G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 12,408
- 39,477
Hatimaye mzee Kingunge Ngombale Mwiru kada wa muda mrefu CCM amekiri kuwa hakuwa anafahamu vyema mambo yanayoendelea ndani ya CCM na kukiri wazi kuwa alipotoshwa na mtia nia mmoja wa urais na kundi lake kupitia CCM.
Mzee Kingunge amekiri kusononeshwa na alichokiita kuwa waraka wa makubaliano alioletewa ambao alidhani kuwa umetoka kwa kiongozi mmoja wa juu serikalini ukionyesha kumuunga mkono mtia nia huyo. Aidha mzee Kingunge anasema kuwa baadaye alibaini kuwa amechezewa sarakasi na mtia nia huyo. Mzee Kingunge amedai kuwa kwa sasa atakaa kimya kuhusiana na mambo ya urais ndani ya CCM hadi hapo mgombea wao atakapopatikana.
Mzee Kingunge amekiri kusononeshwa na alichokiita kuwa waraka wa makubaliano alioletewa ambao alidhani kuwa umetoka kwa kiongozi mmoja wa juu serikalini ukionyesha kumuunga mkono mtia nia huyo. Aidha mzee Kingunge anasema kuwa baadaye alibaini kuwa amechezewa sarakasi na mtia nia huyo. Mzee Kingunge amedai kuwa kwa sasa atakaa kimya kuhusiana na mambo ya urais ndani ya CCM hadi hapo mgombea wao atakapopatikana.