Ndugu, Watanzania walio wengi hawatambuani kwa kutumia makabila, otherwise utakuwa unasumbuliwa na fikra za kibaguzi ambazo kwa sasa dhambi yake inavitafuna baadhi ya vyama vya siasa mpaka vimeamua kulikimbia jina lake linalotambuliwa na msajili wa vyama vya siasa na vimeamua kujificha kwenye mwanvuli wa kikundi kinachoitwa UKAWA,Yaani wewe bongolala kweli nani kasahau uhalifu wa huyu msomali kwa tembo wetu.......?? Pocha ni pocha tu asitusahaulishe machungu ya ndovu wetu aisee
Ndugu, Ni kweli UKAWA ni habari ya mjini ndiyo maana hata viongozi wa hicho kikundi wanaenda mijini pekee kufanya mikutano.Si mmesema anaenda kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM? Sasa ya UKAWA yanatoka wapi tena? Hivi na wewe, utaacha lini kutumia Mekako na Diprosoni na maji ya betri?
Kweli UKAWA ndiyo habari ya mjini.
Ndugu, Wananchi wanachokitaka na kukihitaji huwa kinakuwa manifested kwenye sanduku la kura kupitia sera za vyama na Ilani za Uchaguzi.
Sihitaji kukukumbusha nini wananchi wamekuwa wakihitaji kuanzia mwaka 1995 mpaka leo.
Katibu Mkuu, Kinana anakifahamu kile ambacho wananchi wanakihitaji ndiyo maana CCM imeaminiwa na wananchi kuongoza taifa lao.
KINANA AFICHUA MBINU ZA UKAWA
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana amesema Katiba sio kichochoro kwa wapinzani kuingia Ikulu.
Alisema wenye uwezo wa kuwaweka madarakani ni wananchi, lakini sio Katiba, kwani haipigi kura.
Kinana aliyasema hayo juzi wakati anahutubia wananchi wa Kateshi mkoani Manyara ambapo aliyafananisha madai ya Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu kuhoji uhalali wa saini ya Hayati Baba wa Taifa Julius Nyerere na Abeid Karume kwenye Hati ya Muungano ni sawa na mtoto kuuliza uhalali wa cheti cha ndoa cha wazazi wake.
Pia aliongeza kuwa, madai ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kutaka Serikali Tatu ni ndoto wanazoota kuwa huenda Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikaongoza Serikali ya Tanganyika na Chama cha Wananchi (CUF) kikatawala Zanzibar.
Katiba haiweki watu madarakani, wala Katiba haipigi kura, kwani wanaopiga kura ni wananchi.Lakini pia CCM haikatai Katiba mpya kama wapinzani wanavyodai... CCM wanatumia wingi wao bungeni kuweza kuamua Katiba wanayoitaka.
Kwa nini tusijivunie wingi wetu wakati wananchi ndiyo wametupeleka bungeni na kuiweka madarakani Serikali ya CCM? Halafu duniani kote wachache wao wanasikilizwa, lakini wengi ndiyo wanapewa, alisema Kinana.
Kinana alisema madai ya Lissu kudai saini za Nyerere na Karume sio halali, hizo halali alizionea wapi wakati yeye alikuwa mtoto mdogo na kufananisha kitendo hicho na baba mwenye watoto na wajukuu baadhi ya watoto wake kudai uhalali wa cheti cha ndoa na mkewe.
Madai ya wapinzani hasa Tundu Lissu kudai Hati ya Muungano si halali ni sawa na mtoto kumuuliza baba yake ambaye tayari ana wajukuu, uhalali wa ndoa yake na mama yao. Lakini yeye anasema saini hizo sio halali, saini halali aliziona wapi wakati huo anasoma shule ya msingi. Lakini pia UKAWA wanadhani kukiwa na Serikali tatu, CHADEMA wataongoza Tanganyika, CUF Zanzibar na Serikali ya Muungano itaachiwa CCM.
Halafu wananchi, suala la muungano kwenu sio muhimu, umuhimu ni kupata huduma za jamii kama maji, elimu, afya na barabara.
"Nawashauri wananchi wa Hanang achaneni na siasa zisizo na tija kwenu, bali fanyeni kazi muweze kujiongezea kipato, hata kama Katiba mpya itakuwepo haiwezi kubadilisha maisha yenu kuwa mazuri bila kufanya kazi, alisema.
