GE2025 Kiliba wa TAHLISO: Ni muhimu kufanya maamuzi ya kuchagua viongozi walio bora bila kujali hisia na mihemko

GE2025 Kiliba wa TAHLISO: Ni muhimu kufanya maamuzi ya kuchagua viongozi walio bora bila kujali hisia na mihemko

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
2,439
Reaction score
6,691
Wakuu,

Rais wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO), Geofrey Kiliba, amewataka vijana nchini kutambua nafasi yao katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, akisema matokeo ya uchaguzi huo yatakuwa na mchango mkubwa katika mustakabali wao.

Akizungumza katika kipindi cha Maswali na Majibu kinachoongozwa na mtangazaji Wilberforce Ngoto kupitia Jambo TV, Kiliba amesema vijana wanapaswa kufuatilia kwa makini sera na ahadi zinazotolewa na wagombea, ili kutathmini uwezo wao wa kuzitekeleza kwa vitendo.

“Sisi kama vijana wa leo wa Kitanzania, lazima tujue mustakabali wa maisha yetu unategemea sana uchaguzi wa mwaka 2025. Misingi ya namna ya upatikanaji wa ajira, mazingira wezeshi ya kumuinua kijana na kumfanya awe huru inategemea sana mbegu inayopandwa na viongozi wetu,” amesema

 
Rais wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO), Geofrey Kiliba, amewataka vijana nchini kutambua nafasi yao katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, akisema matokeo ya uchaguzi huo yatakuwa na mchango mkubwa katika mustakabali wao.

Akizungumza katika kipindi cha Maswali na Majibu kinachoongozwa na mtangazaji Wilberforce Ngoto kupitia Jambo TV, Kiliba amesema vijana wanapaswa kufuatilia kwa makini sera na ahadi zinazotolewa na wagombea, ili kutathmini uwezo wao wa kuzitekeleza kwa vitendo.

“Sisi kama vijana wa leo wa Kitanzania, lazima tujue mustakabali wa maisha yetu unategemea sana uchaguzi wa mwaka 2025. Misingi ya namna ya upatikanaji wa ajira, mazingira wezeshi ya kumuinua kijana na kumfanya awe huru inategemea sana mbegu inayopandwa na viongozi wetu,” amesema.

Kiliba ameongeza kuwa ni muhimu vijana kuangalia kama ahadi na sera zinazotolewa na wagombea zinaendana na vitendo vyao, pamoja na namna wanavyowasilisha ujumbe wao wanapokuja kuomba kura.

 
Back
Top Bottom