Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
TAARIFA KWA UMΜΑ
Uongozi wa Kanda ya Kaskazini unawataarifu wanachama na umma kwa ujumla kuwa, viongozi wote wa Kanda hii ambao wanadaiwa kuweka saini kwenye waraka (petition) wataitwa kwa haraka ili;
1. Kuthibitisha kama kweli saini zilizowekwa ni zao, na kama walihusika moja kwa moja kwenye maandalizi au usambazaji wa petition hiyo.
2. Kufafanua dhamira yao, ikiwa ni kweli wanapendekeza mwelekeo tofauti na msimamo wa chama.
Baada ya hatua hizo kukamilika, chama kitapitia kwa kina maelezo na uthibitisho utakaotolewa, na hatimaye kitatoa msimamo rasmi kuhusu hatua zinazopaswa kuchukuliwa dhidi ya wahusika, kulingana na taratibu na maadili ya chama.
Tukijiridhisha kuwepo kwa USALITI na njama za kukisaliti chama, hatutasita kuchukua hatua kali za Kikatiba na Kikanuni dhidi ya wote watakaobainika kuhusika.
Tunawasihi wanachama wote kuendelea kuwa watulivu na waaminifu kwa chama wakati mchakato huu ukiendelea.
Imetolewa leo na;
Samwel Welwel
Mwenyekiti - Kanda ya Kaskazini
Pia soma: Waraka wa wagombea 2020 na watia nia wa ubunge 55 wa CHADEMA. Wapinga chama kususia uchaguzi mkuu
- Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025