Kipimo cha DNA...Ungekuwa Ungefanyaje?

Kipimo cha DNA...Ungekuwa Ungefanyaje?

NGOSWE.120

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2011
Posts
219
Reaction score
234
Wana MMU,

Naomba tuwekane sawa katika hili jambo. Jaribu-ku-imagine kuwa wewe ndio mhusika (ukiwa Ke chukuwa nafasi ya mwanamke, Ukiwa me chukua nafasi ya mwanaume).

Upo na Mkeo/mumeo, mungu amewabariki na mmepata watoto wawili. Mtoto wa kwanza ni wa kike na amefanana sana na baba, na mtoto wa pili wa kiume mnabaini kuwa hajafanana na mama wala baba yake achilia mbali babu,shangazi mjomba n.k

Mume anastuka sana, lakini anaamua kupotezea kwa kuwa mtoto bado mdogo. Baada ya miezi kadhaa sura mtoto inazidi kujionyesha na hatimaye baba-unagundua kuwa amefanana na mtu fulani ambaye mkeo wanafahamiana kwa kuwa ni kabila moja na wametoka sehemu moja.

Kwa kuwa roho inauma na unahisi kuna mchezo umefanyika, unamshauri mkeo muende mpime DNA ya mtoto ili kuondoa hofu iliopo.

Majibu ya mkeo/yaani wewe dada unayesoma uzi huu kwa mume wako:

1. Naona umeamua kunitukana, nashukuru sana.
2.Nakubali kwenda kupima DNA lakini nikiwa kwangu na baba watoto wangu.
3.Umeshafanikiwa ndio maana unanimbia hayo mambo ya kupima DNA, Mimi naenda kuanza maisha yangu; NAONDOKA!


NB: Hivi kuna ugumu gani kwenda kupima DNA wana MMU? Kupima DNA si ni sawa tu na kupima Malaria au HIV-Test?
AU kuna ajenda iliyopo nyuma ya pazia kuhusu huyu mke?

TOA MAWAZO YAKO KUHUSIANA NA HII SINTOFAFAHAMU.

Asanteni, poleni kwa maelezo marefu.
 
Walakini ni asilimia 98 kuna msaada hapo mtoto wa kuchomekeana
 
Kitendo cha kumwambia mkeo mkapime DNA maana yake humuamini na unamchukulia kama msaliti na ndio maana anasema unamtukana!
 
Kupima DNA imezoeleka kuwa ni kwa ajili ya kuondoa sintofahamu ya uhalahi wa watoto kuwa wa baba husika.
Si kitu kizuri mume kukishauri kwa mkewe hasa kama hajawahi kukupa sababu ya kumhisi vibaya.
Binafsi mtu amkague tu vidole mtoto bila mie kujua ila siku akiniambia habari za DNA wakati nina hakika watoto ni wake nitamuuliza tu,yupi unahisi si wako?
Akimtaja namwambia baba wa huyo ndio baba wa fulani na fulani.
Nipe wanangu nikalee mbele ya safari,tafuta utakayemuamini uzae nae.
 
^^
Siwezi kutishwa na kauli nyepesi kama hizo, kuna mambo ukiyaendekeza gharama yake kubwa!
Eti naenda kuanza maisha?? Go for good
^^
 
Kitendo cha kumwambia mkeo mkapime DNA maana yake humuamini na unamchukulia kama msaliti na ndio maana anasema unamtukana!

Lakini kama unajiamini hujachepuka kuna tatizo lolote? si bora kwenda na kuondoa hizo doubts au wewe unaonaje?
 
Lakini kama unajiamini hujachepuka kuna tatizo lolote? si bora kwenda na kuondoa hizo doubts au wewe unaonaje?

Na kwann ufikirie kupima DNA kama kuna uaminifu?thats a big insult ujue!bora uchukue vipimo ukapime kisirisiri!
 
Uaminifu una mipaka yake na mipaka hiyo ikivukwa huwa ubwege.

Dhana ni kitu kibaya sana...kama kuna kila sababu zinazokupelekea usimuamini mtu hapo sawa lakini kama mtu mnaishi kwa amani kabisa halafu unazuka mkapima DNA from nowhere atakuelewaje lazima ujipange haswa kujieleza sababu zinazoeleweka zikapelekea wewe kuchukua hatua hizo!
 
]Ili kuleta imani kwa umpendaye[/B] hubby wako si bora tu mkampime hiyo makitu ili mumeo azidi kukupenda zaidi au unaonaje?


Yaani mume tu ndio center of attention,kwa nini asijiulize mimi nitajisikiaje kwa hiyo suggestion na hasa kama sijawahi kumpa sababu ya kutoniamini?
 
Dhana ni kitu kibaya sana...kama kuna kila sababu zinazokupelekea usimuamini mtu hapo sawa lakini kama mtu mnaishi kwa amani kabisa halafu unazuka mkapima DNA from nowhere atakuelewaje lazima ujipange haswa kujieleza sababu zinazoeleweka zikapelekea wewe kuchukua hatua hizo!

^^
The guilt are always afraid....
^^
 
^^
Mkuu, hawa viumbe ukiwachekea sana, utalea shule nzima isiyo damu yako!
^^

Hahaaa! Umesababisha nicheke Himidini!
Hivi kuna wanaoongoza kuzaa nje ya ndoa kama wanaume? Au kwa sababu pua zenu hazikui sambamba na mimba mlizosababisha ndio mnajiona mko salama sana na kujivika utakatifu msiokuwa nao?
Kupeleka mtoto kupima DNA ni kumtusi mwenza wako,period!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom