Kinana aunguruma Sumbawanga, sasa hivi...!

Kinana aunguruma Sumbawanga, sasa hivi...!

TandaleOne

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2010
Posts
1,644
Reaction score
709
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Mhe. Abdurahaman Kinana anazungumza katika wilaya ya Sumbawanga Mjini ambako amezungumzia juu ya suala la kero za Usafiri na Barabara, ambapo amesema tayari serikali imeshatenga fedha ya kutosha kwa ajili ya barabara hiyo ambapo tayari baadhi ya makandarasi wanaendelea na ujenzi wa makaravati tayari kwa kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Pia Mheshimiwa kinana amezungumza juu ya suala la Uhifadhi wa mazingira ambapo amewataka wachina ambao wanaendesha zoezi la uchimbaji wa madini katika mbuga ya katavi kuondoka mara moja katika hifadhi hiyo na kusisitiza kuwa suala la uhifadhi wa mazingira ni jambo muhimu na kimsingi linaendana na siasa ya CCM ya kupambana na umasikini, alisema " Moja kati ya malengo na maudhui ya CCM ni kuona kwamba matumizi ya utajiri wa taifa yanatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa jitihada za kuondoa Umasikini, Ujinga na Maradhi" alimalizia kueleza kuwa Mazingira ni nyenzo muhimu ya maendeleo na suala mtambuka, ambalo linagusa sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Kisha Mheshimiwa Kinana alizungumza juu ya suala la uwezeshaji wa wananchi kiuchumi na ujenzi wa msingi wa uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegemea hasa kutokana na rasilimali zetu akisisitizia zaidi juu suala la kilimo na utekelezaji wa sera ya kilimo kwanza. Akahimiza vijana kuchakalika na kutumia kikamilifu fursa ya kijiografia ya sumbawanga ambapo hupata mvua nyingi na ya kutosha.

Hivi sasa Mheshimiwa Nape Nnauye, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Idara ya itikadi na Uenezi anashambua jukwaa...,updates zaidi hivi punde...!
 
mBONA MDA WA KUHUTUBIA UMEISHA MAANA NI SAA 12:22, wangekuwa wapinzani nadhani mabomu yangukuwa yanalindima
 
Haya ndio mapya ya katibu mkuu mpya au kuna mengine ya kusisimua aliongea TandaleOne.
 
mBONA MDA WA KUHUTUBIA UMEISHA MAANA NI SAA 12:22, wangekuwa wapinzani nadhani mabomu yangukuwa yanalindima

Huku ni sumbawanga, majira ya huku ni tofauti.,bado ni kweupe na mkutano unaendelea ila karibu utafungwa kwani hivi sasa anaongea mzungumzaji wa mwisho.
 
TandaleOne Haya uliyoleta siamini kama yana ukweli maana tangu upotoshe ile orodha ya viongozi wa chadema vyuo vikuu nimekuwekea nyota ya kutokukuamini tena japo hata saa mbovu huongea ukweli mara mbili kwa siku.
 
Last edited by a moderator:
Haya ndio mapya ya katibu mkuu mpya au kuna mengine ya kusisimua aliongea TandaleOne.


Ameeleza pia juu ya mwelekeo wa sera za CCM katika miaka ya 2010 hadi 2020, na kutoa ufafanuzi wa kutosha katika baadhi ya masuala muhimu yanayoigusa jamii hiyo likiwemo suala la ardhi.
 
Haya ndio mapya ya katibu mkuu mpya au kuna mengine ya kusisimua aliongea TandaleOne.
Huko Mtwara ameishangaa serikali ya CCM kutopandisha na kusimamia bei ya korosho; na Kinana huyo huyo anaisemea serikali ya CCM kuhusu mikakati ya kujenga barabara. SASA, ni wakati gani gani anaisimamia serikali na wakati gani anakuwa mtetezi wa serikali hiyo hiyo. Au ndio ndimi mbili zenyewe tunazozisikia kila siku?

Au ndo anazitekeleza sera za CDM chini kwa chini?
 
ha ha ha ndo wameamka saizi? Kazi wanayo wamesha poteza mvuto kwa wananchi na kwa mtu kama naye jua madudu ya ccm na ya kinana na nikimuona anadanganya watu kwa propaganda za kipuuzi naumia sana na roho yangu inaniuma
 
TandaleOne Haya uliyoleta siamini kama yana ukweli maana tangu upotoshe ile orodha ya viongozi wa chadema vyuo vikuu nimekuwekea nyota ya kutokukuamini tena japo hata saa mbovu huongea ukweli mara mbili kwa siku.

