King'amuzi cha Dish cha Startimes

King'amuzi cha Dish cha Startimes

Tony Laurent

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2011
Posts
6,391
Reaction score
8,294
Nina mpango wa kunua King'amuzi cha Startimes kinachotumia dish. Hivyo naomba kwa yeyote ambaye ameshanunua na anakitumia anijulishe kuhusu ubora wake. Je, hakisumbui kama vile vingine vinavyotumia antenna?
 
Mimi mwenyw nasubiri jibu hili, pia watuambie na bei yake ipo vp
 
sina data za kutosha ila ni majanga kwa kweli azam bado yupo vizuri hawa jamaa wamekuja na vifurushi watu hapana taka
 
mmm nacho kipo?
mi najua kinachotumia antena
 
Nakushauri kwa ubora wa picha na vipindi vizuri ununue kisimbusi cha azam
 
Azam nao wameshaanza uduwansi kama wengine, kwanza walisema free chanel ni 16, baadaye wakaziondoa za kenya na uganda na kubakiza za bongo tu kama sita hivi, sasa wanaondoa hata hizo sita na hivyo kufanya azam isiwe na chaneli yoyote ya bure, kinyume na maagizo ya Tcra, bongo bongolala.hili ni shamba la bibi, usipovuna hapa utavuna wapi pengine?
 
Ngoja tusubiri maelezo ya waliovitumia tuone kama kuna jipya, maana nlichosikia star media wameinunua starsat kampuni ya south africa ambayo imefirisika kwa sasa, hivyo huduma zao za tv zitaongezeka kwa star times, sasa kama kuna aliyetumia atatupa majibu mazuri zaidi
 
Nina mpango wa kunua King'amuzi cha Startimes kinachotumia dish. Hivyo naomba kwa yeyote ambaye ameshanunua na anakitumia anijulishe kuhusu ubora wake. Je, hakisumbui kama vile vingine vinavyotumia antenna?

hamnaga huduma ya Dish mbovu kaka wewe nunua labda kama unauliza channel zao ingia hapa chini za FTA na PAID wamezianisha

http://www.lyngsat.com/packages/startimes.html
 
Wengi wanapenda Star times kwa ajili ya chanel ya TV 1!

Hii chaneli imetoa mvuto wa pekee kwani star times ni majanga!

Watanzania bwana, hiyo TV 1 yenye vipindi vya miaka mitatu iliyopita vya MTV Base na E!?
Startimes mbona ina channel nyingi nzuri za music, movies na vipindi vya kawaida?
Wengi wa wanaolalamikia Startimes huwa wale wa habari za mtaani.
Mimi nina DStv na Startimes, sitaki kuiponda Startimes kuwa eti majanga.
 
Watanzania bwana, hiyo TV 1 yenye vipindi vya miaka mitatu iliyopita vya MTV Base na E!?
Startimes mbona ina channel nyingi nzuri za music, movies na vipindi vya kawaida?
Wengi wa wanaolalamikia Startimes huwa wale wa habari za mtaani.
Mimi nina DStv na Startimes, sitaki kuiponda Startimes kuwa eti majanga.

Ishu ni accessibility!

Watu wana admire kwa vile haikuwahi kutokea katika chanel ambazo zimezoeleka!

Dstv haikuwa rahisi kuipata (afford), wengi walikuwa na madishi ya bure yenye chanel kibao za mashariki ya kati na mbali!
 
Kwanza sijajua hata angle waliyoingia maana kama ni degree 10' pale ipo star time kwa C-BAND.
 
Wadau vipi Visimbusi vya startimes vinavyotumia dish? ni HD na vina record pvr?
 
Back
Top Bottom