Kilimo kwa wasio na ajira

Kilimo kwa wasio na ajira

Superbug

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2018
Posts
15,819
Reaction score
40,320
Hivi mfano serikali ikakusanya vijana wanaozurura dar kama laki tano

Halafu wakawapeleka mikoa ya kilimo kama ruvuma rukwa mbeya

Wakawafungulia shamba moja kubwa LA mahindi kwa ukubwa wa eka LAki nane

Halafu wakawanunulia matrekta elfu moja ya kuwalimia

Hivi hatauwaga umaskini kweli?

Naomba chalenji ya hili wazo langu
 
Mahindi hayo kwa ukubwa wa shamba hilo LA ekari 800,000 utatoa magunia milioni 16 haya yote yauzwe sudani kusini na somalia wallah umaskini tutakuwa tumewaondolea vijana laki tano kwa mpigo
 
Mahindi hayo kwa ukubwa wa shamba hilo LA ekari 800,000 utatoa magunia milioni 16 haya yote yauzwe sudani kusini na somalia wallah umaskini tutakuwa tumewaondolea vijana laki tano kwa mpigo
Watahitaji na semina ya jinsi ya kutumia hizo fedha pia maana tatizo si tu kupata fedha bali na namna ya kuzitumia.
 
Hivi mfano serikali ikakusanya vijana wanaozurura dar kama laki tano

Halafu wakawapeleka mikoa ya kilimo kama ruvuma rukwa mbeya

Wakawafungulia shamba moja kubwa LA mahindi kwa ukubwa wa eka LAki nane

Halafu wakawanunulia matrekta elfu moja ya kuwalimia

Hivi hatauwaga umaskini kweli?

Naomba chalenji ya hili wazo langu

Unauhakika wataweza kuingia kwenye umande bila kushikiwa bakola?

Inabidi uwape na nyagi na ndumu za kutosha la watakutangulia daraja la manzese
 
Kwa kufanya hivyo utakuwa umewaongezea umasikini! Kilimo siyo rahisi Kama
unavyofikiria...
 
Watahitaji na semina ya jinsi ya kutumia hizo fedha pia maana tatizo si tu kupata fedha bali na namna ya kuzitumia.
hawapewi fedha kama fedha, wanapewa pembejeo
 
Hivi mfano serikali ikakusanya vijana wanaozurura dar kama laki tano

Halafu wakawapeleka mikoa ya kilimo kama ruvuma rukwa mbeya

Wakawafungulia shamba moja kubwa LA mahindi kwa ukubwa wa eka LAki nane

Halafu wakawanunulia matrekta elfu moja ya kuwalimia

Hivi hatauwaga umaskini kweli?

Naomba chalenji ya hili wazo langu
Only if serikali ingekuwa na akili hiyo. Tatizo ni kwamba serikali kwa sasa kama vile wamekisahau kilimo.
 
Mahindi hayo kwa ukubwa wa shamba hilo LA ekari 800,000 utatoa magunia milioni 16 haya yote yauzwe sudani kusini na somalia wallah umaskini tutakuwa tumewaondolea vijana laki tano kwa mpigo
Tatizo sio kilimo watu wanalima sana ila shida inakuja kwenye kupata soko la uhakika, serikali yenyewe inafunga mipaka watu wasiuze mazao nje wanaishia kuuza gunia la mahindi 18000 sasa si hasara hiyo
 
Back
Top Bottom