King'amuzi kwenye LCD, LED na PLASMA TV vipi?

King'amuzi kwenye LCD, LED na PLASMA TV vipi?

JamboJema

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2011
Posts
1,143
Reaction score
209
Tuliambiwa LCD, LED na PLASMA Tv zina ving'amuzi ndani na hivyo wakizima hizo 'analojia' tutaweza kudaka matangazo ya dijitali bila kutafuta king'amuzi kingine. Tangu waanze kuzima TCRA hawaongelei tena hili, au hata kutupatia elimu tufanyeje ili tuvitumie ving'amuzi vilivyo 'built - in'. Anayefahamu naomba anivushe tuta hili.
 
TV inaweza kuwa LCD, LED ama Plasma haina uhusiano na Kuwa Digital TV ...cha msingi kama TV yako ni ya digital ndio uongelee swala la kukwepa king'amuzi.
 
Kulikuwa na upotofu,tokea Mwanzo!Unaposema digital TV transmission maana yake ni kuwa baada ya kila TV station kuwa na frequency yake,Inakuwa kwamba TV zote ata kama zipo 500 katika Nchi Moja unazirusha kwa kutumia frequency moja tu.Mfumo kama ZUKU,DSTV au COMCAST wa USA unatumia just one frequency kurusha zaidi ya TV station 200 kwa wakati mmoja.Kingamuzi ni kifaa chenye uwezo wa kungamua na kumsaidia mtumiaji kuchagua TV station ipi ya kuangalia na inakuwa na system ya kujifunga kama ujalipia(zipo nchi zina vingamuzi vya Bure kwa raia wao).Sasa kuna model ya TVs zinakuja na Vingamuzi vimejengewa ndani yake,kwa nchi maalumu kwani kila nchi inasystem ya kingamuzi chake,Star Media wana TV zenye Vingamuzi vyenye system ya Tanzania
 
Hivi wananchi wakishitaki serikali kwa kuwanyima uhuru wa kupata habari hivi ving'amuzi si vitapigwa chini?
 
Nina TV yangu ambayo imejengewa king'amuzi ndani yake. Hivi nikiileta Tanzania ina maana sitaona tv? Ina specifications za kutumia king'amuzi hicho nchi zote za Ulaya. Kama sivyo, itabidi ninue king'amuzi cha kampuni fulani hapo TZ? Kama itakuwa hivyo, naona kuna kamchezo ambako wananchi wanachezewa na ndio maana hawataki kamwe kurudisha matangazo ya analojia!
 
Kulikuwa na upotofu,tokea Mwanzo!Unaposema digital TV transmission maana yake ni kuwa baada ya kila TV station kuwa na frequency yake,Inakuwa kwamba TV zote ata kama zipo 500 katika Nchi Moja unazirusha kwa kutumia frequency moja tu.Mfumo kama ZUKU,DSTV au COMCAST wa USA unatumia just one frequency kurusha zaidi ya TV station 200 kwa wakati mmoja.Kingamuzi ni kifaa chenye uwezo wa kungamua na kumsaidia mtumiaji kuchagua TV station ipi ya kuangalia na inakuwa na system ya kujifunga kama ujalipia(zipo nchi zina vingamuzi vya Bure kwa raia wao).Sasa kuna model ya TVs zinakuja na Vingamuzi vimejengewa ndani yake,kwa nchi maalumu kwani kila nchi inasystem ya kingamuzi chake,Star Media wana TV zenye Vingamuzi vyenye system ya Tanzania
Asante kwa taarifa hii.
 
Back
Top Bottom