Mlyuha
JF-Expert Member
- Apr 27, 2015
- 239
- 94
Nimekuwa nikifuatilia kwa makini mashindano ya mapinduzi yanayoendelea sasa kule Zanzibar. Nimegundua kuwa Ligi ya Zanzibar ni bora kuliko ya bara hasa kwenye maandalizi ya wachezaji wa timu ya Taifa. Timu zao zote zimeundwa na wachezaji wazalendo na pia wanaonyesha mchezo mzuri sana. Kinachowakwaza ni uzoefu tu ambao naamini utapatikana muda si mrefu na hizo timu zitakuwa tishio kwa afrika mashariki. Tofauti na timu zetu za bara zimejaza ma 'professionals' ambao hawaisaidii kwa lolote timu yetu ya Taifa. Ni wakati muafaka sasa TFF kuamka na kuiga kwa ZFF ambao wameona mbali sana. Hongereni ZFF.