Kipanya: Bado yuko na biashara mpaka kieleweke

Kipanya: Bado yuko na biashara mpaka kieleweke

Faana

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2011
Posts
42,787
Reaction score
50,903
1743052109122.png
 
Sijaelewa aisee
Zamani chain ilikuwa na watanzania watatu.. mmoja anatoa mzigo China anapeleka Kariakoo, mwingine anaufata Kariakoo anaenda kuuza Tabora mjini na mwingine anachukua Tabora anaenda kuuza wilayani Sikonge..

Mchina sasa hivi anauza mwenyewe hadi Sikonge hivyo watanzania wote kati shughuli imekufa..

Faida kwa mnunuzi wa mwisho bei inaweza kupungua kidogo lakini hasara kwa hawa wafanyabiashara na Taifa kwasababu hii faida ya kati sasa nayo inaenda China badala ya kubaki kwa watanzania.
 
Faida kwa mnunuzi wa mwisho bei inaweza kupungua kidogo lakini hasara kwa hawa wafanyabiashara na Taifa kwasababu hii faida ya kati sasa nayo inaenda China badala ya kubaki kwa watanzania.
Taifa linapata hasara kivipi mkuu? Kwani mchina anawauzia watu wote (watumiaji wa mwishi) hiyo bidhaa? Si hao wanaonunua wanauza pia kwa faida kidogo. Mchina anauza Sikonge mjini ila mnunuzi wa Sikonge anaenda kuuza minadani vijijini huko, si bado fedha inazunguka hapahapa.

Tatizo ni tamaa tu ya wafanyabiashara kutaka kupata faida kubwa iliyopitiliza. Yaani mfano nipo Mbezi Mwisho nataka kununua shati hapo Mbezi mwisho na bei yake ni Tshs. Elfu 11 ila shati hilohilo Kariakoo linauzwa Tshs. Elfu 10, unafikiri nitaacha kununua mbezi ili nifuate Kariakoo ambako nauli ya kwenda na kurudi itakua Tshs. 2,000/=?
 
Hao wholesalers wa DSM na Tabora waende kufanya shughuli zingine. Wakarine asali, wakavue, wakalime pamba au wakawekeze hata kutengeneza hizo biashara walikuwa wanauza.
Athari yake ni kubwa kuliko hii, pesa ikichukuliwa yote na mchina maana yake hawa watu wa kati spending power yao inakufa. Mathalan kama alikuwa anataka kujenga nyumba ya kuishi hatawaweza tena, watakaoathirika ni mafundi ujenzi, wauza vifaa vya ujenzi, malori ya kubeba vifaa kwenda saiti, mama ntilie wanauza kwenye site etc.. pia hawa wamama na mafundi wanaenda kupunguza matumizi mitaani kwao kama maduka ya mangi etc and the impact goes on.

Ujasiriamali wao ukifa, wao na staff wao waliowaajiri mwanzoni wanakuja kupambania vibarua vilivyopo, chako kinaweza kuporwa etc.

Wachina bora waende kuwekeza sehemu ambazo tulikuwa tunaagiza badala ya kuzalisha mwanzoni kwani inaongeza fursa zaidi kwa Taifa kama kwenye viwanda vikubwa etc. Ila huku kwenye uchuuzi waache waswahili though na wenyewe wateremshe bei.
 
Taifa linapata hasara kivipi mkuu? Kwani mchina anawauzia watu wote (watumiaji wa mwishi) hiyo bidhaa? Si hao wanaonunua wanauza pia kwa faida kidogo. Mchina anauza Sikonge mjini ila mnunuzi wa Sikonge anaenda kuuza minadani vijijini huko, si bado fedha inazunguka hapahapa.

Tatizo ni tamaa tu ya wafanyabiashara kutaka kupata faida kubwa iliyopitiliza. Yaani mfano nipo Mbezi Mwisho nataka kununua shati hapo Mbezi mwisho na bei yake ni Tshs. Elfu 11 ila shati hilohilo Kariakoo linauzwa Tshs. Elfu 10, unafikiri nitaacha kununua mbezi ili nifuate Kariakoo ambako nauli ya kwenda na kurudi itakua Tshs. 2,000/=?
Si hao watu watatu wamepungua mkuu, kwenye uchumi kuna kitu huwa tunaita 'multiplier effect'. Athari kwa watu watatu inaondoka na watu wote waliokuwa wananufaika nao kwa namna moja au nyingine ikiwemo kijamii na kiuchumi.
 
Very deep, safi sana ameilezea kwa lugha ya picha labda wale vichwa ngumu wataelewa.

Kuna watu humu eti kwasababu wao ni consumers aka end users wanaona kama haiwahusu, wanasahau kama tayari hapo tunatengeneza tatizo la ajira.
 
Maiti zilizo kufa miaka 60 iliyo pita hadi ije ifufuke Tanzania itakuwa ipo utumwani.. wacha wachina wapige kazi

Ingekuwa kenya wangesha kinukisha
 
Back
Top Bottom