Kilimanjaro Express yaamriwa kumlipa Leonard milioni 300 kwa kusababisha ajali iliyomuua mwanae

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,445
7,813
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salam imeamuru kampuni ya Kilimanjaro Truck Company Limited, inayomiliki mabasi ya Kilimanjaro Express kulipa fidia ya Sh300 milioni kutokana na moja ya mabasi yake kugonga gari dogo lililokuwa linatumiwa na familia na kusababisha kifo cha mmoja wa wanafamilia.

Amri hiyo imetolewa leo Jumatano Desemba 21, 2022 na Jaji Leila Mgonya katika hukumu ya kesi ya madai iliyofunguliwa na mfanyabiashara Leonard Paul Kisenha dhidi ya kampuni hiyo, Roland Sawaya (mkurugenzi mtendaji na mmiliki wa kampuni hiyo) na dereva wa basi hilo, Mjahid Mohamed.

Ajali hiyo ilitokea Desemba 24, 2021 eneo la Kerege wilayani Bagamoyo mkoani Pwani, wakati Kisena alipokuwa akisafiri na familia yake kuelekea kwao Kilimanjaro, akitumia gari lake binafsi.

Katika ajali hiyo, basi la Kilimanjaro aina ya Scania liliacha njia na kuliparamia gari la Kisena aina ya Toyota Landcruiser.

Mtoto wake mmoja wa kike aliyekuwa na umri wa miaka 16 alifariki dunia na Kisena, mkewe na mtoto wao mwingine wa kiume walinisurika japo walipata majeraha.
 
Mh sawaya, atazitoa kweli hizo pesa

Ova
Mdai akikaza kwa njia sahihi, hatakua na option. Maana hapo mdai akipata guidance sahihi ya kisheria, anaweza kwenda mahakamani kuiomba mahakama kukazia hukumu kuwa Sawaya alipe hiyo hela, ndani ya muda fulani na asipofanya hivyo mahakama itatoa ruhusa ya mali zake (eg hayo mabasi) kukamatwa popote yatakapoonekana.

Japokua bwana Sawaya na yeye bado ana haki ya kukata rufaa, so sio kwamba kesi ndo imeisha kabisa hii, ngoma bado mbichi. Hesabu angalau miaka 3-5 hivi hapo hadi hili sebene kuisha.
 
Mdai akikaza kwa njia sahihi, hatakua na option. Maana hapo mdai akipata guidance sahihi ya kisheria, anaweza kwenda mahakamani kuiomba mahakama kukazia hukumu kuwa Swaya alipe hiyo hela, ndani ya muda fulani na asipofanya hivyo mahakama itatoa ruhusa ya mali zake (eg hayo mabasi) kukamatwa popote yatakapoonekana.
Japokua bwana Sawaya na yeye bado ana haki ya kukata rufaa, so sio kwamba kesi ndo imeisha kabisa hii, ngoma bado mbichi. Hesabu angalau miaka 3-5 hivi hapo hadi hili sebene kuisha.

Mali za sawaya ni za kampuni.

Je watakamata mali za kampuni?

Na je sawaya amemkana Dereva sasa inaonekana hii ajali ilisababishwa na dereva mwingine atadai nani
 
Mali za sawaya ni za kampuni.
Je watakamata mali za kampuni?
Si mtaalam sana wa kisheria, ila hapo uwezekano upo. Kumbuka ndege ya ATCL ilivyokamatwa kwa deni ambalo Tanzania ndo inadaiwa. Ilikamatwa mali ya ATCL wakati mwenye deni ni nchi (Tanzania), na sio kampuni (ATCL). Anyways, wataalamu wa sheria wanaweza kutufumbua macho zaidi, nisije nikawa napotosha.
 
Si mtaalam sana wa kisheria, ila hapo uwezekano upo. Kumbuka ndege ya ATCL ilivyokamatwa kwa deni ambalo Tanzania ndo inadaiwa. Ilikamatwa mali ya ATCL wakati mwenye deni ni nchi (Tanzania), na sio kampuni (ATCL). Anyways, wataalamu wa sheria wanaweza kutufumbua macho zaidi, nisije nikawa napotosha.
Kilichoiokoa ile ndege ni serikali ilidai ndege ile ni ya Rais hivo ilitumika diplomasia, huyu hachomoki kwa sababu mahakama imeshajiridhisha gari haikuwa na Bima na dereva alifanya uzembe,

Japo mimi pia sio mtaalamu wa sheria lakini hapa huyu jamaa ni wazi hachomoi, gari imeua na kaharibu mali ya watu
 
Si mtaalam sana wa kisheria, ila hapo uwezekano upo. Kumbuka ndege ya ATCL ilivyokamatwa kwa deni ambalo Tanzania ndo inadaiwa. Ilikamatwa mali ya ATCL wakati mwenye deni ni nchi (Tanzania), na sio kampuni (ATCL). Anyways, wataalamu wa sheria wanaweza kutufumbua macho zaidi, nisije nikawa napotosha.
Aliyekwambia ATCL inamiliki ndege nani?
 
Back
Top Bottom