Kinachotumwa NEC sio kura zilizohesabiwa vituoni, ni zilizohesabiwa na wasimamizi wa uchaguzi

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,320
Hili jambo kuwa kura za ubunge na uraisi zitahesabiwa na kubandikwa vituoni lisitupumbaze tukaachia goli la mkono kirahisi

Hali huwa hivi

1. Kura zikishahesabiwa vituoni, masanduku hufungwa kwa kufuli mawakala wote wakiona.

2. Masanduku husafirishwa na magari ya halmashauri kupelekwa point moja ya kuhesabia tena pale halmashauri.

3. Ikumbukwe kuwa magari yanayosafirisha kura mara nyingi hayabebi mawakala, Huwa ni gari moja linazunguka kwa vituo kadhaa likikusanya masanduku

4. Masanduku yakishafika kwenye ukumbi wa kuhesabia huko halmashauri, hupokelewa na mkurugenzi wa halmashauri

5. kazi ya kuhesabu UPYA kura za ubunge na uraisi hufanywa tena pale halmashauri. Hapa wanakuwepo wakala mmoja mmoja kwa kila chama chenye mgombea wa uraisi, na wagombea ubunge peke yao.

6. Mbunge hutangazwa kutokana na idadi ya kura zilizohesabiwa PALE HALMASHAURI, sio za vituoni

7. Matokeo ya kura za uraisi hutumwa na mkurugenzi wa wilaya, ambapo ni yale yaliyohesabiwa pale halmashauri, sio ya vituoni

8. Ujumlishwaji wa kura zilivyohesabiwa vituoni unaweza kufanywa, lakini final say ni kura zilizohesabiwa halmashauri.

Kama kuna mtu anaplan kuzuia goli la mkono atafakari yafutayo;
1. Namna ya kuhakikisha masanduku yaliyotoka vituoni, ndiyo yaliyofika halmashauri

2. Namna ya kuhakikisha masanduku yaliyotoka vituoni hayakufunguliwa njiani

3. Namna ya kuhakikisha hakuna masanduku za ziada yataingia kwenye ukumbi wa kuhesabia pale halmashauri

Tahadhari; Mara nyingi umeme huwa unakatika au unazima kwenye ukumbi wa kuhesabia kura pale halmashauri na kutoa mwanya wa GIZA (bebeni tochi). Kukiwa na sintofahamu yeyote pale halmashauri na mawakala/wajumbe wakahoji, huambiwa wanaleta vurugu, hukamatwa na askari wanaokuwa wamemwagwa pale, na hivyo ukumbi huwa "free" baada ya hao kukamatwa.

Tutaendelea kutafakari...
 
Lazima tujue kama ni almashauri au manespaa au kata kwa kata. Hakuna bao ka mkono.


swissme
 
Mwaka huu hawataribu,make sambamba na masanduku hayo lazma iwepo nakala ya matokeo toka kituo husika iliyosainiwa na mawakala wa vyama,pia wakala anabaki na copy kwa ajiri ya rejea ya chama husika,ukawa wamejipanga kila kituo mawakala 3 ila lazma kura zilindwe vituoni na wapiga kura coz kule ndiko wizi unakofanyika sana pamoja na vituo bubu
 
Mwaka huu hawataribu,make sambamba na masanduku hayo lazma iwepo nakala ya matokeo toka kituo husika iliyosainiwa na mawakala wa vyama,pia wakala anabaki na copy kwa ajiri ya rejea ya chama husika,ukawa wamejipanga kila kituo mawakala 3 ila lazma kura zilindwe vituoni na wapiga kura coz kule ndiko wizi unakofanyika sana pamoja na vituo bubu

Hili ndio linatakiwa kutiliwa msisitizo. Kusema na kutenda ni vitu viwili tofauti. Mara nyingi mawakala na wagombea "hupoteana" kuanzia tu ngazi ya kata.

Katika uchaguzi uliopita kwenye jimbo letu, mawakala wengi vituoni waliwekwa na walikuwa wanaripoti kwa wagombea udiwani kwa maana ndiko vituo vilipo. Baada ya wagombea udiwani wengi kushindwa, ama kwa hasira za kushindwa au kwa kuona so, waliachana na kusimamia usahihi wa kura za uraisi na ubunge zilizowasilishwa level ya jimbo. Mgombea ubunge pia baada ya kushindwa alikuwa puzzled, na hakuwa tena makini kwenye kuhakiki kura za uraisi zikihesabiwa, kujumlishwa, na kutumwa NEC,

Tuendelee kujipanga...
 
asante Tuko kwa taarifa lakini nimesikia kuwa kwa sababu wanajua kwamba ukawa umejipanga kuyapata matokeo mapema kabla ya tume ya uchaguzi makamba na timu yake wanajaribu kusuka na makampuni ya simu na umeme ili kukata mawasiliano yote nchi nzima ili kuzuia mawasiliano yote ya simu na umeme ili kushindwa kukusanya matokeo na hivyo kuwapa nafasi wao kutengeneza matokeo kwani makao makuu mikoani watakuwa hawana uwezo wa kuwasiliana na askari wao wa miavuli yaani mawakala wao waliotapakaa nchi nzima kwahiyo lengo ni kukata mawasiliano kati ya wakala na mkoa na pia mkoa na Taifa.
 
Tuko

Hapo no 1 ndiyo ccm huiba kura,nilikua na afisa ugavi halmashauri songea anasema huwa na duplication ya masanduku ya kura,na kura zenyewe zikiwa tayari na idadi sawa na ile ya kituoni,gari lañdcruizer yenye plate namba zinazofanana kabisa na ile halisia,sasa gari hizi hubadilika linapoingia halmashauri lile la wizi ndiyo hushusha masanduku kuhesabiwa
 
Last edited by a moderator:
Hapo no 1 ndiyo ccm huiba kura,nilikua na afisa ugavi halmashauri songea anasema huwa na duplication ya masanduku ya kura,na kura zenyewe zikiwa tayari na idadi sawa na ile ya kituoni,gari lañdcruizer yenye plate namba zinazofanana kabisa na ile halisia,sasa gari hizi hubadilika linapoingia halmashauri lile la wizi ndiyo hushusha masanduku kuhesabiwa

Mkuu hapa ndio inabidi watu wajipange. Ni rahisi sana kuzibiti hali hii...
 
Mkuu Tuko uko sawa kamanda. Mwaka huu watachafua nchi na hawatotoka salama.
 
Last edited by a moderator:
Tuko

Matokeo yanayo tolewa hapo halmashauri ni yale yaliyo toka kutoka kila kituo.....sijui una mdanganya nani wewe Bavicha? Haya twambie hayo matokeo halmashauri wana yapata wapi kama sio kwenye vituo tofauti?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Tuko uko sawa kamanda. Mwaka huu watachafua nchi na hawatotoka salama.

Naomba tuchukulie kwa uzito observation ya mkuu BONGOLALA hapo juu. Kuwa gari baadhi ya gari zinazobeba masanduku vituoni zinakuwa na duplicate zake zenye namba sawa lakini masanduku feki.

Escorts zifanywe hatua kwa hatua kwa gari zinazokusanya masanduku...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom