Habarini wapendwa!!!
Kwa kipindi kilichopita nilitoa Mada kuwa nilianzisha mahusiano na dada yake na mke wangu. Wengi walinikejeli na matusi, wengine wakanipa ushauri mzuri ambao umenisaidia.
Maana ilibidi nimchane live kuwa mwisho utakuwa sio mzuri na itakuwa aibu ambayo haijapata kutokea katika familia zetu na hatujui sehem tungekimbilia. Alichonijibu kuwa ningemwacha angemwambia mke wangu kuwa nilimlewesha kupita kiasi na nikambaka. So ilibidi niendelee na mahusiano kwa muda kidogo ili kuweka mambo sawa kabla mke wangu hajarudi kutoka maternity.
Kutokana na uzuri wa shemeji hata mimi ilinipa wakati mgumu kumwacha.
Mbinu niliyotumia ni kuwa wiki ilopita baada ya kumaliza kufanya mapenzi nikajifanya nimepandisha mashetani. Nikajirusha chini ya kitanda na kufanya vituko vichache... mwanzoni alidhani kama masiara lakini nilikomaa ili aamini. Alitoka chumbani mbio na kwenda sebuleni, baada kama ya dk 5 alirudi kuchungulia. Nilikuwa nimetulia alipokuja kuniuliza "baby vipi" nikamjibu poa. Akaniuliza tena "umepatwa na nini"? Nikamwambia mbona nipo vizuri sina tatizo, akawa ananikumbusha yaliyotokea. Nikamwambia acha masihara......
Kesho yake mke wangu alinipigia kuniuliza una tatizo lolote, nikamjibu mbona niko safi. Akaniambia kuwa dada yake alinisikia napiga kelele chumbani. Nikamjibu labda nilikuwa naota tu.
Shemeji hakukoma, hivi juzi alitaka penzi. kabla sijaanza mapenzi nikanyanyuka nikajifanya mwili umeishiwa nguvu, nikashuka sakafuni. Ilibidi nijikojolee kwa makusudi ili ajue siko poa hata kidogo. Kwani kujikojolea sh ngapi bwana? Hapa nakimbizana na muda wa kurudi mke wangu kama wiki 3 zijazo. Alipoona hivyo alivumilia kuona mwisho wake. Nikachenji sura alitoka nduki. Alirudi baada ya mda kidogo akakuta nipo safi ila ndo ivo nimejikojolea. Nikamuuliza nani kanimwagia maji? Hakujibu
Sasa sijui kama amejua ni kweli nina matatizo au namchezea akili ili aniache?
Nawasilisha