Kiloleni Tabora: Katibu wa CHADEMA apigwa na Polisi na kumweka ndani bila kumwambia kosa lake

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Huyu ni Katibu wa Chadema kata ya kiloleni Tabora manispaa akiwa amelazwa katika hospital ya rufaa Tabora baada ya kupewa kipigo kikali kutoka kwa maafisa wa jeshi la Polisi, ambao walimkamata tangu tarehe 18.10.2018 na kumshikilia bila kumwambia kosa lake na leo amekuwa hospital

 
Sura iko wapi kwenye hiyo picha
Sura siyo issue sana, kubwa ni je kapigwa kweli bila kuambiwa kosa lake? Pamoja na hayo Polisi hatakiwi kumpiga mtuhumiwa kama hajawafanyia fujo, na hata kama mtuhumiwa atawafanyia fujo wanatakiwa kwanza watumie ujuzi wao kumdhibiti, na si kuanza kutumia nguvu ya ziada. Matukio kama haya tusiweke ushabiki wa kichama kwani polisi haohao kesho watakuja kwako kama si kwa familia yako.
 
May be he/she is guilty until proved innocent. It is simply a disregard to the Principles of Natural Justice!
 
Basi tunakoelekea ni kugumu sana askari kutembea na kuchagua mtu barabarani/baadhi ya nyumba na kudabua mtu kama vichaa na kumminyia kipigo bila sababu.
 
Ninyi ni taifa la wajinga mpigwe tuu hakuna namna
 

SURA NI YA MUHIMU ILI KUALALISHA HIYO PICHA.
SI SAHIHI KUMPIGA MTU KAMA HAJAFANYA FUJO AU KUKATAA AMRI HALALI. LAKINI MASWALI HAYA KWA KIPINDI HIKI CHA UONGOZI NI VIGUMU SANA KUPATA MAJIBU YAKE
 
May be he/she is guilty until proved innocent. It is simply a disregard to the Principles of Natural Justice!


Tabora region is under RC Aggrey Mwanri Mzee wa SUKUMA NDANI na FYEKELEA MBALI..!
Je, inaqwezekana RC Mwanri na yeye anaanza kuwasukuma na kuwafyekelea mbali WAPINZANI? Naomba mwenye Tube ya RC akiongelea hii issue ya Diwani wa CHADEMA kusukumwa ndani..!!!
 
Hapo hospitali yuko chini ya ulinzi au yuko huru? Na alifikishwa hapo na Nani?
 
Acheni wizi,eti kisa kada wa chadema,mkipewa discpline mnadai kuonewa,na bado
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…