Kinana: Tunataka CCM ya Nyerere na Karume...

Kinana: Tunataka CCM ya Nyerere na Karume...

ebaeban

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
2,205
Reaction score
2,707
Kinana na kundi lake hawaiwezi CCM ya Nyerere.

Katibu Mkuu wa CCM
, Abdulrahman Kinana akiwa kwenye
ziara ya Mkoa wa Mbeya mwishoni mwa mwaka jana alitangaza waziwazi kwamba yeye anataka CCM ya waanzilishi, yaani ya Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume irudi.



Anasema CCM lazima ipinge unyonyaji, ukabaila uzembe na ufisadi kwa nguvu zote.

Anasema viongozi wa CCM lazima waitishe vikao vyote vya kikatiba kuanzia mashina, matawi, kata, wilaya na mikoa kama ilivyo kwa vikao vya kitaifa.


1.CCM ya Nyerere ilisema nini kuhusu Lowasa na CCM ya kinana inafanya nini kuhusu Lowasa

2. CCM ya Nyerere ilisema nini kuhusu ujangiri na kwa kuonyesha kwamba haikuwa na mzaha kuhusu hilo ilimfanya nini Mbunge wa Songea mjini bwana Kazeharabi? Si Kinana huyo huyo anaambiwa akae mbali na Tembo, Kinana huyo huyo aliwahi sema meli yake ila pembe siyo za kwake, pia aliwahi sema kuwa mchuzi alikunywa ila nyama hakula

3.CCM ya Nyerere alikuwa inafanya nini kuhusu wagombea wasio na chembe ya uadilifu kama akina ADEN RAGE au ANDREW CHENGE? CCM ya Nyerere ilikuwa nan uvumilivu na watu hao, aulizwe RAGE CCM ya Nyerere ilimfanya nini pale alipoongoza kura za maoni Tabora mjini mwaka 1995.

4. CCM ya Nyerere ilikuwa ni ya wanyonge, wakulima , wafanyakazi , wavuvi na wakwea minazi, akane Kinana CCM yake kama haijawa ya matajiri , wafanyabiashara na wakwepa kodi.Wanyonge hawana lao katika CCM ya Kinana hebu aje hapa abishe.

Kinana tafadhari ukome kulinganisha CCM yako na ya Nyerere.
 
Mwache apige kelele akidhani anayoyasema tunayaamini,tunawasubiri mwakani ndio atajua kama tulikuwa tunamsikiliza nakumngojea kwa hamu
 
......4. CCM ya Nyerere ilikuwa ni ya wanyonge, wakulima , wafanyakazi , wavuvi na wakwea minazi, akane Kinana CCM yake kama haijawa ya matajiri , wafanyabiashara na wakwepa kodi.Wanyonge hawana lao katika CCM ya Kinana hebu aje hapa abishe.

Kinana tafadhari ukome kulinganisha CCM yako na ya Nyerere.


Hapo penye nyekundu SWADAKTA Mr. Bulayi
 
Ccm ya kinana inawasumbua sana lazima mtaijua tu hata mkifanya vipi lazima awazamishe tu.
 
Ngoja mgambo wa Lumumba a.k.a LUMUMBA BK7 waibuke huko waliko!!!!
 
CCM ni moja tu. Hakuna CCM ya kinana wala ya Nyerere. ila kule CHADEMA ndo kuna CHADEMA CHUMBANI na CHADEMA SEBULENI
 
[/COLOR]
Hapo penye nyekundu SADAKTA Mr. Bulayi

Sahihisho; ungeandika SADAKTA Bulayi kwa sababu Bulayi ina hadhi kubwa kuliko MR. (Samahani lakini maana hiyo ndiyo nahau na usahihi wa lugha yenye jina hilo)
 
magaidi watahangaika sana kumchafua kinana lakini hachafuliki, mtaishia kunywa gongo zenu na viroba mpaka mchubuke midomo.
 
