Ishaka
Member
- Nov 1, 2011
- 74
- 12
Hii nikwa habari ya mechi ya chumbani. lazima tukubaliane kwamba tendo hili ndio muhimili muhimu wa ndoa, hivyo kwamba kama kuna mushkeli katika hilo basi hata mawasiliano ndani ya nyumba hudorora. Lakini tofauti na mechi za mipira nje uwanjani ambapo matokeo mazuri ni pale mbabe mmoja anapomshinda mwenzie, mechi ya ndoa inafana tu pale ambapo mke na mme wanapomaliza kwa ushindi wa sale ya kufungana mabao mengi! yaani kila mmoja kufikia kilele cha mlima wa mechi hiyo pasipo kumuacha mwenzi na maumivu au hamu ya kuendelea zaidi sababu ya msisimko wa mwili. Na jambo hili kusema kweli limeacha ndoa nyingi mguu pande kama sio solemba. Naamini, ili mechi ipate kuwa huru na haki yenye ufanisi kwa wote wawili na hatimaye mwisho muweze kupogezana au kupeana pole kwa shughuli pevu, kuna vitu muhimu (maandalizi) yanatakiwa. Aidha, mwanzishaji wa mechi muda huo ndiye anaweza kusababisha aina ya matokeo yatakayopatikana mwisho wa mechi. Sasa kina dada mliokwishayavulia maji nguo (ndoa) tuelezeni wanajamii na hasa wale mfumo dume hata katika tendo takatifu la ndoa, ni vipi ungependa kushauri nani amuanze mwenzie, na maandalizi kwa ujumla yahusishe kipi na kipi ambacho pengine ni nadra sana katika mechi za ndoa zingine. Asante karibu kuchangia.