Kinachofanywa Kimara ni Kinyume na UTU Kabisa

Kinachofanywa Kimara ni Kinyume na UTU Kabisa

Tony antony

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2013
Posts
4,988
Reaction score
3,270
Habari wanajukwaa....
Mimi kama kada wa CCM mwenye Mawazo Huru,ninayekubali kukosolewa na kukusoa panapobidi hata iwe ndani ya Chama Changu,naomba nipingane vikali na Serikali juu ya kinachofanywa eneo la Kimara.

Haiwezekani Kesi ipo Mahakamani lakini nyie mnafanya maamuzi ya kuwabomolea wananchi Nyumba zao,ni kinyume na sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,hatuwezi kwenda kwa style hii ya kuignore Mhimili huu wa Mahakama,hapana.

Zaidi ya hapo msivokua na UTU mnawabomolea wananchi nyumba zao bila taarifa bila utaratibu maalumu,hawa watu wanaenda kuishi wapi,hawa watu muda huu wanaenda kujihifadhi wapi? Kwanini msingetenga eneo maalumu kuwahifadhi hawa raia,mnawafanya wakimbizi ndani ya nchi yao,sio haki,sio UTU.

Kama kuna mwanaCCM anayefurahi na kufurahia hili jambo Serikali ya Chama Chetu inafanya Ajitafakari mara mbili,la sivyo hata yeye amekosa UTU.
 
Tatizo ni kisasi cha wana kimara kuinyima kura ccm na ukichangia wakazi wa eneo Hilo Raisi anavyowachukia sasa hyo ndo anafikiri kuwabomolea kutampa amani nafsini mwake. Binadamu bila kujali Chama lazima kuwe na utu
 
Duuuuh 😵🙁🙁😡 hakuna namna tena, amri ikishatolewa na wenye mamlaka hakuna wa kupinga. Na kuhusu fidia kwa wahanga duuuh sidhani!
 
PALE MBEZI MWISHO STENDI MPYA ULE UPANDE WA KITUO CHA KWENDA SEGEREA, KULIKUWA NA GHOROFA LILIVUNJWA NA SASA LINAJENGWA NYUMA YAKE KAMA LILE LA KWANZA.

HIVI HIZI MITA 121.5 ZILIZOANZA KUTUMIKA HAZIMGUSI HUYU MDAU KWELI? MAANA, SIJUI, MUNGU AEPUSHIE MBALI.
 
Kesi IPO mahakamani na ieleweke wananchi wakishinda basi serikali itabidi iwalipe wananchi fidia


Hapo ndo tutazidi kuingia hasara

Mpaka 2020 ndo mtaamini pombe si chai

love without limits
 
Habari wanajukwaa....
Mimi kama kada wa CCM mwenye Mawazo Huru,ninayekubali kukosolewa na kukusoa panapobidi hata iwe ndani ya Chama Changu,naomba nipingane vikali na Serikali juu ya kinachofanywa eneo la Kimara.

Haiwezekani Kesi ipo Mahakamani lakini nyie mnafanya maamuzi ya kuwabomolea wananchi Nyumba zao,ni kinyume na sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,hatuwezi kwenda kwa style hii ya kuignore Mhimili huu wa Mahakama,hapana.

Zaidi ya hapo msivokua na UTU mnawabomolea wananchi nyumba zao bila taarifa bila utaratibu maalumu,hawa watu wanaenda kuishi wapi,hawa watu muda huu wanaenda kujihifadhi wapi? Kwanini msingetenga eneo maalumu kuwahifadhi hawa raia,mnawafanya wakimbizi ndani ya nchi yao,sio haki,sio UTU.

Kama kuna mwanaCCM anayefurahi na kufurahia hili jambo Serikali ya Chama Chetu inafanya Ajitafakari mara mbili,la sivyo hata yeye amekosa UTU.
Adui mkubwa wa mtanzania ni mtanzania mwenyewe wala siyo mzungu
 
Si yeye mwenyewe alisema Urais ameubeep tu, na alishasema mkimchagua kuwa Rais lazima mlimie meno sasa unashangaa na kulalamika nini, si mlidhani Edo fisadi mkampa yeye! huyu anafanya hivi ili msimpe tena uraisi 2020, sasa kwa ujinga wako mtampa tena, kama wewe umevunjiwa ukomeshwe kabisa hadi utembelee ndala, na wale wenzangu na mie poleni sana, tuliyajua haya.
 
Back
Top Bottom