getrusa
JF-Expert Member
- Aug 16, 2013
- 2,150
- 1,824
Wakuu, kumekuwa na taarifa za mauaji na vifo vya watu wanaokadiriwa kufikia 30 mpaka sasa kati ya makundi kadhaa yanayohasimiana huko Sudani baada ya kufanyika maandamano ya kumuondoa Omar Bashir, sio hivyo tu ila pia kuna tetesi ya hali kutokuwa tengefu kwa serikali iliyojiita ya Mpito.
Kwa mtazamo wangu kinachotokea Sudani ni sawa na kile kilichotokea Libya miaka kadhaa iliyopita, swali la kujiuliza je ni ipi faida wanayopata hawa wanaojiita wanaharakati baada ya uharibifu huu?
Baada ya machafuko haya kuanza wao huwa wanafaidi nini?
Je, wale wanaharakati wa Demokrasia kule sudan wanafirahia matunda ya jitihada zao?
Kama haitoshi kesi anayohukumiwa kwayo Rais omar Bashir ni ya miongo kadhaa iliyopita je hiki ndicho kinachotafutwa na wanaharakati wetu hapa Tanzania kwa mgongo wa Demokrasia.?
Nawasilisha..
Kwa mtazamo wangu kinachotokea Sudani ni sawa na kile kilichotokea Libya miaka kadhaa iliyopita, swali la kujiuliza je ni ipi faida wanayopata hawa wanaojiita wanaharakati baada ya uharibifu huu?
Baada ya machafuko haya kuanza wao huwa wanafaidi nini?
Je, wale wanaharakati wa Demokrasia kule sudan wanafirahia matunda ya jitihada zao?
Kama haitoshi kesi anayohukumiwa kwayo Rais omar Bashir ni ya miongo kadhaa iliyopita je hiki ndicho kinachotafutwa na wanaharakati wetu hapa Tanzania kwa mgongo wa Demokrasia.?
Nawasilisha..