Raimundo
JF-Expert Member
- May 23, 2009
- 13,415
- 12,622
Kuna dada tuko naye ofisini, sasa huku na huku akapata mchumba kutoka West Africa, huyu mchumba anadai amesoma Russia na sijui alikuwa anafanya kazi gani hapa Bongo, maana hata dada mwenyewe ukimuuliza haelewi elewi. Harafu jamaa alikuwa fasta kujitambulisha mpaka kwa bi mkubwa, akaonyesha ana nia ya kweli kabisa ya kuoa, akawa anaenda naye kwenye harusi za hapa ofisini na za kwa marafiki zao wengine.
Basi mapenzi yameendelea, jamaa akawa ndo anaendesha gari la yule dada, anampeleka ofisini na kumfata jioni. Jamaa taratibu akaanza kutumia hela ya yule dada huku akidai kuna mafao yake atalipwa soon so watakuwa poa kifedha.
Dada wa watu akachukua mkopo kama Mil 9 kwa ajili ya kuanza ujenzi lakini kumbe zikaingia kwenye mkumbo wa kuliwa. Ikafikia wakakubaliana eti jamaa aende Marekani, akifika kule akishaandaa mazingira atamchukua dada yetu wa kazini akaishi naye huko mambelez. Hela ya mkopo ikaisha, akakopa kwa washkaji hapa hela nyingine kama Mil 2 ya kuongezea ili kufanikisha safari.
Jamaa sasa ni muda kama wa miezi miwili toka aende USA na hajawahi hata kutoa contacts zake kwa dada yetu, huku jamaa wanamsakama kwa madeni yao (hasa hasa ile mil 2 ya nyongeza). Facebook jamaa hayuko active tena, inshort kapotea mazima. Dada wa watu saa hizi ni full stress, mshahara unakatwa hela ambayo hakuitumia, madeni yanamwandama, mpenzi kamkatia mawasiliano.
Kwa hiyo dada zetu mfanye uchunguzi wa kina kabla ya kugawa mioyo na mali wa wageni, wengine wamekuja kuchuma vilivyo vyetu kwa njia yoyote ile.
Basi mapenzi yameendelea, jamaa akawa ndo anaendesha gari la yule dada, anampeleka ofisini na kumfata jioni. Jamaa taratibu akaanza kutumia hela ya yule dada huku akidai kuna mafao yake atalipwa soon so watakuwa poa kifedha.
Dada wa watu akachukua mkopo kama Mil 9 kwa ajili ya kuanza ujenzi lakini kumbe zikaingia kwenye mkumbo wa kuliwa. Ikafikia wakakubaliana eti jamaa aende Marekani, akifika kule akishaandaa mazingira atamchukua dada yetu wa kazini akaishi naye huko mambelez. Hela ya mkopo ikaisha, akakopa kwa washkaji hapa hela nyingine kama Mil 2 ya kuongezea ili kufanikisha safari.
Jamaa sasa ni muda kama wa miezi miwili toka aende USA na hajawahi hata kutoa contacts zake kwa dada yetu, huku jamaa wanamsakama kwa madeni yao (hasa hasa ile mil 2 ya nyongeza). Facebook jamaa hayuko active tena, inshort kapotea mazima. Dada wa watu saa hizi ni full stress, mshahara unakatwa hela ambayo hakuitumia, madeni yanamwandama, mpenzi kamkatia mawasiliano.
Kwa hiyo dada zetu mfanye uchunguzi wa kina kabla ya kugawa mioyo na mali wa wageni, wengine wamekuja kuchuma vilivyo vyetu kwa njia yoyote ile.