Nape hujambo povu linakutokaNdugu, Wananchi wanachokitaka na kukihitaji huwa kinakuwa manifested kwenye sanduku la kura kupitia sera za vyama na Ilani za Uchaguzi.
Sihitaji kukukumbusha nini wananchi wamekuwa wakihitaji kuanzia mwaka 1995 mpaka leo.
Katibu Mkuu, Kinana anakifahamu kile ambacho wananchi wanakihitaji ndiyo maana CCM imeaminiwa na wananchi kuongoza taifa lao.
Ukawa ni ugonjwa Wa fikra kila siku wanatoka na kiroja kipya ni watu wanaowadaa watanzania hawana lolote
Kinana is talking the reality and the reason for CCM being against three tier country system of governments. Unfortunately he pimp himself and his party in the thought that they will lead in the Union governmen, teh teh teh. How come if the majority would have given the opposition the leadership to the federal states and not the federation itself? Obviously the Federal Government will be having a GNU structure.
Hongera Kinana for revealing the 'secret' why CCM does not want 3 government system!!! :clap::clap: Ritz, FaizaFoxy, mfumo, Polite
Ndugu, Mimi siko hapa kubishana. Kama wewe uko hapa kujenga ubishi, basi mimi siyo mmoja wao.
Kila mbunge aliyeko bungeni yuko kisheria na wale ambao walishindwa katika chaguzi walishindwa kisheria. Kama unajenga hoja kwa kutumia hisia, basi hilo,ni tatizo lako ambalo halitambuliwi hata kisheria. Ndiyo maana nikakuambia huwezi kusema umeibiwa kura wakati milango ya mahakama iko wazi.
Huwezi kujadili 'ujinga', otherwise utakuwa hufahamu unachokifanya. Vile vile huwezi kujadili 'ujinga' na kudai unauweka hadharani ili wengine pia wauelewe kama vile unaowawekea hawafahamu kama unaojadili ni ujinga. Kujivika kazi ya uchambuzi wa hoja ya 'kijinga' ili uweke hadharani bila kuombwa kufanya hivyo ni dalili ya kuwaingiza wananchi wengine kwenye box la fikra zako.
umeeleza vizuri sana...hongera
Ndugu, mimi kuwa mpuuzi hakuondoi ukweli kuwa CCM ina wabunge zaidi ya 250 wanaotambuliwa kisheria ambao kwa sasa wanatunga sheria ambazo ni lazima uzitii ukiwa nchini na kuendesha maisha yako ya kila siku ndani ya sheria hizo.Imeaminiwa na nani mpuuzi wewe? Yapo wapi mapendekezo ya tume ya Jaji Nyalali au Kisanga yaliyofanyiwa kazi ili kuweka mazingira sawa na ya haki kiushindani? Kama mnakubalika hivyo kwa nini miaka nenda rudi munaogopa kuwepo tume huru ya uchaguzi??? Kama huwa mnakubalika inakuwaje mwahadae wananchi hasa vijijini wasio na uelewa kwa wali,kanga,tshit,vilemba vya kijani na kununua shahada zao ili wasipige kura??? Mmezoea vya kunyonga vya kuchinja hamviwezi!
Hawa ukawa wanavuruga mipango ya maendeleo hivyo lazima wakemewe make kutwa wanaandamana na kuleta usumbufu kwa wafanyabiashara.Si mmesema anaenda kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM? Sasa ya UKAWA yanatoka wapi tena? Hivi na wewe, utaacha lini kutumia Mekako na Diprosoni na maji ya betri?
Kweli UKAWA ndiyo habari ya mjini.
Unataka ashike kama unavyoshika bakuri la gongo.Hivi huyu Mbunge wa Babati aliyeshika hicho kifaa eti anajenga ni kweli huwa kinashikwa hivyo? imefikia wakati sasa CCM muache usanii kwa kutumia picha
Kinana akiasaidiana na Mbunge wa Babati Mjini, Kisyeri Chambiri kujenga jengo la Zahanati ya Malangi, katika Kata ya Maisaka, Babati.
Mkuu salamu kwako.Asante
Mkuu salamu kwako.