Elections 2010 Kila la heri na uchaguzi uende kwa usalama

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,598
Ndugu zangu wana JF na wa Watanzania wote, leo ndiyo siku ambayo tumeisubiri kwa muda mrefu. Ni siku muhimu sana katika mapambazuko mapya ya nchi yetu. Nawaomba kila mmoja wetu ambaye amejiandikisha na hana kizuizi chochote akapige kura. Tujitahidi kuwahi katika vituo vyenu ili tuweze kutekeleza wajibu huu muhimu wa kumpigia kura kiongozi wetu ajaye.

Nawatakia kila la heri mnapoenda kupiga kura katika vituo vyenu. Kumbukeni, kura yako moja ni muhimu sana kati huu uchaguzi.

Mungu awabariki sana na uchaguzi wetu uishe salama.

DC
 
Back
Top Bottom