Kina dada muwe makini na Foreigners

Kina dada muwe makini na Foreigners

Raimundo

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2009
Posts
13,415
Reaction score
12,622
Kuna dada tuko naye ofisini, sasa huku na huku akapata mchumba kutoka West Africa, huyu mchumba anadai amesoma Russia na sijui alikuwa anafanya kazi gani hapa Bongo, maana hata dada mwenyewe ukimuuliza haelewi elewi. Harafu jamaa alikuwa fasta kujitambulisha mpaka kwa bi mkubwa, akaonyesha ana nia ya kweli kabisa ya kuoa, akawa anaenda naye kwenye harusi za hapa ofisini na za kwa marafiki zao wengine.


Basi mapenzi yameendelea, jamaa akawa ndo anaendesha gari la yule dada, anampeleka ofisini na kumfata jioni. Jamaa taratibu akaanza kutumia hela ya yule dada huku akidai kuna mafao yake atalipwa soon so watakuwa poa kifedha.

Dada wa watu akachukua mkopo kama Mil 9 kwa ajili ya kuanza ujenzi lakini kumbe zikaingia kwenye mkumbo wa kuliwa. Ikafikia wakakubaliana eti jamaa aende Marekani, akifika kule akishaandaa mazingira atamchukua dada yetu wa kazini akaishi naye huko mambelez. Hela ya mkopo ikaisha, akakopa kwa washkaji hapa hela nyingine kama Mil 2 ya kuongezea ili kufanikisha safari.

Jamaa sasa ni muda kama wa miezi miwili toka aende USA na hajawahi hata kutoa contacts zake kwa dada yetu, huku jamaa wanamsakama kwa madeni yao (hasa hasa ile mil 2 ya nyongeza). Facebook jamaa hayuko active tena, inshort kapotea mazima. Dada wa watu saa hizi ni full stress, mshahara unakatwa hela ambayo hakuitumia, madeni yanamwandama, mpenzi kamkatia mawasiliano.

Kwa hiyo dada zetu mfanye uchunguzi wa kina kabla ya kugawa mioyo na mali wa wageni, wengine wamekuja kuchuma vilivyo vyetu kwa njia yoyote ile.
 
Pole kwa Dada not only in Tz tu hata nje wa dada waingizwa kwenye mitego kama hiyo
 
na dunia ya sasa wanaume wengi wanapenda dezo. utasikia ohh sitaki kuoa goli kipa nataka msomi kama mie maisha magumu. akishampata kila jukumu la mwanamke masikini wamama tulivyo na huruma ukishaambiwa ahh we lipia ada za watoto bwana si una mshaharaunatoa sasa utaacha watoto wasiende shule kisa baba yao kakataa kutoa ada. ,kesho utasikia mama nanihii bill ya maji hiii rekebisha basi yeye kutwa pesa zake katika viwalo ,starehe na wenzake baa vikao vya harusi nk.
 
sio kwa wageni tu hata hapa matapeli wa mapenzi ni wengi sana.

Ila kwa wenyeji ni rahisi kumtafuta na kujua info zake, lakini kwa huyu jamaa dada wa watu hata alikuwa hajui wapi aulizie habari zake.

Hafu dada mwenyewe ni mjanja, born town lakini kakutana. Imagine ndani ya miezi sita mapenzi yameshamiri mpaka jamaa kajitambulisha na hela kapewa.
 
Matapeli ni weng tu wabongo na wagen

Ivi inakuweje tugegedane afu hela zangu tna nikakope nikupe
Hii akili ya huyu Dada nadhan ndo mapenz nivuruge kumbe anajivuruga mwenyewe
 
Tatizo la akina dada wengi wana stress za kuolewa,akishaona umri umekimbia kidogo,rafiki zake wote wameolewa kabaki yeye anaanza kuchanganyikiwa.Bahati mbaya akikutana na mtoto wa mjini fasta anenda kujitambulisha kwao,akijua kabisa ndio mume ,kumbe wapi.

mimi kuna jamaa mmoja namjua tena yupo humu JF wametambulishana vizuri(pande zote mbili) mapaka vikao vya send off vinafanyika jamaa yupo, siku ya tukio lenyewe sasa(send off)jamaa hapatikani mpaka leo hii.

