Standards Person
JF-Expert Member
- Apr 22, 2021
- 668
- 861
Kimeumana ndani na nje ya bunge. Baada ya siku moja Rais kuwaambia wabunge wawakosoe Mawaziri na serikali, jana mapema bungeni wabunge Gambo na Gwajima wameibuka na hoja nzito. Gambo amehoji kutopandishwa madaraja kwa watumishi pamoja na waliokua watumishi hewa kutopewa mafao yao. Tuendelee kufuatilia tutasikia mengi.
Gwajima ameelezea namna ambavyo wafanyabiashara wameumizwa na watumishi wasiokua waadilifu. Watu kibao wametishiwa na wengine kuwekwa ndani kwa uonevu. Kuhusu wastaafu kusumbuliwa naibu spika nae akatia neno. Akauliza kama mtu unachukua michango yake inakuaje mwisho wa siku unamwambia akuletee barua ya ajira? Kama humjui mbona ulikua unachukua hela zake?
Hapo akaibuka Jenista Mhagama akadai kweli wastaafu wanasumbuliwa. Huyu nae bora angetuliatu ila naona wanajitetea maana wanaogopa kuzinguliwa. Tena atulie maana sasa watakosolewa, ahsante Rais wetu. Ila kilizidi kuumana pale ambapo Jeska Kishoa alikiri kufukuzwa CHADEMA lakini naibu spika akamwambia afute kauli kwani ofisi ya spika haina taarifa hiyo, yaaaaani pale kiliumana maana mkosaji kakubali kosa lakini msuluhishi au hakimu anasema hapana usikubali kihivyo bali futa kauli lengo nikwenda na katiba aisee kimeumana.
Huku mtaani nako nipiga nikupige. Ukisikia ya Songwe kwamba DC,RC, mbunge na mwenyekiti wa CCM hakuna picha angavu kwakuwa mkuu wa wilaya ni mbabe,utajua kimeumana. Kama mbunge anafanyiwa ubabe vipi mwananchi wa kawaida au huyo mnaiyemuita mnyonge? Sasa ukisikia ya Sengerema utajua mh.Rais kazi anayo ya kuisuka nchi upya.
Eti katibu wa mbunge anaambiwa na DC asizungumzie kero za wananchi kuhusu ardhi. DC amemtishia katibu huyo kumuweka ndani bali katibu alikomaa hadi mwisho. Kama wenyewe wanaotumia maviieghty wanagombana vipi wakikutana na waendesha baiskeli na wasukuma mkokoteni kwa punda?
Mh. Rais wawakilishi wako mikoani na wilayani baadhi nivivuruge na viburi. Hawapo kwaajili ya wananchi bali kwa ajili ya matumbo yao. Kwa tanga mjini hata lukuvi alizongwa akashindwa kufanya maamuzi sahihi. Mh Rais wasaidie watanzania wanamatumaini makubwa kwako
Gwajima ameelezea namna ambavyo wafanyabiashara wameumizwa na watumishi wasiokua waadilifu. Watu kibao wametishiwa na wengine kuwekwa ndani kwa uonevu. Kuhusu wastaafu kusumbuliwa naibu spika nae akatia neno. Akauliza kama mtu unachukua michango yake inakuaje mwisho wa siku unamwambia akuletee barua ya ajira? Kama humjui mbona ulikua unachukua hela zake?
Hapo akaibuka Jenista Mhagama akadai kweli wastaafu wanasumbuliwa. Huyu nae bora angetuliatu ila naona wanajitetea maana wanaogopa kuzinguliwa. Tena atulie maana sasa watakosolewa, ahsante Rais wetu. Ila kilizidi kuumana pale ambapo Jeska Kishoa alikiri kufukuzwa CHADEMA lakini naibu spika akamwambia afute kauli kwani ofisi ya spika haina taarifa hiyo, yaaaaani pale kiliumana maana mkosaji kakubali kosa lakini msuluhishi au hakimu anasema hapana usikubali kihivyo bali futa kauli lengo nikwenda na katiba aisee kimeumana.
Huku mtaani nako nipiga nikupige. Ukisikia ya Songwe kwamba DC,RC, mbunge na mwenyekiti wa CCM hakuna picha angavu kwakuwa mkuu wa wilaya ni mbabe,utajua kimeumana. Kama mbunge anafanyiwa ubabe vipi mwananchi wa kawaida au huyo mnaiyemuita mnyonge? Sasa ukisikia ya Sengerema utajua mh.Rais kazi anayo ya kuisuka nchi upya.
Eti katibu wa mbunge anaambiwa na DC asizungumzie kero za wananchi kuhusu ardhi. DC amemtishia katibu huyo kumuweka ndani bali katibu alikomaa hadi mwisho. Kama wenyewe wanaotumia maviieghty wanagombana vipi wakikutana na waendesha baiskeli na wasukuma mkokoteni kwa punda?
Mh. Rais wawakilishi wako mikoani na wilayani baadhi nivivuruge na viburi. Hawapo kwaajili ya wananchi bali kwa ajili ya matumbo yao. Kwa tanga mjini hata lukuvi alizongwa akashindwa kufanya maamuzi sahihi. Mh Rais wasaidie watanzania wanamatumaini makubwa kwako
