Kilichomponza Trump hiki hapa

Kilichomponza Trump hiki hapa

Kingsmann

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2018
Posts
5,197
Reaction score
19,465
Bwana Trump na timu yake ya kampeni wamekosea mahesabu na inaenda kuwagharimu vibaya sana. Matumaini ya kushinda ni chini ya 20%.

Kwenye siasa propaganda na figisu huwa hazikosekani. Kama ambavyo Dem walilalamika mwaka 2016 kufanyiwa figisu na bwana Trump, safari hii kibao kimegeuka na mtetezi wa kiti cha urais ndio analalamika kufanyiwa figisu.

Kutokana na COVID19 safari hii kulikuwa na njia 2 za kupiga kura, ya kwanza ni moja kwa moja kwenye vituo vya kupigia kura na ya pili ni kwa njia ya posta.

Trump akawaambia wafuasi wake wakapigie kura moja kwa moja kwenye vituo vya kupigia kura, waachane na posta. Huku nyuma ya pazia akajaribu kuingilia na kuzuia utendaji wa mifumo ya posta ili kura za Biden zisiweze kufika kwa wakati kwenye vituo vya majumuisho. Pia alidhani ataweza kusitisha uhesabuji wa kura za posta baada ya kura za vituoni kuhesabiwa na ndio maaana anashout muda wote STOP THE COUNT.

Hii ndio ilifanya ajitangaze mshindi mapema kwa sababu kura za mwanzo kabisa zilizopigwa kwenye vituo zilionesha anaongoza. Lakini akasahau kwamba Biden yeye aliwahamasisha wafuasi wake watumie njia ya posta ili kujikinga na corona. Hapo ndio meza ilipompindukia Trump.

Pia alidhani ataweza kusitisha uhesabuji wa kura za posta baada ya kura za vituoni kuhesabiwa na ndio maaana anashout muda wote STOP THE COUNT. Amejaribu kila njia mpaka kufile lawsuit kuzuia uhesabuji wa kura za posta usitishwe lakini wapi. Wananchi nao wamekomaa EVERY VOTE MUST BE COUNTED.

Kwa mtu mwenye busara alitakiwa awe ameshadeclare kushindwa na aangalie mambo mengine sababu hakuna namna ataweza kushinda electoral votes za states zote zilizobakia ambazo ili afikishe kura 270 inabidi ashinde zote. There is no way.

Nadhani by January tutakuwa tumeshamsahau bwana Trump.

Screenshot_20201106-100330.jpg
 
Kikubwa kabisa kilichomponza Trump ni tabia.

Hakubadilika hata kidogo aliposhinda urais.

Tabia na mwenendo wake [character] watu wengi sana hawapendezwi nayo.

Kwa mfano, Trump hakupaswa kushindwa kwenye jimbo kama la Arizona. Jimbo la John McCain. Shujaa na mateka wa vita.

Ndiyo, enzi za uhai wake McCain, yeye na Trump zilikuwa haziivi.

Lakini, hata baada ya McCain kufariki, Trump bado tu akaendelea kumsema vibaya marehemu.

Sasa kwa tabia kama hiyo, unategemea kweli angeshinda kwenye jimbo analotokea McCain?

Arizona wanajivunia kuwa na Seneta kama McCain.

Trump kuendeleza bifu na marehemu kuliwaboa watu wa Arizona na wakaamua kumpa fundisho kwenye sanduku la kura.

La, kwenye hali ya kawaida, Arizona ni jimbo la Republican.

Hata 2016 Trump alishinda Arizona tena kwa kura za kutosha kabisa.

Sasa tabia na mwenendo mbaya, ongeza na corona juu yake, ni vigumu sana kushinda.

Kama seneti Republicans wataendelea kuwa na viti vingi, na kule kwenye chemba ya wawakilishi wameongeza viti, ni wazi kabisa watu walio wengi hawaipendi tu tabia yake na wanataka aondoke.

Biden kamwe hajawahi kuwa mgombea mzuri. Kawekwa tu hapo awe Rais wa mpito.
 
Trump hana tena matumaini ya kushinda. Anaishia kulalamika tu kwamba anahujumiwa na kufanyiwa figisu.
 
Yani tume ya uchaguzi haimsikilizi rais!
Fukuza yote unda nyingine.

Bw Trump chukua ushauri huu.
 
Trump ananyweshwa dozi yake mwenyewe. Hii ilikuwa tweet ya mwaka 2012 akidai hakuna haja ya kufanya recount. Atulie tu sasa dawa imuingie kisawasawa!

F51F0A7B-8DDF-4A9A-8E07-FA6FC3BAE1CF.jpeg
 
Kikubwa kabisa kilichomponza Trump ni tabia.

Hakubadilika hata kidogo aliposhinda urais.

Tabia na mwenendo wake [character] watu wengi sana hawapendezwi nayo.

Kwa mfano, Trump hakupaswa kushindwa kwenye jimbo kama la Arizona. Jimbo la John McCain. Shujaa na mateka wa vita.

Ndiyo, enzi za uhai wake McCain, yeye na Trump zilikuwa haziivi.

