Kila wakiita interview wananikuta nina ukwasi wa kutosha hivyo napuuzia

Kila wakiita interview wananikuta nina ukwasi wa kutosha hivyo napuuzia

Kazanazo

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2023
Posts
5,557
Reaction score
8,193
Wahenga wanasema kumpiga teke chura ni kumuongezea hatua sasa Serikali imenikaanga mtaani mwaka wa saba huu bila ajira nikatafuta chimbo likawa linanipa dor za kulipa bills zote za muhimu na vichenchi kidogo kubaki

Sasa kuna wakati natamani ajira maana mishe zinakazaga kiasi kwamba hata kwa mangi hakuendeki lakini kipindi kama hicho Serikali nayo imeukausha hakuna mikeka ya nafasi za kazi wala kuitwa interview/kazi.

Cha ajabu sasa pale wanapoita wananikuta nipo well off na miharakati kibao na mishe za pesa kila siku najikuta sina habari na ajira zao tena kwanza hakuna boss alieajiriwa
 
Dah! Sasa mimi nakushauri usiwe unaomba kabisa mkuu, we komaa tuu na ngekewa yako ya kupata hela. 😊
Nitafanyia kazi ushauri wako maana nimeitwa interview post ya mwaka jana sasa wajiuliza mwaka mzima mtu huyo bado anashida na ajira hiyohiyo tu yani hana kazi nyingine anasubiri hiyo ajira pekeake
 
Back
Top Bottom