Nilivyoona picha za wanafiki wakiwa wamepanda treni, kula chakula na wananchi, kupanda bodaboda nikadhani usanii uliishia kwenye picha tu kumbe hata maneno waliyoyasema yalikuwa ni ya kisanii kiasi hiki!!!!?
 
Blayi wa Mpwapwa kununua majumba dubai kwa pesa ya ruzuku ya chama
kuvinjari na mke wa mtu ulaya kwa pesa ya ruzuku ya chama
kukatisha ziara za wabunge wa viti maalumu na kwenda nao dubai kuponda raha
kurusha helikopta kwa mamilioni ya fedha wakati chama hakina ofisi hata ya makao makuu ni ya kusaidiwa
chadema ni janga na ni genge la waporaji
 
Last edited by a moderator:
Hakuna chama cha siasa hapa Tanzania zaidi ya CCM, zingine ni saccos tu, magenge ya walaghai na waganga njaa
 
Jengo linawasaidia nn wanachi wa vijijini amabao wana kiu ya kusikia maovu ya CCM. watanzania simiyu kule ndani au Nyakanazi kule Biharamulo ofisi ya lumumba imewasaidaje? hivi ukilinganisha madudu ya CDM uliyoweka hapo juu tuyapime na madudu ya CCM alafu twende kwa wananchi. nani atakimbizwa na mawe?
 
kununua majumba dubai kwa pesa ya ruzuku ya chama
kuvinjari na mke wa mtu ulaya kwa pesa ya ruzuku ya chama
kukatisha ziara za wabunge wa viti maalumu na kwenda nao dubai kuponda raha
kurusha helikopta kwa mamilioni ya fedha wakati chama hakina ofisi hata ya makao makuu ni ya kusaidiwa
chadema ni janga na ni genge la waporaji

1.Ndege kupishana angani ingine ikiingia inchini na condom kwa msaada wa marekani na ingine ikitoka inchini imesheheni vinoo vya thahabu toka barrick gold mine.
2.Ndege ya jeshi la inchi ingine ikipaa toka KIA na twiga
3. Wabunge wakiwa bungeni wanasinzia tu halafu wanakuja na hoja ya kulipwa tshs.million 160 kwa miaka 5 tu
4. Watoto wa vigogo wa CCM wakijazana benki kuu bila kuwepo vijijini kufundisha shule za msingi
5.Wanainchi kuporwa ardhi yao ya urithi toka kwa babu zao na kupewa wawekezaji mchana kweupe
6.Vigogo kuweka wigo kwenye fukwe ambazo ni gift of nature, leo hii fukwe zinataifishwa na wenye nazo
7. Kero kwa wanainchi ya manoti mabovu ya shs 500, na 2000 zitakanazo na rushwa kwa wazabuni wasio na uwezo

Utaifakwanza bado hujitambui?
 
Ni sawa na kulinganisha kichuguu na mlima.sisiemu hii ni genge la wanyan'ganyi.
 
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa kwenye ziara ya Mkoa wa Mbeya
mwishoni mwa mwaka jana alitangaza waziwazi kwamba yeye anataka CCM ya waanzilishi,
yaani ya Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume irudi.



Anasema CCM lazima ipinge unyonyaji, ukabaila uzembe na ufisadi kwa nguvu zote.


Anasema viongozi wa CCM lazima waitishe vikao vyote vya kikatiba kuanzia mashina,
matawi, kata, wilaya na mikoa kama ilivyo kwa vikao vya kitaifa.



Viongozi hao wa CCM, Kinana anasema, lazima watoke ndani ya CCM na kusisitiza kwamba
makatibu wa mikoa wawe na utaratibu wa kuwapendekeza wanaofanya vizuri kupanda vyeo
kuwa makatibu wa wilaya, hali kadhalika wa wilaya lazima wawapendekeze wale wa kata ili
wapande vyeo wanaofanya vizuri.
 
Ccm kwa sasa iko imara kama jiwe wapinzani wataisoma namba tu.
 
Back
Top Bottom