Lakini, hata baada ya McCain kufariki, Trump bado tu akaendelea kumsema vibaya marehemu.

Sasa kwa tabia kama hiyo, unategemea kweli angeshinda kwenye jimbo analotokea McCain?

Arizona wanajivunia kuwa na Seneta kama McCain.

Trump kuendeleza bifu na marehemu kuliwaboa watu wa Arizona na wakaamua kumpa fundisho kwenye sanduku la kura.

La, kwenye hali ya kawaida, Arizona ni jimbo la Republican.

Hata 2016 Trump alishinda Arizona tena kwa kura za kutosha kabisa.

Sasa tabia na mwenendo mbaya, ongeza na corona juu yake, ni vigumu sana kushinda.

Kama seneti Republicans wataendelea kuwa na viti vingi, na kule kwenye chemba ya wawakilishi wameongeza viti, ni wazi kabisa watu walio wengi hawaipendi tu tabia yake na wanataka aondoke.

Biden kamwe hajawahi kuwa mgombea mzuri. Kawekwa tu hapo awe Rais wa mpito.
Well said. A lesson to chew.
 
Kama atashindwa atakuwa kaponzwa na tabia yake ya kutokubali kuwajibika kwa masuala mbalimbali yanayotokea. Hua always anatafuta wa kumlaumu mambo yanapo enda kombo. Ni jamii ya wale watu mambo yakienda vizuri anataka awe mbele kwenye wanao pewa sifa ila yakiharibika anatafuta wa kumuweka mbele ashambuliwe. Issue ya corona ilinifanya nimdharau huyu mzee
 
Brisbane, Australia
November 6, 2020

We want a fair election’: Donald Trump Jr​


Donald Trump Jr says his father is “a fighter” and will continue to fight for a fair election. His remarks come after President Trump spoke about a “tremendous amount of litigation” taking place in a bid to win the presidential election.

The president's campaign called for voting to stop in several crucial states until Republicans are allowed to view the ballots as they are counted.

“We want a fair election, we want all legal votes counted,” Mr Trump told a crowd in Atlanta, Georgia. “I’ve lost all faith in the process, no one believes that this is real. “We’re going to fight each and every one of these (states).”
Source : Sky News Australia
 
Kiburi, Majino yamemshusha Sasa aende zake akapambane na apartment zake
 

Attachments

  • VID-20201105-WA0015.mp4
    727.1 KB
Kilichomponza ni kashindwa ku-deliver!

Mpaka sasa USA is great kwenye vitu viwili tu.

1- Defense spending.

2- Idadi kubwa ya watu wazima wanaoamini angels are real.
 
Kilichomponza ni kashindwa ku-deliver!

Mpaka sasa USA is great kwenye vitu viwili tu.

1- Defense spending.

2- Idadi kubwa ya watu wazima wanaoamini angels are real.
Kashindwa ku deliver kitu gani?

Angekuwa kashindwa ku deliver ungeona hata down ballot candidates wakishindwa vibaya sana.

Hilo halijatokea.

Ni character yake ndo iliyomwangusha.

Hakubadilika alipochaguliwa kuwa Rais.
 
Kikubwa kabisa kilichomponza Trump ni tabia.

Hakubadilika hata kidogo aliposhinda urais.

Tabia na mwenendo wake [character] watu wengi sana hawapendezwi nayo.

Kwa mfano, Trump hakupaswa kushindwa kwenye jimbo kama la Arizona. Jimbo la John McCain. Shujaa na mateka wa vita.

Ndiyo, enzi za uhai wake McCain, yeye na Trump zilikuwa haziivi.

Lakini, hata baada ya McCain kufariki, Trump bado tu akaendelea kumsema vibaya marehemu.

Sasa kwa tabia kama hiyo, unategemea kweli angeshinda kwenye jimbo analotokea McCain?

Arizona wanajivunia kuwa na Seneta kama McCain.

Trump kuendeleza bifu na marehemu kuliwaboa watu wa Arizona na wakaamua kumpa fundisho kwenye sanduku la kura.

La, kwenye hali ya kawaida, Arizona ni jimbo la Republican.

Hata 2016 Trump alishinda Arizona tena kwa kura za kutosha kabisa.

Sasa tabia na mwenendo mbaya, ongeza na corona juu yake, ni vigumu sana kushinda.

Kama seneti Republicans wataendelea kuwa na viti vingi, na kule kwenye chemba ya wawakilishi wameongeza viti, ni wazi kabisa watu walio wengi hawaipendi tu tabia yake na wanataka aondoke.

Biden kamwe hajawahi kuwa mgombea mzuri. Kawekwa tu hapo awe Rais wa mpito.
Baba umeua we ninoma
 
Kashindwa ku deliver kitu gani?

Angekuwa kashindwa ku deliver ungeona hata down ballot candidates wakishindwa vibaya sana.

Hilo halijatokea.

Ni character yake ndo iliyomwangusha.

Hakubadilika alipochaguliwa kuwa Rais.
Upande wa tabia zake i agree.,
And Joe is the opposite of that
 
Back
Top Bottom