana na heshima yake.

“Kama mdahalo ni wa vyama vitatu na kimoja kikaahirisha, viwili vinaweza kuendelea. Lakini kama ni mdahalo wa vyama viwili na chama kimoja kikijitoa, huo si mdahalo tena. Vilevile, kama umeita Makatibu Wakuu, hakikisha wote ni Makatibu Wakuu na siyo chama kimoja Katibu Mkuu, kingine mweka hazina – huo si mdahalo,” amesema Kisaka.

Aidha, Kisaka ameonya juu ya upendeleo katika idadi ya wafuasi wanaoruhusiwa kuingia ukumbini, akibainisha kwamba kila chama kinachoshiriki mdahalo lazima kipewe nafasi sawa ya wawakilishi.

“Kama CCM imeruhusiwa watu 20, basi na CHADEMA wapate 20. Na hao watu wasiwe kundi la upande mmoja tu – changanya walimu, wafanyabiashara, manesi, vijana na wasomi ili ukumbi uakisi taswira halisi ya jamii,” ameongeza.
Screenshot 2025-08-16 164809.png
 
Meneja wa Huduma za Utangazaji katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mhandisi Andrew Kisaka, amesisitiza kuwa midahalo ya kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lazima izingatie usawa na weledi ili isiwe na kasoro zinazoweza kupotosha taswira ya uchaguzi.

Akizungumza Agosti 16, 2025 jijini Arusha katika Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji Kanda ya Kaskazini, Kisaka ameeleza kuwa midahalo yenye washiriki wachache au usiokuwa na uwiano wa vyeo vya chama inapoteza maana na heshima yake.

“Kama mdahalo ni wa vyama vitatu na kimoja kikaahirisha, viwili vinaweza kuendelea. Lakini kama ni mdahalo wa vyama viwili na chama kimoja kikijitoa, huo si mdahalo tena. Vilevile, kama umeita Makatibu Wakuu, hakikisha wote ni Makatibu Wakuu na siyo chama kimoja Katibu Mkuu, kingine mweka hazina – huo si mdahalo,” amesema Kisaka.

Aidha, Kisaka ameonya juu ya upendeleo katika idadi ya wafuasi wanaoruhusiwa kuingia ukumbini, akibainisha kwamba kila chama kinachoshiriki mdahalo lazima kipewe nafasi sawa ya wawakilishi.

“Kama CCM imeruhusiwa watu 20, basi na CHADEMA wapate 20. Na hao watu wasiwe kundi la upande mmoja tu – changanya walimu, wafanyabiashara, manesi, vijana na wasomi ili ukumbi uakisi taswira halisi ya jamii,” ameongeza.

Mkutano huo uliandaliwa na TCRA kwa ushirikiano na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), ambapo washiriki kutoka sekta ya habari na vyombo vya usalama walikumbushwa kuzingatia kanuni na maadili ya kitaaluma katika uripoti na uendeshaji wa midahalo kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Chanzo: Jambo Tv
 
Nilichogundua awaambiwi kufanya hivyo ila nizamu ya uoga tu inawafanya kujipendekeza, kwaiyo mdahalo pia unatakiwa kuchujwa TCRA
 
Ungepigwa mdahalo wa mama abdul na TAL kwa nusu saa tu, baada ya mdahalo yule mother angewekewa drip za maji, mafuta,chakula na damu kwa pamoja
 
Mhandisi anaweka misingi na utaratibu wa namna vyombo vya habari vinavyopaswa kuendesha wajibu wao. Kana kwamba hakuna wenye uweledi huo ndani ya waandishi wenyewe.

Kwamba, kama mdahalo unawahusu makatibu uenezi na chama x kikawakilishwa na katibu mkuu ambaye wiki mbili alikuwa katibu mwenezi, huo sio mdahalo!.

Kama chama.kimetuma.mwakilishi wewe ni nani wa kukipangia? BBC waliendesha mdahalo, Mkapa hakutokea na badala yake akatumwa mwakilishi kuwakabili kina Mrema, Lipumba nk, ule haukuwa mdahalo?
Wakati umefika waandishi mjitambue.
 
Meneja wa Huduma za Utangazaji katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mhandisi Andrew Kisaka, amesisitiza kuwa midahalo ya kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lazima izingatie usawa na weledi ili isiwe na kasoro zinazoweza kupotosha taswira ya uchaguzi.

Akizungumza Agosti 16, 2025 jijini Arusha katika Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji Kanda ya Kaskazini, Kisaka ameeleza kuwa midahalo yenye washiriki wachache au usiokuwa na uwiano wa vyeo vya chama inapoteza maana na heshima yake.

“Kama mdahalo ni wa vyama vitatu na kimoja kikaahirisha, viwili vinaweza kuendelea. Lakini kama ni mdahalo wa vyama viwili na chama kimoja kikijitoa, huo si mdahalo tena. Vilevile, kama umeita Makatibu Wakuu, hakikisha wote ni Makatibu Wakuu na siyo chama kimoja Katibu Mkuu, kingine mweka hazina – huo si mdahalo,” amesema Kisaka.

Aidha, Kisaka ameonya juu ya upendeleo katika idadi ya wafuasi wanaoruhusiwa kuingia ukumbini, akibainisha kwamba kila chama kinachoshiriki mdahalo lazima kipewe nafasi sawa ya wawakilishi.

“Kama CCM imeruhusiwa watu 20, basi na CHADEMA wapate 20. Na hao watu wasiwe kundi la upande mmoja tu – changanya walimu, wafanyabiashara, manesi, vijana na wasomi ili ukumbi uakisi taswira halisi ya jamii,” ameongeza.
View attachment 3443161
Mbona.katolea.mfano katibu na siyo mwenyekiti
 
Back
Top Bottom