Kimsingi hakuna aliyejitokeza kupinga kuwa wale hawakuwa viongozi wa Chadema katika vyuo husika.,alichofanya makene ni kutaja majina ya viongozi wengine wakiwemo wenyeviti, makatibu, waenezi na watunza fedha na hakukanusha kuwa orodha ile si ya viongozi wa chadema vyuoni bali alisema miongoni mwao si wenyeviti bali hakusema si viongozi.,naomba ufahamu hivyo. Hakuna upotoshaji juu ya jambo hilo.
 

Huko Mtwara ameishangaa serikali ya CCM kutopandisha na kusimamia bei ya korosho; na Kinana huyo huyo anaisemea serikali ya CCM kuhusu mikakati ya kujenga barabara. SASA, ni wakati gani gani anaisimamia serikali na wakati gani anakuwa mtetezi wa serikali hiyo hiyo. Au ndio ndimi mbili zenyewe tunazozisikia kila siku?

Au ndo anazitekeleza sera za CDM chini kwa chini?

Wajibu wa Chama Cha Mapinduzi kama Chama tawala ni kuisimamia serikali katika utekelezaji wa ilani ya chama hiko na si kuitetea, kimsingi makosa ya serikali yanatambulika kuwa ni ubovu wa chama kuisimamia na kinachofanyika sasa ni kuhakikisha kuwa serikali inafanya kazi yake kama watekelezaji wakuu wa ilani ya chama tawala.,dont get confused, ielewe nafasi ya CCM katika Serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.
 

Huko Mtwara ameishangaa serikali ya CCM kutopandisha na kusimamia bei ya korosho; na Kinana huyo huyo anaisemea serikali ya CCM kuhusu mikakati ya kujenga barabara. SASA, ni wakati gani gani anaisimamia serikali na wakati gani anakuwa mtetezi wa serikali hiyo hiyo. Au ndio ndimi mbili zenyewe tunazozisikia kila siku?

Mkuu.
Wala usishangae ndio ndimi mbili zenyewe hizo.

Juzi alipo hojiwa kwenye Jenerali on monday anasema hana muarobaini wa rushwa wa haraka ndani ya ccm, mzee Mangula yeye kasema walio toa rushwa na kupata uongozi kwa rushwa wote watang'oka ndani ya ccm katika kipindi cha miezi sita. Hizo ni ndimi ngapi?!

Mukama alisema wanajivua gamba ndani ya siku 90 ilivyoshindikana Nape akasema ni siku 120 hizo nazo ni ndimi ngapi?

Walio kataa kuwa hakuna pesa za epa zilizoibwa baadae wakaja kukubali kuwa zimeibwa. Hizo ni ndimi ngapi?
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Mhe. Abdurahaman Kinana anazungumza katika wilaya ya Sumbawanga Mjini ambako amezungumzia juu ya suala la kero za Usafiri na Barabara, ambapo amesema tayari serikali imeshatenga fedha ya kutosha kwa ajili ya barabara hiyo ambapo tayari baadhi ya makandarasi wanaendelea na ujenzi wa makaravati tayari kwa kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Pia Mheshimiwa kinana amezungumza juu ya suala la Uhifadhi wa mazingira ambapo amewataka wachina ambao wanaendesha zoezi la uchimbaji wa madini katika mbuga ya katavi kuondoka mara moja katika hifadhi hiyo na kusisitiza kuwa suala la uhifadhi wa mazingira ni jambo muhimu na kimsingi linaendana na siasa ya CCM ya kupambana na umasikini, alisema " Moja kati ya malengo na maudhui ya CCM ni kuona kwamba matumizi ya utajiri wa taifa yanatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa jitihada za kuondoa Umasikini, Ujinga na Maradhi" alimalizia kueleza kuwa Mazingira ni nyenzo muhimu ya maendeleo na suala mtambuka, ambalo linagusa sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Kisha Mheshimiwa Kinana alizungumza juu ya suala la uwezeshaji wa wananchi kiuchumi na ujenzi wa msingi wa uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegemea hasa kutokana na rasilimali zetu akisisitizia zaidi juu suala la kilimo na utekelezaji wa sera ya kilimo kwanza. Akahimiza vijana kuchakalika na kutumia kikamilifu fursa ya kijiografia ya sumbawanga ambapo hupata mvua nyingi na ya kutosha.

Hivi sasa Mheshimiwa Nape Nnauye, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Idara ya itikadi na Uenezi anashambua jukwaa...,updates zaidi hivi punde...!

Hili neno Mheshimiwa sasa linatumika vibaya.

Ama tulifute kabisa kulitumia au tupeane semina elekezi nani anastahili kuitwa hivi
 
Huku ni sumbawanga, majira ya huku ni tofauti.,bado ni kweupe na mkutano unaendelea ila karibu utafungwa kwani hivi sasa anaongea mzungumzaji wa mwisho.

jibu la hovyoo kama la sharobaro Tendwa wakati anamtetea Kikwete kwa kukiuka taratibu za uchaguzi
 
Wajibu wa Chama Cha Mapinduzi kama Chama tawala ni kuisimamia serikali katika utekelezaji wa ilani ya chama hiko na si kuitetea, kimsingi makosa ya serikali yanatambulika kuwa ni ubovu wa chama kuisimamia na kinachofanyika sasa ni kuhakikisha kuwa serikali inafanya kazi yake kama watekelezaji wakuu wa ilani ya chama tawala.,dont get confused, ielewe nafasi ya CCM katika Serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Mkuu.
Wala usishangae ndio ndimi mbili zenyewe hizo.

Juzi alipo hojiwa kwenye Jenerali on monday anasema hana muarobaini wa rushwa wa haraka ndani ya ccm, mzee Mangula yeye kasema walio toa rushwa na kupata uongozi kwa rushwa wote watang'oka ndani ya ccm katika kipindi cha miezi sita. Hizo ni ndimi ngapi?!

Mukama alisema wanajivua gamba ndani ya siku 90 ilivyoshindikana Nape akasema ni siku 120 hizo nazo ni ndimi ngapi?

Walio kataa kuwa hakuna pesa za epa zilizoibwa baadae wakaja kukubali kuwa zimeibwa. Hizo ni ndimi ngapi?

Hoja ilikuwa kwa namna ya jicho la Mmohamed Mtoi
 
Siku hizi tuna cabinets ngapi? Kama Kinana anaenda all the way Sumbawanga kuongelea barabara kwanini Magufuli awepo? Naona hatari ya Lumumba kuingilia kazi za mawaziri!
 
MKUU hapa naona kuna kutokuelewa maana ya "... Chama tawala CCM kuisimamia serikali yake...". Katibu mkuu KINANA hana mamlaka ya kuiagiza serikali, kwa kisingizio cha chama kusimamia serikali. CCM kuisimaia serikali siyo kupitia mtu mmoja mmoja, bali vikao:mkutano mkuu, NEC & CC, hivi vina mamlaka ya kuisimamia serikali siyo KINANA mkuu, tunapaswa kuelewa hili. Jambo hili ni sawa na BUNGE kusimamia serikali: MBUNGE mmoja mmoja hana mamlaka ya kutoa maagizo kwa serikali, bali MBUNGE (SOMA IBARA 63 ya KATIBA TZ 1977).

NAKUMBUKA alipoingia Sec Gen MKAMA naye alizunguka nchi nzima na kutoa ahadi "mpya kabisa" na kukoromea serikali, aliitwa na kuambiwa anakosea na akapotelea kusikojulikana. MOJA ya ahadi za MKAMA ni kujenga hospitali ya RUFAA eneo la Kwangwa MUSOMA , yenye pia na chuo kikuu cha afya kama MUHIMBILI, MJINI MUSOMA, na akasema isipojengwa hadi 2015 basi CCM isichaguliwe ... TUNASUBILIA TUONE. KINANA naye anapita mle2, haya bwana: naona hawajajua kuwa CHAMA KUSHIKA HATAMU ILISHAKWISHA ZAMAAAAAAAAAAAAANI ...

Wajibu wa Chama Cha Mapinduzi kama Chama tawala ni kuisimamia serikali katika utekelezaji wa ilani ya chama hiko na si kuitetea, kimsingi makosa ya serikali yanatambulika kuwa ni ubovu wa chama kuisimamia na kinachofanyika sasa ni kuhakikisha kuwa serikali inafanya kazi yake kama watekelezaji wakuu wa ilani ya chama tawala.,dont get confused, ielewe nafasi ya CCM katika Serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.
 
Siku hizi tuna cabinets ngapi? Kama Kinana anaenda all the way Sumbawanga kuongelea barabara kwanini Magufuli awepo? Naona hatari ya Lumumba kuingilia kazi za mawaziri!

Ni kutimiza wajibu wa chama kwa serikali.,kwa maana kuisimamia lakini pia ni kufanya kazi ya chama nje ya chama kwa maana ya kuwafikia wananchi na kuwaeleza kuwa tumekuja kuyatekeleza na kuyasimamia yale tuliyoyaahidi kwenye majukwaa wakati tukiomba kura. Ni uelewa mdogo kudhani kuwa chama kinaingilia utendaji wa serikali, kifupi ni kutoelewa nafasi ya chama kwa serikali na nafasi ya serikali kwa wananchi...!
 
Back
Top Bottom