Kingunge kasema jambo muhimu, CCM sasa ni Obsolutely Power Corrupts

Kingunge kasema jambo muhimu, CCM sasa ni Obsolutely Power Corrupts

Chakaza

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
41,011
Reaction score
74,659
Lazima tukubali Mzee Kingunge anazijua sana siasa za nchi hii kwani ameshiriki kwa kipindi kirefu sana. Almost 61 years yupo katika ulingo huo wa siasa katika nafasi nyingi. Tena sio katika ushiriki ule wa "Ndio mzee" bali pia wa misukosuko ndani ya chama chake na serikali kama alivyoeleza mwenyewe jana.

Kwa maana hiyo TANU na CCM anaijua zaidi kuliko Kikwete, Kinana na wengine wengi wakiwamo wakina Msekwa na Warioba. Lakini katamka wazi kuwa CCM ya sasa sio ile iliyokuwa na misingi yake ya awali bali hii imebinafsishwa na hajui kwa manufaa ya nani (ingawa nadhani anajua).

Kauli mbiu yake ni kuwa CCM imekuwa OBSOLUTELY POWER CORRUPTS na haiwezi tena kuongoza, ni sawa na mtu anayepanda mlima na kisha akaishiwa pumzi inambidi ashuke tuu. Maneno hayo kwa wale wanaoendelea kuiunga mkono CCM wameyaelewa? Mkongwe kasema chama chao ndio kimefikia mwisho iweje nyie tena wengi wamezaliwa kikiwepo wao wasimuelewe huyu mzee?

ONDOKENI HUKO SASA, ASIYESIKIA LA MKUU ........!
 
mzee katuonea hurumu,speed ya maendeleo haiendani na miaka ccm imekaa madaraka,kasema wa tz weng wanataka mabadiliko
 
Ccm imebinafsishwa, kama wewe ni mmoja wa wanaoitetea hakikisha una shea yako usitoke povu la bure
 
Mzee kajua CCM mbaya baada ya lowasa kukatwa?
 
CCM ya sasa inamilikiwa na WAMA

Na hilo Mzee alikuwa analisema kwa kutumia nahau za kiutu uzima ili kutunza heshima. Ila kamaliza vizuri kwa kusema "chama kinaajiri Mavuvuzela wawe wanatukana watu majukwaani na hawakemewi"
Nadhani hilo limewaudhi wazee wengi na wale vijana wenye ufahamu kwani chama kikongwe hakiwezi kuwa na tabia za kichokoraa kama hizo.
 
Mzee kajua CCM mbaya baada ya lowasa kukatwa?

Wenye akili zetu tume muelewa vizuri saana.

Sababu alizotoa hazihitaji hata elimu ya chekechea kumuelewa mzee, ni kuwa na masikio yanayo weza kusikia tu basi.

Katoa sababu za msingi sana !
 
He is no more a threat to ccm@hapa kazi tuuuu

Majibu mepesi katika hoja ngumu. Wewe unasema sio threat, lakini habari ziko wazi kuwa viongozi wako wamekesha usiku kujadili repercusions za tukio hilo ambalo ni pigo. Kingunge alikuwa amebaki kama Icon ya chama ndani ya nchi na nje.
Nenda kawaulize ANC ya South Africa ambacho ni chama rafiki na CCM watakueleza vizuri kuhusu Kingunge na mambo ambayo wewe huyajui kuhusu yeye na pengine vijana wengine ndani ya chma kama Nape.
 
Tunahitaji wazee wenye maamuzi magumu kama Kingunge. MUNGU akutangulie katika mabadiliko yasiyozuilika tena. asante mzee
 
Yaani hata hayati Mzee nyerere angekuwepo ajivue ugamba kuna makinda wangethubutu kusema hana threat kwa chama!!!!

Hii ni kielelezo uvccm hawana adabu kwa wazee waasisi.
 
Back
Top Bottom