Kinachovuruga Taifa ni Ubaguzi

Kinachovuruga Taifa ni Ubaguzi

Rlukaku

Senior Member
Joined
Dec 11, 2013
Posts
100
Reaction score
20
Pale inapotokea shughuli fulani ya kisiasa zinapigwa marufuku kwa vyama vyote halafu chama kimoja kinaendelea kufanya hilo lililokatazwa.

Yanazuiwa Mahafali ya wanafunzi wanaoshabikia chama kile lakini yanaruhusiwa ya wale wa chama hiki. Huu ubaguzi ndio unaolimaliza Taifa hili.

Inazuiwa Mikutano ya vyama vya siasa, inatumiwa nguvu kubwa kuwadhibiti wale wanaokiuka katazo kutoka upande ule, lakini wanaachwa wa upande huu wafanye wanavyotaka. Huu ubaguzi ndio unaotuingiza matatizoni, mambo haya yanaonekana na ni hatari jamani..

Mkutano Mkuu wa chama hiki unafanyika wakati kukiwa na katazo la kuzuia mikutano ya kisiasa kwa vyama vyote. Katazo hilo linakuwa ''suspended" siku moja kabla ya Mkutano. Halafu linarudishwa tena baada ya kukamilika Mkutano. Yawezekana litaondolewa tena kukiwa na haja ya kufanya mkutano. Haya mambo hayafai na ndio yatakayotuletea matatizo.

Kama tunataka kujenga Taifa moja hatupaswi kufanya ubaguzi wa aina yoyote kwa wananchi. Tusiweke matabaka miongoni mwetu. Kusiwe na watu wenye haki zaidi kuliko wengine. Tusione mtu ambaye hakubaliani na mawazo yetu kuwa ni mkosaji na hana haki ya kutenda mambo kadhaa.

Leo hii ni nadra sana kuona wale wa upande huu wakiburuzwa Mahakamani kwa makosa ambayo tunaona wale wa upande ule wakihenyeshwa Mahakamani kila kukicha. Haya mambo yanaonekana jamani watu wapo kimya tu lakini wanajua.

Mfano mdogo tu, jaribu kupita kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii, utakumbana na matusi wakitukanwa watu flani flani wa upande ule lakini hutasikia wakihojiwa popote.

Haya mambo jamii inayaona, na niwaambie tu, wengi hawayakubali lakini wanaamua kunyamaza kwa kuwa wameshajua upo ubaguzi na ukionekana hauko upande wao au ukiwapinga, uko matatani.

Nadhani kama Taifa tunahitaji kutafakari masuala haya. Nawahakikishia tunaweza tukawadhibiti sasa wasifanikiwe kufanya hicho wanachotaka kukifanya lakini kama na sisi tutaendelea kufanya haya tunayoyafanya, basi ni muda tu, tutarejea tena hapa hapa.

Mambo haya yakiendelea kufanyika kwa muda mrefu zaidi, basi tutakuwa tunaliingiza wenyewe Taifa letu matatizoni.

Niwambie tu, sababu za wazee wetu zamani kupigania uhuru hazitofautiani sana na haya tunayoyaona leo.

Wazee wetu walibaguliwa, walinyanyaswa, walionekana hawana hakli ya kufanya mambo flani flani ndani ya Taifa lao. Walivumilia hadi wakachoka. Wakatumia kila mbinu walizojaliwa na Mwenye ez Mungu kujikomboa.

Hakuna tofauti sana na sasa.

Swala hili si dogo kama wengi wanavyodhania, hapa ndio tunapohitajika kuonyesha busara zetu, tuumalize mgogoro huu tukiwa wamoja, tuachae kuligawa taifa kwa misingi ya vyama vyetu.

Ajenda yetu iwe moja, kujenga Taifa moja, tuwe wamoja katika kutekeleza hili. Tukubali kukosolewa pia tukubali mawazo ya wenzetu ili kufanikisha lengo letu moja.

Tusidhani kama sisi tuna haki miliki ya Taifa. Kiburi si maungwana, tutumie matukio yaliyotokea kwa wenzetu kama funzo. Tusirudie makosa.
 
Tatizo hatutengenezi sera/kanuni/sheria zinazoendana na haliyetu...huwezi tafuta eneo la duara kwa kanuni ya kutafutia eneo la pembetetu japo kanuni zote ni za kutafuta eneo
 
Si mnamini Mungu nyie? Amewasahau? Muhahaha... Kasikilizeni kibao cha Hard Blasters mburudike... Mwokozi nitoe roho niepuke hili balaa maisha yaliisha kwa kikwete... Sasa mtalia sana tu... Kila rangi hamtaacha kuiona... Upepo umebadilika... Msifikiri huyo kaja kwa bahati mbaya..
Mipango ilishapangwa kitambo... Lazima mnye kudadeki... Unyambilisi ni unyambilisi kwenu... Historian husema watu hawa huishi muda mrefu muumie sana hahahaha
 
Taifa limepasuka sana kwa sababu ya ubaguzi wa kisiasa.
 
Pale inapotokea shughuli fulani ya kisiasa zinapigwa marufuku kwa vyama vyote halafu chama kimoja kinaendelea kufanya hilo lililokatazwa.

Yanazuiwa Mahafali ya wanafunzi wanaoshabikia chama kile lakini yanaruhusiwa ya wale wa chama hiki. Huu ubaguzi ndio unaolimaliza Taifa hili.

Inazuiwa Mikutano ya vyama vya siasa, inatumiwa nguvu kubwa kuwadhibiti wale wanaokiuka katazo kutoka upande ule, lakini wanaachwa wa upande huu wafanye wanavyotaka. Huu ubaguzi ndio unaotuingiza matatizoni, mambo haya yanaonekana na ni hatari jamani..

Mkutano Mkuu wa chama hiki unafanyika wakati kukiwa na katazo la kuzuia mikutano ya kisiasa kwa vyama vyote. Katazo hilo linakuwa ''suspended" siku moja kabla ya Mkutano. Halafu linarudishwa tena baada ya kukamilika Mkutano. Yawezekana litaondolewa tena kukiwa na haja ya kufanya mkutano. Haya mambo hayafai na ndio yatakayotuletea matatizo.

Kama tunataka kujenga Taifa moja hatupaswi kufanya ubaguzi wa aina yoyote kwa wananchi. Tusiweke matabaka miongoni mwetu. Kusiwe na watu wenye haki zaidi kuliko wengine. Tusione mtu ambaye hakubaliani na mawazo yetu kuwa ni mkosaji na hana haki ya kutenda mambo kadhaa.

Leo hii ni nadra sana kuona wale wa upande huu wakiburuzwa Mahakamani kwa makosa ambayo tunaona wale wa upande ule wakihenyeshwa Mahakamani kila kukicha. Haya mambo yanaonekana jamani watu wapo kimya tu lakini wanajua.

Mfano mdogo tu, jaribu kupita kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii, utakumbana na matusi wakitukanwa watu flani flani wa upande ule lakini hutasikia wakihojiwa popote.

Haya mambo jamii inayaona, na niwaambie tu, wengi hawayakubali lakini wanaamua kunyamaza kwa kuwa wameshajua upo ubaguzi na ukionekana hauko upande wao au ukiwapinga, uko matatani.

Nadhani kama Taifa tunahitaji kutafakari masuala haya. Nawahakikishia tunaweza tukawadhibiti sasa wasifanikiwe kufanya hicho wanachotaka kukifanya lakini kama na sisi tutaendelea kufanya haya tunayoyafanya, basi ni muda tu, tutarejea tena hapa hapa.

Mambo haya yakiendelea kufanyika kwa muda mrefu zaidi, basi tutakuwa tunaliingiza wenyewe Taifa letu matatizoni.

Niwambie tu, sababu za wazee wetu zamani kupigania uhuru hazitofautiani sana na haya tunayoyaona leo.

Wazee wetu walibaguliwa, walinyanyaswa, walionekana hawana hakli ya kufanya mambo flani flani ndani ya Taifa lao. Walivumilia hadi wakachoka. Wakatumia kila mbinu walizojaliwa na Mwenye ez Mungu kujikomboa.

Hakuna tofauti sana na sasa.

Swala hili si dogo kama wengi wanavyodhania, hapa ndio tunapohitajika kuonyesha busara zetu, tuumalize mgogoro huu tukiwa wamoja, tuachae kuligawa taifa kwa misingi ya vyama vyetu.

Ajenda yetu iwe moja, kujenga Taifa moja, tuwe wamoja katika kutekeleza hili. Tukubali kukosolewa pia tukubali mawazo ya wenzetu ili kufanikisha lengo letu moja.

Tusidhani kama sisi tuna haki miliki ya Taifa. Kiburi si maungwana, tutumie matukio yaliyotokea kwa wenzetu kama funzo. Tusirudie makosa.
Taifa limepasuka sana kwa sababu ya ubaguzi wa kisiasa.


Vigezo mnavyotumia kusema kuna ubaguzi au mmeonewa vinautata. Mkishinda kesi mnasema mahakama inatenda haki, mkishindwa mnasema mahakama haitendi haki. Msigwa akifanya mikutano yake Iringa ikiisha salama bila kusumbuliwa na polisi hamsemi kuna ubaguzi. Lowassa akifanya mikutano yake Mtwara ikiisha salama bila kusumbuliwa hamsemi kuna ubaguzi. Lakini Lissu akifanya mikutano yake singida na kukamatwa unasema kuna ubaguzi. Nasubiri siku CCM watakaposhindwa kesi ya uchaguzi alafu walalamike kuna ubaguzi. Hivyi CCM wameshawahi kushindwa kesi ya uchaguzi?
 
