Mafyangula
JF-Expert Member
- Jan 16, 2025
- 505
- 887
Mwenyekiti wa Kampeni ya Kitaifa ya Mama Asemewe Bw. Geofrey Kiliba amesisitiza umuhimu wa kila mmoja kuwajibika kulinda amani ya Tanzania, akitaka pia wale wote wenye maoni na hisia tofauti kutumia njia rafiki za kutaka mabadiliko badala ya maneno ya kichochezi na yenye kuhatarisha amani na hatua za maendeleo zilizopigwa pamoja na ustawi wa jamii.
Kiliba ametoa wito huo leo Jumanne Oktoba 14,2025 wakati alipozungumza na wanahabari Mkoani Kagera akiwasihi Vijana pia kujiepusha na kutumia kwenye matendo ovu na kuwataka kujifunza kukosa umakini na umoja kwa Vijana wa Nepal na Madagascar kulivyozisambatarisha nchi hizo na kuua ustawi wa jamii yake.
"Hatukatai kuwa Tanzania yetu sio peponi tupo duniani na mojawapo ya sifa ya uwepo wetu duniani ni pamoja na kukutana na kukabiliana na changamoto mbalimbali. Hatuna sababu ya kuua ama kudhohofisha msingi wa maendeleo tuliyonayo kwasababu ya madai ya kutatua changamoto zilizopo." Amekaririwa Kiliba akiwaambia wanahabari.
Kiliba ametoa wito huo leo Jumanne Oktoba 14,2025 wakati alipozungumza na wanahabari Mkoani Kagera akiwasihi Vijana pia kujiepusha na kutumia kwenye matendo ovu na kuwataka kujifunza kukosa umakini na umoja kwa Vijana wa Nepal na Madagascar kulivyozisambatarisha nchi hizo na kuua ustawi wa jamii yake.
"Hatukatai kuwa Tanzania yetu sio peponi tupo duniani na mojawapo ya sifa ya uwepo wetu duniani ni pamoja na kukutana na kukabiliana na changamoto mbalimbali. Hatuna sababu ya kuua ama kudhohofisha msingi wa maendeleo tuliyonayo kwasababu ya madai ya kutatua changamoto zilizopo." Amekaririwa Kiliba akiwaambia wanahabari.