Bado ninaushauri uongozi wa Itv wakiboreshe kipindi hiki kiwe kama kile cha tbc cha mchakato majimboni wakati wa uchaguzi! Hii itatusaidia kuyaibua matatizo ya wananchi from the grass root. Kuna matatizo makubwa huko majimboni na hayapati nafasi ya kusikika. Binafsi nimepoteza imani na wakazi wa dar! Licha ya kuwa wengi ni wasomi na mabigwa wa kulalamika kwenye media, uchaguzi ukifika utadhani wamelogwa! Wanasahau kila kitu na kuichagua ccm! Huu ni unafiki mkubwa. Na kujidhalillisha wenyewe. Ni aibu upinzani kupata ushindi mkubwa shy, kigoma, kilimanjaro na kwingineko kuliko dar!
Haki ya mungu we una akili sana! Vipindi hivi hebu viandaliwe kushirikisha maskini wenyewe kule Kwetu Kishumundu, Mpitimbi, Kanyigo,Nyamongo etc. Na tuwaulize kwa nini pamoja na hali zao wanachagua bado serikali yenye mfumo ule ule? Kwa nini vijana wao wanawakimbia nakutua mijini n never come back. Kwa nini wana rasilimali lakini bado hawasogei. Wakishirikishwa hivyo na kuchangiwa na wasomi wetu watapata hatua ya kuanzia. Kuwachukua wala chipsi kuku kama mimi waliopo mijini tu tutabaki tunajadiliana tu na kusifia mijadala. Tuwafanye wenye nchi wanaoipa CCM kura bila kutaka wala kujiuliza wajiunge kwenye mbio za ukombozi.