King'amuzi cha continental

King'amuzi cha continental

Linamo

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2011
Posts
9,976
Reaction score
24,498
Naomba mnijulishe uzuri wa king'amuzi cha continental kwa mnaokitumia,bei yake,malipo yake na channel zake japo kwa uchache.Kwenu wana JF.
 
Sifa kubwa ni kusifia sana ccm mafisadi na viongozi wake, kumwonyesha Dialo kila wakati na kugeuza mabaya kwa wananchi kuwa mazuri pasipo sababu n.k
 
Bado hakipo, hao jamaa sijui wanafanya nini! Startimes wanapeta tu wao wamelala! Kama kuna muhusika humu awaambie wakuu wake waache ujinga tumeichoka Startimes, wafanye haraka kuingia sokoni! watu wanapigika
 
Bado hakipo, hao jamaa sijui wanafanya nini! Startimes wanapeta tu wao wamelala! Kama kuna muhusika humu awaambie wakuu wake waache ujinga tumeichoka Startimes, wafanye haraka kuingia sokoni! watu wanapigika
Kipya kinyemi!
Usimtukane mamba kabla hujavuka mto.
 
Mara nyingi kinamuonyesha Le mutuz akiwa na wadada huku amelegeza macho...
 
Sifa kubwa ni kusifia sana ccm mafisadi na viongozi wake, kumwonyesha Dialo kila wakati na kugeuza mabaya kwa wananchi kuwa mazuri pasipo sababu n.k mmh una uhakika?
 
Bado hakipo, hao jamaa sijui wanafanya nini! Startimes wanapeta tu wao wamelala! Kama kuna muhusika humu awaambie wakuu wake waache ujinga tumeichoka Startimes, wafanye haraka kuingia sokoni! watu wanapigika Startms hakuna kitu..
 
hiv vya startmz vinaproblem? Yani havifai bora kutokuwa nacho kabisa hawa jamaa hakuna kitu ngoja tuangalie hawa continental na hicho cha digtek...
 
Bado hakipo, hao jamaa sijui wanafanya nini! Startimes wanapeta tu wao wamelala! Kama kuna muhusika humu awaambie wakuu wake waache ujinga tumeichoka Startimes, wafanye haraka kuingia sokoni! watu wanapigika

Mijitu mingine utafikiri haikusoma A B C D za sales and marketing ! Unatangaza vp kitu ambacho hakuna !? Ndio hivi hivi Mengi alitangaza ile pombe yake "Hakuna Matata" wakati ametoa order ya kuletewa Mashine za uzalishaji, mpaka anaanza kuzalisha na kuuza, watu wamechoka. Ngoma iko fail sokoni !
 
Kama kuna uwezekano wa ving'amuzi mbadala ni bora tukajulishwa mapema hivi vya startimes havina kiwango. Na bei zake ziwekwe wazi na channels zitakazoonyeshwa pia na kama kuna vituo mikoani hivi vyote ni vitu muhimu tukajulishwa ili tuweke maamuzi sahihi.
 
hiv vya startmz vinaproblem? Yani havifai bora kutokuwa nacho kabisa hawa jamaa hakuna kitu ngoja tuangalie hawa continental na hicho cha digtek...

Yaani mi nimeacha kulipia kabisa, manake ujinga mtupu nabaki naangalia taarifa ya habari tu kwny hizo TV zao tano! Yaani inakera mpaka basi
 
tatizo lao wanatoa matangazo bila kuwa na ving'amuzi husika
 
Bora wewe unaweza kuona taarifa ya habari mimi nina mwezi sipati chochote ilianza vizuri ikawa inakata kata mara gii mpaka na leo na nilikuwa nimelipia ile miezi mitatu waliyo kuwa wanatangaza ya ofer one month.
 
Back
Top Bottom