Yaliyojiri Ikulu: Mazungumzo kati ya Viongozi wa dini nchini na Rais Magufuli

Hahahaha kuna mtu anataka "kutembelea Nyota" ya viongozi wa dini! Maana siku hizi kila shughuli yupo nao kama vile Gwajima, Kakobe, mara wapo Maaskofu etc

Anajua viongozi wa dini wakiwa upande wake , wakimzungumzia kwa uzuri basi na kondoo wao watakuwa sympathetic naye!

Kule kwa ndugu zetu Waislamu yeye ameridhika kujumuika na Sheikh Alhadi, lakini kwa Jinsi yule dada wa Marekani alivyokwishatoa tuhuma kali kwa huyo Sheikh keshachafuka sana, hakuna Muislamu anayemchukulia serious!!

Ngoja nimshauri njia nzuri ya kuleta umoja na mshikamano wa Kitaifa!

1. Mzee angalia TEUZI zako zimeegemea upande mmoja zaidi, watu wanalisema hili mtaani

2. Heshimu katiba ya nchi, hakuna haja ya kuminya haki ambayo makundi mengine yamepewa na katiba, haikufanyi kuonekana strong kwa kujaribu kuimply kwamba uko sahihi kuliko katiba

3. Kazi zako zilenge kupanua uhuru wa watu zaidi kuliko kuuminya. Hii miswada ya vyama vya siasa ambayo inakwenda kuminya vyama na kuvifanya viwe vyama visivyong'ata hailisaidii Taifa. Nyerere alidhani mwaka 1965 kuwa vyama vingi vinamchelewesha kuleta maendeleo lakini Nyerere huyohuyo miaka 25 baadae akagundua kuwa alifanya mistake kubwa, please usichukue njia hiyo ya kale kwa sababu kwanza Kizazi kijacho kitaifuta hiyo sheria unayotaka kuifunga, lakini utakuwa umeshawachelewesha kwenye kujenga Taifa lililokomaa kidemokrasia

4. Mzee, Mshikamano bila uchumi ni sawa na kiwiliwili bila mikono na miguu, hapawezi kuwepo na mshikamano wakati vyuma vimekaza, bila uchumi ndoa zitakufa, watu watashikana uchawi, vibaka wataongezeka, misongo ya mawazo itaongezeka na hatimaye kuzaa chuki baina ya wenye nacho na wasionacho, Mshikamano hautakuwepo!. Badili sera zako za uchumi sasa ili kustimulate biashara, Ikibidi kupunguza kodi punguza, nimeona leo kwenye taarifa ya habari kuwa uchumi wa china umeshuka na njia moja wanayoifanya sasa ni kupunguza kodi na kuinject mabilioni ya dola kwenye miradi inayogusa wananchi moja kwa moja ili kupunguza makali!. Ongea vizuri na wafanyabiashara wakubwa nchini, wafanyie wepesi kwenye mambo yao usiwakwaze, Matajiri ni mawakala wa Mungu kwenye kusambaza Rizki kwa waja wake duniani!, Wana upako wa hela hao, ukiwajaribu kuwashusha utashuka mwenyewe!, Ukijaribu kuwakwaza utajikwaza Mwenyewe, maana maandiko yanasema yule aliyepewa na Mungu hakuna mwanadamu anayeweza kumnyang'anya labda Mungu mwenyewe awe ameamua hivyo!!.

5. Mzee inabidi sasa uanze kuwa Stateman, Unahitajika sasa Kupandisha "Game" yako iwe international zaidi. Uwanja wa hapa nyumbani muachie Kassimu, sina shaka naye, ni kiungo mchezeshaji mzuri sana, nazikubali kazi zake. Sasa inabidi uende Ulaya uongee na akina Angela Merkel, akina Theresa May, Nenda Canada, Nenda hata hapo Australia kaongee na Investors waje, Shuka hata South hapo bondeni uangalie nini wataalamu wa madini hapo wanaweza kushare nasi katika hii sekta

6. Mzee, Maendeleo ya vitu bila Uhuru ni kazi bure!. Leo hii tunamkumbuka Nyerere siyo kwa sababu alijenga reli ya Tazara, na bomba la TAZAMA au Viwanda kedekede tunamkumbuka zaidi kwa sababu alitupa Uhuru kutoka kwa mkoloni!. Na wewe unayonafasi ya kutupa Uhuru mpana zaidi, hizi sheria za Habari na Takwimu hazitusaidii katika azma ya kuwa na watu wenye FIKRA HURU, Zinaweza kukusaidia kisiasa katika mwaka wako mmoja uliobaki au ukibahatika Sita iliyobaki lakini zina athari isiyomithilika kwa Usitawi wa Taifa. Zitakwenda kujenga Taifa la Watu Vipofu, Wasiohoji, Wenye kuamini Propaganda za Serikali inayotawala, Kiufupi zinakwenda kujenga Taifa la watu walio usingizini!. Je ungependa miaka 30 ijayo kuwa na TAIFA la watu bongolala?. Angalia miaka 50 ijayo mzee, usiangalie uchaguzi ujao

