Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,637
KURUKARUKA kwa maharage ndio kuiva kwake. Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Abdulrahman Kinana, alirukaruka weeee!
Mwisho, Kinana amejitokeza kumuomba radhi Rais John Magufuli kwa maneno aliyotamka dhidi yake.
Kinana amesema kuwa ‘anadhani’ alivuka kiasi baada ya kukereka, kwa hiyo akatamka maneno ambayo hayakuwa mazuri kwa Rais Magufuli, hivyo amemuomba radhi Rais Magufuli binafsi na wote waliokwazika.
Kinana alizungumza nini? Bila shaka ni ile sauti yake iliyovuja akizungumza na aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye. Hilo ni tukio la Julai 2019.
Mazungumzo ya Kinana na Nape yalifuatia waraka wa malalamiko ambao Kinana aliuandika kwa kushirikiana na Katibu Mkuu mwingine wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba. Waraka ni wa Julai 2019.
Kinana na Makamba waliandika waraka kwenda kwa Katibu wa Baraza la Wazee CCM, lakini waliusambaza kwenye mitandao ya kijamii.
Malalamiko yao yalihusu ukimya wa viongozi wa CCM, kipindi ambacho wao walikuwa wakishambuliwa na mwanaharakati mtetezi wa Rais Magufuli, Cyprian Musiba.
Kwa maelezo yao, Kinana na Makamba walidai kuwa Musiba amekuwa akiwashambulia na kuwachonganisha na Mwenyekiti wa CCM na wanachama wengine, kwa kuwapa jina la uasi na wahujumu wa chama.
Walisema kwa mshangao, kwamba wao wakiwa nyumbani kwao, bila mamlaka yoyote, wanawezaje kumhujumu Mwenyekiti wa CCM?
Zikafuata zama za sauti za Kinana na Nape, Makamba na mwanaye Januari, William Ngeleja na Nape, vilevile Bernard Membe, kuvuja mitandaoni wakimteta vibaya Rais Magufuli. Hayo ni mambo ya Julai 2019.
Kisha zikaja zama za kuomba radhi; Nape, Ngeleja na Nape waliomba msamaha Agosti 2019. Makamba, Kinana na Membe walibaki kimya.
Kilichofuata; Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), iliagiza Makamba, Membe na Kinana waitwe kwenye kamati ya Maadili. Baada ya kuitwa, Makamba aliomba radhi na kusamehewa. Hiyo ni Februari 2020.
Kinana hakuomba radhi, akapewa adhabu ya kifungo cha kutogombea nafasi yoyote CCM kwa kipindi cha miezi 18, Membe alifukuzwa uanachama CCM. Hukumu hiyo ilitangazwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Humphrey Polepole Februari 2020.
TUJADILI
Kwa nini Kinana hakuomba radhi muda wote na aombe sasa? Ina maana siku zote hizo Kinana hakuwa amegundua kama alimkosea Rais Magufuli? Tangu Julai 2019.
Kweli, Kinana hata baada ya kukutana na wazee wenzake katika kamati ya Maadili, hakuona kosa lake na kushindwa kuomba radhi mpaka imepita takriban miezi mitatu? Alikutana na kamati ya Maadili Februari 2020.
Hivi karibuni, mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, alimuomba radhi Kinana kwa matamshi yake aliyowahi kuyatoa bungeni na kwenye mikutano ya hadhara, akimhusisha Kinana na kashfa za ujangili.
Siku chache baada ya Kinana kuombwa radhi na Msigwa, ndio na yeye amemuomba radhi Rais Magufuli. Je, alikuwa anangoja Msigwa amuombe radhi ndipo na yeye amuangukie Rais Magufuli? Au baada ya kuombwa radhi na Msigwa ndio na yeye amegundua uungwana wa kuomba radhi?
Inafahamika kuwa pamoja na tofauti za kisiasa kati ya Msigwa na Rais Magufuli, lakini ni ndugu. Familia zao zimeoleana. Kwa kuzingatia undugu huo, kuna uhusiano wowote wa ombi la radhi alilotoa Msigwa kwa Kinana, kisha Kinana kwa Rais Magufuli? Au imetokea tu?
Raia wa 32 wa Marekani, Franklin Roosevelt alipata kusema kuwa katika siasa huwa hakuna ajali. Ukiona kitu kimetokea, unaweza ‘kubeti’ kwamba hivyo ndivyo ilivyopangwa.
Je, Kinana kaomba radhi kutoka moyoni au ni katii matakwa ya mazungumzo ya pembeni?
Je, Kinana kwa utashi wake aliona umuhimu wa kumwangukia Rais Magufuli au alifuata ushauri wa waona mbali ambao husema "kwani ukimuomba msamaha utapungukiwa nini?" Walimwengu tunafahamiana.
Je, Kinana kuomba radhi inamaanisha adhabu aliyopewa imemuivisha au msimamo wake umechacha?
Mwisho; kuomba radhi ni uungwana bila shaka Rais Magufuli amemsikia na atamsamehe. Amani itawale.
