Siku chache baada ya Papaa Koffi Langa Mususu Olomide kukamatwa Kinshasa na kupandishwa kizimbani kisha kuhukumiwa kifungo taarifa zisizo na mashaka kutoka CongoDR zimebaini kilichomponza Koffi ni uswahiba wake na hasimu mkubwa wa Rais Kabila Papaa Moise Katumbi.
Ukweli huo umebainika baada ya mwendesha mashtaka kumtia hatiani Koffi na kumfunga bila faini pamoja mhusika aliyefanyiwa tukio hilo mnenguaji wake kukiri kuwa hakupigwa na teke na Koffi.
Koffi amekuwa na urafiki wa muda mrefu na Katumbi ambaye ni mmiliki wa timu ya TP Mazembe ambaye awali alitangaza kugombea Urais wa CongoDR na lakini akaishia kufungwa akiwa nje ya Congo kwa madai ya kuhifadhi wahamiaji na kukwepa kodi.
Koffi aliwahi kumtungia wimbo Moise Katumbi na uswahiba wao pia unahusishwa na ujenzi wa ngome nzito ya kimkakati inayoweza kumshinda Kabila katika uchaguzi. Tayari Katumbi yuko nchini UK uhamishoni alikoenda akitokea Afrikakusini alikokuwa kimatibabu na hukumu ya miaka mi3 jela ilimkuta akiwa huko.
Ukweli huo umebainika baada ya mwendesha mashtaka kumtia hatiani Koffi na kumfunga bila faini pamoja mhusika aliyefanyiwa tukio hilo mnenguaji wake kukiri kuwa hakupigwa na teke na Koffi.
Koffi amekuwa na urafiki wa muda mrefu na Katumbi ambaye ni mmiliki wa timu ya TP Mazembe ambaye awali alitangaza kugombea Urais wa CongoDR na lakini akaishia kufungwa akiwa nje ya Congo kwa madai ya kuhifadhi wahamiaji na kukwepa kodi.
Koffi aliwahi kumtungia wimbo Moise Katumbi na uswahiba wao pia unahusishwa na ujenzi wa ngome nzito ya kimkakati inayoweza kumshinda Kabila katika uchaguzi. Tayari Katumbi yuko nchini UK uhamishoni alikoenda akitokea Afrikakusini alikokuwa kimatibabu na hukumu ya miaka mi3 jela ilimkuta akiwa huko.