Kilimanjaro: Kauli ya Rais 'Nimewasamehe kwa kuchagua upinzani'. Je, ni kosa kuchagua chama pinzani?

Kilimanjaro: Kauli ya Rais 'Nimewasamehe kwa kuchagua upinzani'. Je, ni kosa kuchagua chama pinzani?

Hilo jani halimaanishi msamaha tuu bali amani na furaha. Mzee mzima kakurupuka..
 
Hivi hao watu WANAOMSIMAMISHA raisi kwenye msafara wake hutokaga wapi? taarifa za kuwa raisi atapita hutolewa wapi? Hii ni mipango inayojulikana kuwa msafara utapita hapo (muda hautajwi( na watu ANAANDALIWA kumpokea. Ajabu ni kuwa INARIPOTIWA kuwa eti Wananchi wameusimamisha msafara. Sipidi ya motakedi ya Prezidaaa twajua ina kasi ya ajabu. Kwa kasi hiyo watu wakusanyane barabarani (tena sehemu moja) na WASHINIKIZE kuhutubiwa....Hii ina makengeza. Msafara huo ulokuwa unatoka Arusha mbona hapa Kikatiti sijaona ukisimamishwa? Tuwe WAKWELI katika hili maana limepitiliza uhalisia...
 
Kwa kauli aliyotamka Mhe.Raisi kilimanjaro kwa kusema amewasamehe kwa kuchagua upinzani, kuna haja gani ya vyama vingi?

Jimbo la Hai kuchagua chama pinzani ni kosa?

Hatambui kuichagua CCM toka 1995 ndio kosa kubwa na ndio sababu ya kudolola kwa uchumi wa TANZANIA toka uhuru.

View attachment 502815

Tunaomba viongozi wetu wawe wanaandikiwa hotuba.

Mbeya walikuja waafrika kusini walitaka kujenga kiwanda cha kuzalisha umeme kupitia taka chafu serikali ilikataza tokana Mbeya Mjini na Mbeya kiujumla kuwa na wafuasi wengi wa vyama pinzani wakaja DAR wajerumani nao walitaka kufanya wa-afrika kusini serikali ikazuia.

Moshi kisa upinzani ujenzi wa stendi ukahamishiwa anakotaka Rais.

Hatuwezi kuendelea kwa staili ya kusema CCM ITAWALE daima.

Mhe. Rais tunaomba u-deal na mafisadi wa serikali zilizopita hata kama wanatoka CCM mbona nchi za wenzetu watu wanafungwa miaka mingi tokana na hatia za 1960 shuka chini?

Wewe serikali iliyopita tu unashindwa? Kamata Tibaijuka, Ngeleja, Chenge na wengine wote funga mpaka Lowassa.
ndio ni kosa. upinzani ni hovyoo sanaaaaa
 
Kwani wewe huamini kwamba Magu kandinda kwa golu la mkoni? Huyu jamaa hakushinda uchaguzi .Anausongo sana na upinzani.Akili yake nyingi katika awamu yake hii ni kuodhofhsha upinzani. Ili uchaguzi ujao ajaribu khshinda kiuhalali.Tatizo letu watanzania njaa zinatusumbua sana.Viongozi wengine wa upinzani wanakubali kurubuniwa na majambazi ccm kurahisi kusaliti vyama vyao.Wapinzanu wanatakuqa wawe imara sana ili kumuondoa mkoloni ccm madarakani.
Najua hakushinda ila alitangazwa tu na kile kizee cha kondoa...

Uchaguzi ujao tunaye..
 
Mkuu umesema na langu,, yaani mimi sasa hivi hata sihangaiki naye kabisa nimeshajua tumekula hasara sasa ya nini kukaa najinyima raha kiasi hicho? Yeye afanye tu anavyotaka lakini 2020 haki ya nani hata atambalie tumbo badala ya push-up hapati kura yangu!! Kwani huko Moshi ameona kuna mahali ma Mangi wamelegalega katika kupiga maendeleo?
Sasa hivi anafanya maigizo tu...

ATATUKUTA..
 
Kwani walimwomba msamaha?
Hakuwa na cha kuwaambia, unadhani angesema nini? Ccm mkoa wa Kilimanjaro ndiyo wenye ziara, wanadhani Rais atawasaidia kurudiwa na wananchi. Walishapewa talaka tatu, wasahau
 
Hili lizee linajisahau sana, halijui hii ni nchi ya kidemokrasia,
kila mwananchi ana haki ya kumchagua kiongozi anayemuona kuwa ni bora kwake. Sasa shida hapo iko wapi???
Hii ni nchi yetu sote bila kujali chama, Kabila, dini, rangi, wala asili ya lugha na mkoa utokao.
Anadhani wanachama na washabiki wa ccm ndo watanzania ila wengine waliosalia ni wazamiaji!!!!
Eti nimewasamehe kwa kuchagua upinzani!!!! Kwani wao sio watanzania!!! Na je kwani wao hawana sifa za kuwa viongozi???!!!!
Shubamiiiit!!!
 
Rais amewajibu wananchi baada ya kubebe majani kama ishara ya kumuomba msamaha.
Rais amesema nimewaelewa na nimewasamehe.. sasa hayo ya kusema sababu ni kuchagua upinzani unatakiwa kuwauliza walio omba msamaha.
Wanaccm ndiyo waliojibebesha hayo majani. Kwani Kilimanjaro imeanza kuukubali upinzani leo?
 
Yani Mimi hata ndugu yangu tu akiniambia anapenda CCM ajue asikae anililie shida hata siku moja bora MTU uwe neutral ULA kuna miwatu inashabikia ujinga ambao mpaka kiongozi wao wakiona ujinga wakikataaa nao ndo wanakataaa sasa si uzombie huu jamani. Dah sijui Nani katuloga
 
Upinzani uko wapi? Amkeni naona bado mnakula mbonji nzito, upinzani ni saccos za watu,kama tungekuwa na upinzani imara kama kenya nadhani hata kina jpm wasingebeza upinzani wao tatzo ccm inajiamn maana inajua hakuna wapinzani ni wanafiki tu
Tanzania hakuna upinzani bora ufe tuwe na chama kimoja then tuchagulie humo watu
 
Back
Top Bottom