7. Mzee Korosho, Korosho, Korosho Mzee, Kangomba na Mkulima wa Korosho ni sawasawa na chungu na Kata, Mkulima anayetafuta hela ili amcheze mwanae Ngoma, Kangomba ndiye Mkombozi wake!. Huwezi kudhani Kangomba anamdhulumu mkulima, wakati Mahitaji ya Mkulima yanatimizwa na Kangomba!. Nyinyi watu wa Mjini mnadhani mahitaji yenu ya mjini ndo yaleyale ya mkulima!. Ni sawasawa na Mzungu atoke huko Ulaya akute mwalimu wa Msingi analipwa dola 300 ( shilingi laki sita) halafu aanze kudai eti Mwajiri anamdhulumu mwalimu!. WE NEED TO KNOW basic economics pribciples za NEEDS za watu na WANTS za watu!
We bwege nimekuelewa mpaka nimekuelewa tena.
ILA mkumbushe pia kupunguza kibuli kwa kufanya hivyo kutamrejeshea mahusiano na nchi wahisani ambao kila siku wana withdraw mikono yao kwenye hii nchi.MZUNGU NDIYE MSHIKA REMOTE YA MAENDELEO KWENYE NCHI ZA KIAFRIKA SO A PLAY NAO SMART AACHE MTINDO WA KUWATUNISHIA MISULI.
Kwa kurejesha maelewano na nchi hisani wa Tz kutamfanya asitegemee chanzo kimoja(kodi) cha fedha za kuendeshea serikali yake.
LA SIVYO ATAZIDI KUTUBANA NASI KAMA WANANCHI TUTAMCHUKIA RAISI WETU KWA KUTUPA MAISHA MAGUMU TOFAUTI NA YALE YA ENZI ZA UFISADI(JK).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimetumiwa sasa hvi na kila siku lazima nitumiwe, naamini maamuzi yatachukuliwa.
Screenshot_20190123-135405.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mama Riona Kimario nakupongeza sana kwa mchango wako hili mimi nililiwazaga siku nyingi sana. Ukipita njiaani hasa barabara za mikoani utaona vibwawa vidogovidogo vilivyiochimbwa na wachina wakati wakijenga barabara. Utashuhudia watu wakichota maji na wengine wakilima kandokando ya bwawa, lakini ni vidogo na havitoshelezi mahitaji.

Sasa huwa najiuliza serikali haiwezi weka sera ili hawa wajenzi wa barabara angalau wawe wanachimba square metre kadhaa ambazo zitatoa bwawa kubwa ambalo litahifadhi maji ya kutosha kufanyia kilimo kulisha mifugo na kufuga samaki ili kurahisisha mapinduzi ya kilimo, kuliko kuwaacha wachimbe vibwawa vidogo vidogo tena vipo karibu karibu ambovyo huchangia kuchafua mazingira. Haya mabwa yakitumiwa vizuri yanaweza kuwa chanzo kizuri cha mapato cha halmashauri hata taifa sababu wenye mifugo watalipia ushuru na wenye kilimo watalipia ushuru wafuga samaki ambso wanaweza kuwa kwenye vikundi na watalipia ushuru.

Imani yangu ni kuwa tuma Raisi msikivu mno na amini atalifanyia kazi wazo lako.
 
naunga mkono kupigwa marufuku biashara zote za bahati nasibu, betting na kamari.
Na ile gaming board ifutiliwe mbali kabisa.
Ushoga ndio kabisa Mungu atuepushie mbali usitokee kabisa


Hii sio nchi ya kidini. Vitu vibaya sio kamali tu, hata Pombe na music. Mbona hivyo hamsemi vizuiwe?.

Kikubwa ni taratibu na shria za michezo kuzingatiwa. Tusifuate mkumbo.

Betting ni kama games nyingine.Kodi wanalipa n.k.
 
Huyo Mchungaji kijana mchumi anaitwa KIMARO amemwaga fact sana sana, HIVI WACHUMI MNASHINDWA KUWAZA KAMA ANAVYOWAZA HUYO MCHUNGAJI, AU MUENDE MKASWALI KANISANI KWAKE MUOMBE KIPINDI MAALUMU CHA UCHUMI.

HUYU MCHUNGAJI ANAONYESHA MADHARA KABISA YA WASOMI WETU KUKOSA EXPOSURE MAANA ANAJUA VITU VINGI AMBAVYO WATU KAMA WANGEKUWA WANAVIJUA NA KUVIAPPLY TUNGEKUWA MBALI SANA..
Tatizo mifumo yetu ya utawala haitaki watu waerevu ndyo maana wakina bashite wanatamba na matamko ya hovyo

Yaani mfumo unachohitaji ni uwe kada mtiifu tu basi unapewa shavu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ukiwa Rais lazima uwe na strategies nyingi sana za kufanya kazi yako iwe bora, vinginevyo utakwama na wananchi watakuchukia.
 
Back
Top Bottom