bridalmask
JF-Expert Member
- Jan 14, 2015
- 2,195
- 1,169
Hivi wizara hii ya uchukuzi ilikuwa na kasoro kiasi kwamba Mwakyembe alitakiwa kunyakuliwa kwenye wizara ya uchukuzi na kisha kupelekwa wizara nyingne?!!?!, au ndio kuwa mwakyembe akipelekwa huko sifa aliyokuwa nayo itafifia!!!?
Mzee huyu huwa akiamua anafanya kazi hata huko EAC tutamskia tu!!!
Asee,mwakyembe ni mbunge wangu na mbaya zaidi ni jirani yangu nyumba ya tatu toka kwao ikolo kwa mama yake njia ya kwenda ngonga,hii n kwa faida ya wadau humu kule hakana alichofanya,kna manomba ya maji kila baada ya nyumba kumi yalijengengwa na wananchi miaka thelathini iliyopita kwa hisani ya mfuko flan wa jamii ndo pekee ukija kyela tena ikolo utakuta bara bara ni mbovu za zaman sana tena kuelekea bandarini na njia ni kokoto kwa upandea wa njia ya kwao inayopita uani kwao yaani nyumba yao n.kama jeng la benjamin mkapa afu bar bar ni ile ya nje pale ila ni ya vumbi,maji hakna tena mabomba yameziba,umeme hakna,mashirika na vikundi vidogo vya uuzaji wa kokoa vmekufa na magodwn pia yamekua magofu ambayo yalkua n sehm ya uchumi wa watu wa kyela...kwa kweli niljarbu kwend kukutana na badhi ya wadau wa chama na weny viti wa vijiji asee ni tatzo kwao pamoja na kua team mwakyembe ila shida zile za kule zmewavaa japo kyela n wilaya yenye utajir mkubwa sana na rasilimali nyingi haiitaji jambo kubwa sanaaa kufanya maisha ya wanakyela ambao kwa ssa n mchanyiko wa makabila karbu yote na mchaga na mkinga na mmakonde akiweka makaz kwa ajili ya biashar kufanya kyela iwe juu na nzr.na iwe ni sehem inayochangia pato la taifa kwa kiwango cha juu..ssa kiongoz anajenga nyumban kwanz na nje pia ssa kwa kweli mr kule kaacha kama alivyokuta sana sana jiran yetu pale mr mwamunyange mkuu wa majeshi ndo kidogoo kafany kitu sio yye..Asanteni
Mashauri,
Mwakiembe kapata wapi pesa bilioni
moja ya kununua kiwanja Bahari beach?
Ikulu wanajua kila kitu na deals zake bandarini ndio maana wamemtoa,
Hata yeye anajua kwanini katolewa.
Yaani hii nchi imegeuzwa kikampuni cha familia kadhaa tu na wanaitafuna kweli kweli. Mwakyembe amerudisha imani na nchi majirani wanaotumia bandari yetu baada ya kukata tamaa kutokana na kuchukua muda mrefu kutoa mizigo yao na mingine kupotea hovyohovyo na makusanyo yalikuwa kidogo sana na Mwakyembe kayapandisha Kwa sana. Jamaa kaleta treni Dar na limesaidia wananchi wengi. Leo kweli unamtoa Mwakyembe wizara ile? Rais hauko na nia njema na hii nchi na watanzania wengi wanaoteseka Kwa umaskini ili hali kuna watu wachache wamejilimbikizia mali kiasi kwamba hata hawajuwi wazifanyie nini.
Washauriiii????? Kwani Raisi anafanya kazi kwa ushauri tuu??? Yaaani ni Kwamba kwa kelele hizi hata mwananchi wa kawaida ama sisi wenye akili ndogo kama tungekiwa na nafasi tafsiri yake uhamisho wa mwakyembe usingeweza kufanywa hata Kama tungeshauriwaje na maanisha Kuwa hii kitu kuielewa haihitaji ushauri . Serikali hii inafanyakazi kwa kufurahishana si kwa manufaa ya wengi.Me wizara hizo nyingine siwezi sema mengi lakini hii ya mwakyembe ,nadhani kuna hira ba uvundo ndani yake yaaani kuna vitu mwakyembe haendani na kikwete yeye kama yeye au nawashauri wake wa karbu na pengine wakiwa wanahofia baadhi ya vitu,ukumbuke sita alitupwa huko EAC,baada ya kuwa anaikosoa sana safu ya uongozi wa juu na hasa reaction alizoonesha baada ta kukosa uspeaker.