Nilikuwa najiuliza hivi ingetokea Ndugu Edward Lowasa akatangaza kurejea CCM mwezi mmoja kabla ya uchaguzi mkuu wa kumchagua mwenyekiti na kuonyesha nia ya kuanzisha movements za kugombea uenyekiti ili kuondoa dhana ya uenyiki na uraisi na kuwagawa wanachama kifikra. Kisha unexpectedly akatinga kwenye mkutano mkuu akiwa na wapambe huku akiwa si miongoni mwa wajumbe,Je walinzi kwa maana ya polisi wangemruhusu kuingia ukumbini kama ilivyotokea kwa CUF?.
 
Vigezo mnavyotumia kusema kuna ubaguzi au mmeonewa vinautata. Mkishinda kesi mnasema mahakama inatenda haki, mkishindwa mnasema mahakama haitendi haki. Msigwa akifanya mikutano yake Iringa ikiisha salama bila kusumbuliwa na polisi hamsemi kuna ubaguzi. Lowassa akifanya mikutano yake Mtwara ikiisha salama bila kusumbuliwa hamsemi kuna ubaguzi. Lakini Lissu akifanya mikutano yake singida na kukamatwa unasema kuna ubaguzi. Nasubiri siku CCM watakaposhindwa kesi ya uchaguzi alafu walalamike kuna ubaguzi. Hivyi CCM wameshawahi kushindwa kesi ya uchaguzi?
Usiseme maneno mengi.Ingia mtaani ujionee mpasuko wa wananchi.
 
Wajameni mnatuchosha na makelele yenu. Ngojeni hiyo tarehe mosi septemba muingie mitaani kuandamana. Kelele zenu hazisaidii kwa sasa na hazitabadilisha lolote.
 
Yaani unavyoshabikia kama toto la kindergarten hivi,yaani hujifikirishi kabisa...

Kwahiyo kwa akili yako fupi kama midget unaona ni sahihi wanadamu kama wewe,wenye uhitaji wa maisha kama wewe,wenye mawazo tu tofauti na wewe wafanyiwe "unyambilisi" mpaka "wanye",yaani wewe akili yako ipo m.a.ta.ko.ni...

Mtu kutofautiana na wewe kifikra sio tiketi ya kuwageuza ng'ombe,kajifunze ustaarabu
We tukana lakini ndio hali ya sasa ilivyo yaani Bado miaka Tisa na mkitaka katiba sharti kifungu cha uraisi kiongezwe muhahaha... Afu sikia neno Ustaarabu linapatikana Arabuni na lina maana yake hivyo haliwezi practice utawala huu...
 
Vigezo mnavyotumia kusema kuna ubaguzi au mmeonewa vinautata. Mkishinda kesi mnasema mahakama inatenda haki, mkishindwa mnasema mahakama haitendi haki. Msigwa akifanya mikutano yake Iringa ikiisha salama bila kusumbuliwa na polisi hamsemi kuna ubaguzi. Lowassa akifanya mikutano yake Mtwara ikiisha salama bila kusumbuliwa hamsemi kuna ubaguzi. Lakini Lissu akifanya mikutano yake singida na kukamatwa unasema kuna ubaguzi. Nasubiri siku CCM watakaposhindwa kesi ya uchaguzi alafu walalamike kuna ubaguzi. Hivyi CCM wameshawahi kushindwa kesi ya uchaguzi?
Kwenye kesi za uchaguz kila mtu anapewa jimbo lake hakuna kutengua kama lipo hiyo ni zuga tu.
 
Na wenyewe wanajipa moyo kuwa kila utawala haukosi lawama... Hata waisrael walishushuwa chakula kutoka mbinguni wakakilalamikia pia..

Ila magufuli akiamua tutaelewana na asipotaka tutaendelea na hali hii hadi tusaidiwe na Marekani
 
ubaguzi wa kisiasa ni mbaya sana hata nchi haiwezi kwenda.
kwa nchi maskini kama tanzania. ambayo saizi ndio ipo kuhangaika kuchonga madawati ilikuwa haina sababu ya kubaguana. ilitakiwa kuwe na ushrikiano wa hali juu sana kama inawezekana siku moja rais anawaita viongo wa upinzani ikulu na wanakula chakula pamoja na wanazungumza mambo mawili matatu ambayo yanafaida kwenye nchi yetu.

lakini sio unasikia mara leo viongozi waupinzani wamevamiwa na polisi
mara sijui nani anatafutwa na polisi.
inakuwa haipendezi na tunakuwa tunjijengea picha mbaya kimataifa na inaondoa sifa ya tanzania kuitwa nchi ya amani.
 
Back
Top Bottom