BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
ANASHANGAA MHESHIMIWA LISSU KUSHAURIWA NA ASKOFU KWA KUWA HAMJUI ASKOFU ANAYEMSHAURI RAIS MAGUFULI!
Ukiongea na Askofu Mwamakula uwe makini sana kwa sababu anatunza kumbukumbu vizuri. Hebu fuatilia mazungumzo yake na mmoja wa viongozi wa dini siku kadhaa zilizopita.
Kiongozi wa Dini: Nimesikia kuwa wewe ni Askofu Mshauri wa Tundu Lissu! Ni kweli? Leo nataka nikusikie kwa kinywa chako.
Askofu Mwamakula: Sahihi
Kiongozi wa Dini: Kwa nini?
Askofu Mwamakula: Kwani ni dhambi kwa Askofu kuwa Mshauri wa Mgombea Urais?
Kiongozi wa Dini: Sio dhambi! Lakini huoni kama hiyo itakuwa ni hatari sana kwako na kwa Kanisa lenu?
Askofu Mwamakula: Ni hatari kwa mgombea Urais kushauriwa na Askofu? Ulitaka ashauriwe na wachawi au waganga wa kienyeji?
Kiongozi wa Dini: Hapana! Lakini kuwashauri wapinzani ni hatari sana katika mazingira ya sasa! Utaonekana kama unapingana na Serikali.
Askofu Mwamakula: Kwani wapinzani sio Watanzania?
Kiongozi wa Dini: Ni Watanzania
Hivi wewe huogopi lakini?
Askofu Mwamakula: Siogopi! Kwani katika Biblia, Wafalme walikuwa hawashauri na manabii?
Kiongozi wa Dini: Walikuwa wanashauriwa kabisa.
Askofu Mwamakula: Hivi unamjua Askofu Mshauri wa Rais Magufuli?
Kiongozi wa Dini: Hivi kweli yupo? Simjui!
Askofu Mwamakula: Ukiombwa wewe uwe mmoja wa Viongozi wa Dini Washauri wa Rais Magufuli utakubali?
Kiongozi wa Dini: Ha ha ha! Kwa nini nikatae kama kuna uhitaji?
Askofu Mwamakula: Haitakuwa hatari kwako?
Kiongozi wa Dini: Ha ha ha! Kwa kuwa nitakuwa nashauri serikali haitakuwa hatari.
Askofu Mwamakula: Mheshimiwa Lissu akiingia madarakani utakuwa tayari kuwa mshauri wake?
Kiongozi wa Dini: Hapo hakuna shida.
Ukiongea na Askofu Mwamakula uwe makini sana kwa sababu anatunza kumbukumbu vizuri. Hebu fuatilia mazungumzo yake na mmoja wa viongozi wa dini siku kadhaa zilizopita.
Kiongozi wa Dini: Nimesikia kuwa wewe ni Askofu Mshauri wa Tundu Lissu! Ni kweli? Leo nataka nikusikie kwa kinywa chako.
Askofu Mwamakula: Sahihi
Kiongozi wa Dini: Kwa nini?
Askofu Mwamakula: Kwani ni dhambi kwa Askofu kuwa Mshauri wa Mgombea Urais?
Kiongozi wa Dini: Sio dhambi! Lakini huoni kama hiyo itakuwa ni hatari sana kwako na kwa Kanisa lenu?
Askofu Mwamakula: Ni hatari kwa mgombea Urais kushauriwa na Askofu? Ulitaka ashauriwe na wachawi au waganga wa kienyeji?
Kiongozi wa Dini: Hapana! Lakini kuwashauri wapinzani ni hatari sana katika mazingira ya sasa! Utaonekana kama unapingana na Serikali.
Askofu Mwamakula: Kwani wapinzani sio Watanzania?
Kiongozi wa Dini: Ni Watanzania
Hivi wewe huogopi lakini?
Askofu Mwamakula: Siogopi! Kwani katika Biblia, Wafalme walikuwa hawashauri na manabii?
Kiongozi wa Dini: Walikuwa wanashauriwa kabisa.
Askofu Mwamakula: Hivi unamjua Askofu Mshauri wa Rais Magufuli?
Kiongozi wa Dini: Hivi kweli yupo? Simjui!
Askofu Mwamakula: Ukiombwa wewe uwe mmoja wa Viongozi wa Dini Washauri wa Rais Magufuli utakubali?
Kiongozi wa Dini: Ha ha ha! Kwa nini nikatae kama kuna uhitaji?
Askofu Mwamakula: Haitakuwa hatari kwako?
Kiongozi wa Dini: Ha ha ha! Kwa kuwa nitakuwa nashauri serikali haitakuwa hatari.
Askofu Mwamakula: Mheshimiwa Lissu akiingia madarakani utakuwa tayari kuwa mshauri wake?
Kiongozi wa Dini: Hapo hakuna shida.