Mwaka jana Tume ya Warioba ilitikisa sana nchi hii kuhusiana na kukusanya maoni ya wananchi na hatimaye kuja na Rasimu ya Katiba Mpya; wote tunaelewa kilichotokea rasimu ya Jaji Warioba ikatupiliwa mbali na CCM wakiongozwa na mwenyekiti wao. Utupiliaji mbali wa rasimu hiyo uliambatana na kashifa na kejeli kwa iliyokuwa tume ya Warioba.
Kwa uadilifu kabisa, wajumbe wa iliyokuwa tume ya katiba wakajikusanya kwa umoja wao chini ya Nyerere Foundation kutetea rasimu yao ya katiba wakisema yaliyokuwemo ndani ya rasimu hiyo ya katiba yalikuwa maoni ya watanzania. Jaji Warioba, H. Polepole, Butiku, Prof. Kabudi na wengineo walizunguka nchini wakieleza bayana kwamba serikali ya CCM imetupilia mbali maoni ya wananchi. Wananchi walitaka wawe na uwezo wa kuwawajibishia viongozi wao wa kisiasa, kupunguza madalaka ya ya rais, kutoruhusu viongozi kuwa na akaunti nje ya nchi, uadilifu na uwajibikaji.
Kinachonishangaza ni pale ninapoona watu wale wale waliozunguka kote nchini wakiendesha midahalo kuwaelimisha wananchi namna ambavyo serikali ya CCM ilivyodharau maoni ya wananchi. Wananchi wakafika mahala wakawaelewa waliokuwa wajumbe wa tume ya Jaji Warioba; lakini leo hii, wajumbe wale wale wanajitokeza hadharani na kusema hakuna waliobora miongoni mwa viongozi zaidi ya watu hao hao waliokataa katakata kuwajibishwa na wananchi; watu hao hao waliokataa kwa nguvu zao zote kuingiiza vipengele vya uadilifu na uwajibikaji katika katiba mpya.
Mwenzenu, hakika nawashangaa kina Jaji Warioba na wenziye.
Kwa uadilifu kabisa, wajumbe wa iliyokuwa tume ya katiba wakajikusanya kwa umoja wao chini ya Nyerere Foundation kutetea rasimu yao ya katiba wakisema yaliyokuwemo ndani ya rasimu hiyo ya katiba yalikuwa maoni ya watanzania. Jaji Warioba, H. Polepole, Butiku, Prof. Kabudi na wengineo walizunguka nchini wakieleza bayana kwamba serikali ya CCM imetupilia mbali maoni ya wananchi. Wananchi walitaka wawe na uwezo wa kuwawajibishia viongozi wao wa kisiasa, kupunguza madalaka ya ya rais, kutoruhusu viongozi kuwa na akaunti nje ya nchi, uadilifu na uwajibikaji.
Kinachonishangaza ni pale ninapoona watu wale wale waliozunguka kote nchini wakiendesha midahalo kuwaelimisha wananchi namna ambavyo serikali ya CCM ilivyodharau maoni ya wananchi. Wananchi wakafika mahala wakawaelewa waliokuwa wajumbe wa tume ya Jaji Warioba; lakini leo hii, wajumbe wale wale wanajitokeza hadharani na kusema hakuna waliobora miongoni mwa viongozi zaidi ya watu hao hao waliokataa katakata kuwajibishwa na wananchi; watu hao hao waliokataa kwa nguvu zao zote kuingiiza vipengele vya uadilifu na uwajibikaji katika katiba mpya.
Mwenzenu, hakika nawashangaa kina Jaji Warioba na wenziye.