Credit: Luqman Maloti
Sent using Jamii Forums mobile app
Mwisho, Kinana amejitokeza kumuomba radhi Rais John Magufuli kwa maneno aliyotamka dhidi yake.
Kinana amesema kuwa ‘anadhani’ alivuka kiasi baada ya kukereka, kwa hiyo akatamka maneno ambayo hayakuwa mazuri kwa Rais Magufuli, hivyo amemuomba radhi Rais Magufuli binafsi na wote waliokwazika.
Kinana alizungumza nini? Bila shaka ni ile sauti yake iliyovuja akizungumza na aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye. Hilo ni tukio la Julai 2019.
Mazungumzo ya Kinana na Nape yalifuatia waraka wa malalamiko ambao Kinana aliuandika kwa kushirikiana na Katibu Mkuu mwingine wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba. Waraka ni wa Julai 2019.
Kinana na Makamba waliandika waraka kwenda kwa Katibu wa Baraza la Wazee CCM, lakini waliusambaza kwenye mitandao ya kijamii.
Malalamiko yao yalihusu ukimya wa viongozi wa CCM, kipindi ambacho wao walikuwa wakishambuliwa na mwanaharakati mtetezi wa Rais Magufuli, Cyprian Musiba.
Kwa maelezo yao, Kinana na Makamba walidai kuwa Musiba amekuwa akiwashambulia na kuwachonganisha na Mwenyekiti wa CCM na wanachama wengine, kwa kuwapa jina la uasi na wahujumu wa chama.
Walisema kwa mshangao, kwamba wao wakiwa nyumbani kwao, bila mamlaka yoyote, wanawezaje kumhujumu Mwenyekiti wa CCM?
Zikafuata zama za sauti za Kinana na Nape, Makamba na mwanaye Januari, William Ngeleja na Nape, vilevile Bernard Membe, kuvuja mitandaoni wakimteta vibaya Rais Magufuli. Hayo ni mambo ya Julai 2019.
Kisha zikaja zama za kuomba radhi; Nape, Ngeleja na Nape waliomba msamaha Agosti 2019. Makamba, Kinana na Membe walibaki kimya.
Kilichofuata; Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), iliagiza Makamba, Membe na Kinana waitwe kwenye kamati ya Maadili. Baada ya kuitwa, Makamba aliomba radhi na kusamehewa. Hiyo ni Februari 2020.
Kinana hakuomba radhi, akapewa adhabu ya kifungo cha kutogombea nafasi yoyote CCM kwa kipindi cha miezi 18, Membe alifukuzwa uanachama CCM. Hukumu hiyo ilitangazwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Humphrey Polepole Februari 2020.
TUJADILI
Kwa nini Kinana hakuomba radhi muda wote na aombe sasa? Ina maana siku zote hizo Kinana hakuwa amegundua kama alimkosea Rais Magufuli? Tangu Julai 2019.
Kweli, Kinana hata baada ya kukutana na wazee wenzake katika kamati ya Maadili, hakuona kosa lake na kushindwa kuomba radhi mpaka imepita takriban miezi mitatu? Alikutana na kamati ya Maadili Februari 2020.
Hivi karibuni, mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, alimuomba radhi Kinana kwa matamshi yake aliyowahi kuyatoa bungeni na kwenye mikutano ya hadhara, akimhusisha Kinana na kashfa za ujangili.
Siku chache baada ya Kinana kuombwa radhi na Msigwa, ndio na yeye amemuomba radhi Rais Magufuli. Je, alikuwa anangoja Msigwa amuombe radhi ndipo na yeye amuangukie Rais Magufuli? Au baada ya kuombwa radhi na Msigwa ndio na yeye amegundua uungwana wa kuomba radhi?
Inafahamika kuwa pamoja na tofauti za kisiasa kati ya Msigwa na Rais Magufuli, lakini ni ndugu. Familia zao zimeoleana. Kwa kuzingatia undugu huo, kuna uhusiano wowote wa ombi la radhi alilotoa Msigwa kwa Kinana, kisha Kinana kwa Rais Magufuli? Au imetokea tu?
Raia wa 32 wa Marekani, Franklin Roosevelt alipata kusema kuwa katika siasa huwa hakuna ajali. Ukiona kitu kimetokea, unaweza ‘kubeti’ kwamba hivyo ndivyo ilivyopangwa.
Je, Kinana kaomba radhi kutoka moyoni au ni katii matakwa ya mazungumzo ya pembeni?
Je, Kinana kwa utashi wake aliona umuhimu wa kumwangukia Rais Magufuli au alifuata ushauri wa waona mbali ambao husema "kwani ukimuomba msamaha utapungukiwa nini?" Walimwengu tunafahamiana.
Je, Kinana kuomba radhi inamaanisha adhabu aliyopewa imemuivisha au msimamo wake umechacha?
Mwisho; kuomba radhi ni uungwana bila shaka Rais Magufuli amemsikia na atamsamehe. Amani itawale.
Credit: Luqman Maloti
Sent using Jamii Forums mobile app