Kipi kitangulie kati ya haki na amani?

Kipi kitangulie kati ya haki na amani?

VIVIANET

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2015
Posts
2,129
Reaction score
2,920
Si mara moja au mbili ni mara nyingi nimesikia kama si kwa viongozi waandamizi,basi viongozi wa dini.

Pia si haba kusikia watu wa kada mbalimbali nchini wakitoa wito wa kutunza amani.Vyombo vya dola navyo haviko nyuma katika kuwataka watu kuendelea kuitunza amani,sambamba na hilo wamekuwa wakiwatahadharisha wanchi kwamba vyombo vya dola havitaweza kumvumilia mtu yeyote atakayejaribu kuvunja amani. Pia jana ktk hotuba yake Rais amesema hatoweza kumvumilia mtu anayethubu kuivunja amani.

Swali langu ni hili hivi ni kipi kinachotakiwa kutetewa na kupewa kipaumbele kati ya amani na haki? Kwa ufahamu wangu naamini amani ni tunda linalozaliwa na haki. kutokana na andiko la Biblia Mithali 14:34 haki uinua taifa, bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.

Haki ndicho chanzo cha amani, Lakini sijasikia vyombo vya dola na viongozi waandamizi wakitetea haki kwa nguvu na kutahadharisha wale wote wanaowanyima watu haki zao kwamba wangekiona au kuchukuliwa hatua kali. Hivi ni kipi kinatangulia kati ya Haki na Amani?
 
Wao wanafikiri amani inapatikana kwa kusali na vitisho na ubabe, kumbe amani inapatikana kwa kutenda haki, ndiyo maana unakuta viongozi wengine wanataka kuombewa kwa Mungu kila siku, ukitenda haki huitaji kuombewa Mungu mwenyewe anaona
 
Haki ni stahili ya MTU! Amani kwa upande naitafasiri kama ni stahili ya watu wote na si MTU mmoja kama tafasiri ya haki. Kimsingi amani na haki ni sawa na Maji na samaki. Ushauri wangu kwa watz tuzingatie, tudumishe amani na tudai haki kwa haki, tunajua haki haidaiwi ila huchukuliwa, ifahamike kwamba hata katika mandiko matakatifu imeandikwa 'USIWE MWENYE HAKI KUZIDI KIASI'
 
Si mara moja au mbili ni mara nyingi nimesikia kama si kwa viongozi waandamizi,basi viongozi wa dini. Pia si haba kusikia watu wa kada mbalimbali nchini wakitoa wito wa kutunza amani.Vyombo vya dola navyo haviko nyuma katika kuwataka watu kuendelea kuitunza amani,sambamba na hilo wamekuwa wakiwatahadharisha wanchi kwamba vyombo vya dola havitaweza kumvumilia mtu yeyote atakayejaribu kuvunja amani. Pia jana ktk hotuba yake Rais amesema hatoweza kumvumilia mtu anayethubu kuivunja amani. Swali langu ni hili hivi ni kipi kinachotakiwa kutetewa na kupewa kipaumbele kati ya amani na haki? Kwa ufahamu wangu naamini amani ni tunda linalozaliwa na haki. kutokana na andiko la Biblia haki uinua taifa.Haki ndicho chanzo cha amani, Lakini sijasikia vyombo vya dola na viongozi waandamizi wakitetea haki kwa nguvu na kutahadharisha wale wote wanaowanyima watu haki zao kwamba wangekiona au kuchukuliwa hatua kali. Hivi ni kipi kinatangulia kati ya Haki na Amani?
madikteta hupenda sana amani lakini sio kutenda haki, haiwezekani hutendi haki alafu utegemee kuwa na amani
 
Neno la MUNGU katika Mithali linasema " Haki huinua Taifa". Misingi ya amani ni pamoja na haki. Nashangaa hata viongozi wa dini wanapotosha ukweli wanaoujua. Mmoja kazindua kitabu juzijuzi kusisitiza amani na hazungumzi lolote kuhusu haki. Nimeamua kutonunua kitabu hicho ambacho kwa maoni yangu kinazungumza jambo nusunusu. Machafuko yote hutokea pale watu wanaponyimwa haki yao ya kiroho, kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni. Unategemea nini kama watu wanalipa kodi lakini hospitalini, shuleni, miundombinu, n.k hakuna kinachoendelea? Viongozi wa dini semeni ukweli badala ya kila siku kufuatana na Makonda. Yaani siku hizi ukiwa na shida na kiongozi wa kiroho uliza tu alipo Makonda. Kwani Makonda amewaahidi nini ninyi viongozi wetu wa kiroho?
 
Hakuna amani bila haki hata aombe Papa bila haki hakuna amani acha viongozi Wa dini waombe labda Mungu atawasikia
 
a
Haki ni stahili ya MTU! Amani kwa upande naitafasiri kama ni stahili ya watu wote na si MTU mmoja kama tafasiri ya haki. Kimsingi amani na haki ni sawa na Maji na samaki. Ushauri wangu kwa watz tuzingatie, tudumishe amani na tudai haki kwa haki, tunajua haki haidaiwi ila huchukuliwa, ifahamike kwamba hata katika mandiko matakatifu imeandikwa 'USIWE MWENYE HAKI KUZIDI KIASI'
andiko gani na mstari wa ngapi?
 
Back
Top Bottom