Akina dada tulieni haya mambo ya ndoa hayataki papara.
 
Inawezekana alikuwa desparate kutafuta ndoa.....ikamponza



Ila kwa wenyeji ni rahisi kumtafuta na kujua info zake, lakini kwa huyu jamaa dada wa watu hata alikuwa hajui wapi aulizie habari zake.

Hafu dada mwenyewe ni mjanja, born town lakini kakutana. Imagine ndani ya miezi sita mapenzi yameshamiri mpaka jamaa kajitambulisha na hela kapewa.
 
Matapeli ni weng tu wabongo na wagen

Ivi inakuweje tugegedane afu hela zangu tna nikakope nikupe
Hii akili ya huyu Dada nadhan ndo mapenz nivuruge kumbe anajivuruga mwenyewe

Hujagegedwa vizuri wewe,ukigegedwa vizuriiiiiiiii utatoa kila kitu chako.
 
Nina rafiki zangu wengi wa wacameroon na waghana, almost nafahamiana na wa cameroon wote walioko hapa dar maana wana chama chao na kila anauekuja lazima areport kwao. Raisi wa chama chao ni rafiki yangu.
Almost 95% wanaish kwa kuwalaghai akina dada. Mimi uwa naeaonea huruma lakini kasumba ya wadada wengi kujiingiza kichwa kichwa kwa maforeigners uwa naona ngoja wajifunze from their mistakes
 
Umenikumbusha kuna kisa kimoja kilitokea mahali fulani..
Bidada alikuwa anauza duka la kaka yake na akawa anauza pesa ndefu tu kwa siku. Akatokea kijana akawa anakuja kufunga mzigo mkubwa tu hapo dukani.....mazoea yakaenda baadae wakawa wapenzi. Yule kaka akawa anakuja na briefcase imejaa mahela anampa yule dada amuwekee then jioni anakuja kuichukua..bas dada wa watu kaona mwanaume si ndio huyu....?! Siku moja yule kaka akamwomba yule dada amuazime milioni arobaini kuna mahali amekwama na asubuhi yake atarudisha. Dada wa watu wala hakuwa na hiyana akampa.....asubuhi yake ilipofika simu ya yule kaka imezimwa na hajaonekana mpaka kesho.
 
Tatizo la akina dada wengi wana stress za kuolewa,akishaona umri umekimbia kidogo,rafiki zake wote wameolewa kabaki yeye anaanza kuchanganyikiwa.Bahati mbaya akikutana na mtoto wa mjini fasta anenda kujitambulisha kwao,akijua kabisa ndio mume ,kumbe wapi.

mimi kuna jamaa mmoja namjua tena yupo humu JF wametambulishana vizuri(pande zote mbili) mapaka vikao vya send off vinafanyika jamaa yupo, siku ya tukio lenyewe sasa(send off)jamaa hapatikani mpaka leo hii.

Akina dada tulieni haya mambo ya ndoa hayataki papara.

Da huyo jamaa naye noma sana.
 
Inawezekana alikuwa desparate kutafuta ndoa.....ikamponza

Hii inawezekana kwa sababu before that alikuwa na mtu ambaye ameshaoa, kila waikiachana wanarudiana. Sasa alivyokuja huyu ikawa rahisi kumteka. maana alikuwa so stragestically.
 
Inawezekana alikuwa desparate kutafuta ndoa.....ikamponza

Na hii ndo inawaponza weng wasichana

Mtu anahonga akitaraj ndo mshikaji atampenda na kumuoa kumbe zile hela na gar ndo anatanulia na wengine
Chezea mapenz

Angewekeza kwenye biashara Leo angefaidi
Huu upuuzi wa kuhongana,kujenga pamoja,kwangu not applicable kwa maisha ya boy/ gal friend
At end lazima mmoja ataumia tu.moyo wa mtu fumbo
 
Back
Top Bottom