Kipindi hiki cha TBC 1 mlengwa ni nani?

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,457
956
Kipindi cha "This week in Perspective" ni moja ya vipindi vizuri vyenye kuchambua mambo muhimu sana katika jamii ya kitanzania.Hujaribu kufafanua masuala mbalimbali yaliyomo ndani ya jamii - kiuchumi, kisiasa na hata kijamii. Suala au mada huchambuliwa kwa kina na katika hilo hujaribu pia kugusia ufumbuzi wa baadhi ya changamoto zinazojitokeza.

Mfano kipindi cha wiki hii kilikuwa juu ya "Youth and Employment". Mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na kuibua tatizo katika kutegemea ajira kwa vile kijana "kamesoma", kumbe basi kama mfumo ungeboreshwa, vijana wangeandaliwa mapema kabla hata hawajaingia vyuoni ili watakapofuzu mafunzo yao wajiajiri wenyewe.

Kitu nilichoona ni kwamba mada zinahusu jamii za kitanzania.Nikabaki najiuliza, mada za kiingereza zitawafikiaje? Tunajua kabisa kwamba Tanzania inatumia Kiswahili kama lugha ya taifa, na isitoshe wasikilizaji wengi hawatumii lugha ya kiingereza. TBC ni TV ya taifa. Kipindi muhimu kama hiki hakiwezi kutafsiriwa kwa kuweka "sub titles",kama ni lazima kiingereza kitumike ili watu wengi wafuatilie.Au basi kipindi kiwe kwa kiswahili ili wananchi wafaidike na elimu inayotolewa kwenye kipindi hiki. Au walengwa ni akina nani?
 
Kipindi cha "This week in Perspective" ni moja ya vipindi vizuri vyenye kuchambua mambo muhimu sana katika jamii ya kitanzania.Hujaribu kufafanua masuala mbalimbali yaliyomo ndani ya jamii - kiuchumi, kisiasa na hata kijamii. Suala au mada huchambuliwa kwa kina na katika hilo hujaribu pia kugusia ufumbuzi wa baadhi ya changamoto zinazojitokeza.

Mfano kipindi cha wiki hii kilikuwa juu ya "Youth and Employment". Mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na kuibua tatizo katika kutegemea ajira kwa vile kijana "kamesoma", kumbe basi kama mfumo ungeboreshwa, vijana wangeandaliwa mapema kabla hata hawajaingia vyuoni ili watakapofuzu mafunzo yao wajiajiri wenyewe.

Kitu nilichoona ni kwamba mada zinahusu jamii za kitanzania.Nikabaki najiuliza, mada za kiingereza zitawafikiaje? Tunajua kabisa kwamba Tanzania inatumia Kiswahili kama lugha ya taifa, na isitoshe wasikilizaji wengi hawatumii lugha ya kiingereza. TBC ni TV ya taifa. Kipindi muhimu kama hiki hakiwezi kutafsiriwa kwa kuweka "sub titles",kama ni lazima kiingereza kitumike ili watu wengi wafuatilie.Au basi kipindi kiwe kwa kiswahili ili wananchi wafaidike na elimu inayotolewa kwenye kipindi hiki. Au walengwa ni akina nani?

Kipindi ni kizuri kama ulivyosema inawezekana kimewekwa makusudi pia kwa ajili ya kuwezesha wageni waalikwa wasiojua kiswahili pamoja na baadhi ya watanzania n.k wasiojua vizuri kiswahili waweze kutoa michango yao kwa ufasaha ila kingerushwa pia kwa Lugha ya kiswahili, mimi binafsi chambuzi zao fulani zilinisaidia sana kwenye mitihani yangu mwisho mwaka wa jana hivyo kwa wanachuo nafikiri kinamsaada.
 
Back
Top Bottom