Mkereketwa_Huyu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 9,225
- 6,349
Kwako Mh. rais wetu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania. Miaka michache iliyopita uliunda TAKUKURU kuja kudhibiti rushwa hapa Tanzania na tukaipokea kwa mashaka pamoja na furaha kwa wale waliokurupuka kwa kuundwa chombo kipya. Ni dhahiri kabisa hapa Tanzania kuwa baadhi ya mawaziri, makatibu wakuu, ma dc, ocd, rpc, na wengine kibao ni wala rushwa lakini mpaka leo hii naandika makala hii sijapata sikia hawa watu kukamatwa na TAKUKURU. Utakuja sikia tu mtu asiyefahamika kakamatwa, au mtu wa chini kabisa mla elfu 10 mpaka 100,000 kakamatwa wale wala mamilioni wako wanapeta kulikoni? Kwenye wizara yetu (mafichoni) waziri na katibu mkuu wake ni wala rushwa sana, na baadhi ya wafanyakazi wengi tu tuliandika barua na kutia kwenye sanduku la maoni mpaka leo hii hawa jamaa bado wanapeta na tena sasa wana hasira zaidi nasi, je walitonywa na TAKUKURU kuwa tunawalalamikia? Kwa mtazamo wa wengi, TAKUKURU is not fair as they are only there kula na kunyanyasa watu wasiokula nao. Sasa kwa nini Mh. rais usiue hii TAKUKURU na utuachie madaraka sie wananchi tufanye kazi kama Rwanda? Kule kila mwananchi ni askari wa mwenziwe katika kupambana na rushwa na waangalie sasa waliko. Ile nchi ndiyo nchi inayokuwa kuiuchumi zaidi hapa Afrika because of good governance, why not US?