Kimenuka: Wakurugenzi wa NSSF wasimamishwa kazi kupisha uchunguzi

Its normal. Ni kutoelewa kwa watanzania wengi. Lakini normally ikiingia management mpya popote pale, lazima mkurugenzi (or wheoever) apewe nafasi kupanga timu yake. So you should expect this in most places....Bandari, TRA, Reli, ATC nk...lazima wakurugenzi wengi watapigwa chini....kibaya ni kwamba wengi wakipata hizi nafasi wanajisahau wanashindwa kujua kwamba ni kazi za mkataba!

Tutanyooka tuu.
 
Nami nawahi kuandika humu..

Weka habari ndugu...

Update yangu mie...nimeisoma toka kwa mkurugenzi mmojawapo katuandikia kututaarifu, kwenye group moja hivi
 
Watanzania tunasahau kwamba kazi ya uma ni ya kupokezana, hakuna mwenye ajira ya milele, ila sote tupo katika kuhakikisha kwamba taifa linasonga mbele , ndio maana serikali inaweka pesa kwenye elimu, ili watendaji wapatikane...tukiona unakotupeleka siko, unatupisha tunaendelea mbele...
 
sio vizuri kujambuli jukwaani,watu wametulia unakuja ghafla eti kimenuka!! Panga unachokisema weka na vyanzo
 
Mkuu stroke, kawaambie hayo wabunge wanaofikia hatua ya kutambulisha nafasi za kuchaguliwa eti ni 'majimbo yao'
 
Nimeambiwa na chanzo rasmi...
Wamesimamishwa kazi kwa tuhuma za ubadhirifu na uzembe
1. Operations Director - Chris Magori
2. Investment Director- Yusuph Kidula
3. Finance Director - Mrosso
4. HR Director- Chiku Matesa
5. Chief Accountant- Karanje
6. Project Manager- John Msemo Mzee wa DeRM towers
7. Investment Manager- Abdallah Mseli
8. Risk Director- Saidi Shemriwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…