Kila mwanaume na treatment zake

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,778
Kawaida huwezi kumpa kila mwanaume treatment za mume wakati bado ni mchumba tu.
Vijana wengi leo wanapochumbiana au kutafuta urafiki wa kawaida katika ya kaka na dada (dating) wengi hawajajua kwamba hiyo ni hatua ya mwanzo kabisa na ni kama usaili tu wa kumpata mtu wa kuoana naye.
Ndoa na uchumba (girlfriend/boyfriend) ni vitu viwili tofauti kabisa uchumba huhusisha kumfahamu mwenzako kama anafaa kuwa mke au mume na ndoa ni agano na kumkubali mtu kuishi naye “No matter what” hadi kifo.

Hata siku moja uchumba si ndoa na ndoa si uchumba.

Ukimpa mchumba haki za mume au mke siku mkiachana na huo uchumba (kitu ambacho ni kawaida kama ukiona candidate uliyaye katika uchumba hawezi kwa excellent material ya ndoa) utaumizwa zaidi hasa mwanamke kwani mwanaume anaweza kumpata binti mwingine jioni yake au usiku huohuo na akaendelea na maisha.

Kinachoshangaza pia ni kwamba hata relationship inapovunjika mara nyingi mwanaume huumia kidogo kwa kuwa mwanaume siku zote anapoingia kwenye mapenzi huingia na “open mind”, wakati mwanamke akimpata mwanaume (uchumba) anajiona amampata “the Special one”.

Utasikia akina dada wengi wanasema “Nipo kwenye committed relationship” wakati ni ugirlfriend na uboyfriend tu, ni kweli uposahihi hata hivyo unatakiwa kuacha nafasi kwa ajli ya kuchunguza na si kumfanya huyo mwanaume ni mume wako na kumpa haki zote au services zote kiasi kwamba mahusiano yakivunjika unaanza kusaga meno.

Si busara kumpa mwanaume kila kitu katika mahusiano ya uchumba wakati hujaoana naye. Unamfulia nguo, unalala kwake, unampikia chakula wakati yeye ni boyfriend tu!

Swali ambalo mwanaume anajiuliza ni kwa nini aingie gharama za kukuoa kama umeshakuwa mke hata bila ring kwenye kidole?

Kwa nini akuoe wakati tayari ameshajua kila kitu kuhusu wewe?

Kwa nini anunue ng’ombe kama maziwa na nyama vyote anapata bure?

Kumbuka wazazi wetu walikuwa makini sana na hayo na mwanamke yeyeyote hakujifanya mke wakati ni mchumba tu. Uchumba ni daraja tu la kupita kufikia ndoa. Huwezi kugawa zawadi zote ambazo zipo kwenye begi kabla ya kufika kwa mwenyeji wako katika safari ya kuelekea kwenye ndoa.

Wanaume ni binadamu si Mungu na kila binadamu ana sifa ya kugeuka nyuma pale anapoona njia anayoenda si yenyewe.

Uwe na lengo lakuhakikisha unaweza kuweka mipaka na usimfanye huyo mwanaume ndo kila kitu hata duniani kwani kuna siku anaweza kubadili uamuzi ndipo kujuta kutakuja.
Ni busara kwa wewe mwanamke hata kama una mchumba uendelee kujihusisha na kazi yako, taaluma yako kiasi kwamba hata ikitokea amekuacha huwezi kuchanganyikiwa.

Kama umewekeza kwa mchumba upendo na mapenzi ya asilimia 100 Je, baada ya kuoana utawekeza kiaasi gain?

Usijifanye mke wakati ni mchumba.

“Don’t play wife if you are nothing, but mere girlfriend”

 
Si busara kumpa mwanaume kila kitu katika mahusiano ya uchumba wakati hujaoana naye. Unamfulia nguo, unalala kwake, unampikia chakula wakati yeye ni boyfriend tu!
Kwa kweli mie nafanya haya yote na yeye pia kwangu sioni shida hata tukija kuachana haijalishi kila mtu ali benefit in one way or another
 
Nimeipenda thread yako,tatizo vijana hawawezi kutofautisha hayo,lakini hili ni tatizo kwani mume/mke wote wanatazamwa tofauti,lakini uchumba wa siku hizi ni ndoa tofauti ni kuwa hawaishi pamoja,yote wanayofanya mke na mume wanayafanya wachumba!Wat a shame!
 
Back
Top Bottom