Sasa basi makyembe amekuwa amejizolea umaarufu na alikuwa amepambana na uozo ulikuwa umejificha hko bandarini na kna watu hadi leo wanapga makofi na yamkini watardushwa tena kwani mwakyembe katoka!!!
Ngurubhe...... Huo ndio ukweli mchungu. Nilichofanya ni kuacha ushabiki na kuelezea FACTS na sio kutoa hoja kwa hisia.
wewe nenda kwenye kila fact...niambie wapi ni uwongo....
..Bath 13&14 zimejengwa? Zipo wapi?
Reli ya Kati ishajengwa? Ipo wapi? Na je ni uwongo kwamba Rwanda na Uganda sasa wameamua kuweka matumaini yaomkwenye reli ya Kenya badala ya Tanzania?
ATCL ishatoka ICU? Ipo wapi?
Meli za uhakika katika ziwa Victoria na Tanganyika zishapelekwa? Zipo wapi?
Mkurugenzi Mkuu wa Bandari keshateuliwa? Ameteuliwa lini? Ninajua aliyepo anakaimu
niambie huo ukweli uliokuwa faslified ni upi? Tusipende kusifia vitu hewa........
Acha kabisa mkuu, huyu Mwakyembe ni sawa kabisa na David Mwakyusa Rungwe Magharibi. Yaani hopeless kabisa hata alivyokuwa waziri wa afya 2005. Yaani sijui hawa wanyaki Nani kawaloga?Kama huijui Kyela nyamaza tafadhali
Kyela tuna bandari HAJAWAHI igusa hata kwa miundo mbinu kila siku tunaona anaimarisha bandai ya Dar,Mwanza na Tanga
Kyela tuna meli chakavu zinazo zima katikati ya ziwa kila siku lkn ni Mwakyembe aliyeipa Mwanza hela za meli mpya!
Mwakyembe ni mbunge wa hovyo hovyo kupata kutokea ktk Wilaya ya Kyela na hawezi shinda hata kura za maoni
achilia mbali kupambana na CHADEMA
Mashauri,
Mwakiembe kapata wapi pesa bilioni
moja ya kununua kiwanja Bahari beach?
Ikulu wanajua kila kitu na deals zake bandarini ndio maana wamemtoa,
Hata yeye anajua kwanini katolewa.
Hivi aliyekuwa anashughulikia sana madawa ya kulevya ni nani.......?.......nashawishika kuamini kwamba.......Mwakyembe ameziba mengi hivyo funika kombe mwanaharamu apite.........
wamalize muda wao waondoke........washatuchosha..........aaaaaghh ........
Tatizo ni kuwa Mwkyembe alivunja mkatapa wa kifisadi kwenye suala la upanuzi wa bandari ambapo tungepigwa mamilioni ya dolaukiwa mtendaji mzuri kwa maana ya kuangalia maslahi ya umma huwezi kuwa rafiki wa Jk na CCM yake.
Ona mfano mwanasheria wa Tanesco katika sakata la Escrow alivyopigania nchi,matokeo yake akapigwa chini na kubambikiziwa kesi ya mauaji,Jk hakumtaja kabisa huyu wakati akiongea na wazee wa dar.
Huyu ndio Jk,si kila king"aacho ni dhahabu.Hakuna aliyetegemea huyu jamaa atakuwa hivi mwaka 2005.
yaani mi ananipa mawazo sana maana huwa nafikiria nchi yetu Hadi nakosa hamu ya kula
Kwani ili aonekane anafanta kitu tunatazama na kuangalia kona zipi!?,kuwa kafanya nin kitaifa au kijijini kwaoooo?,na kama hajfanya hivo vitu kjjn kwaoo basi huyo si fisadi!!!.tunaongea kitaifa zaidi mkuu!
Issue sio wakati gani alitakiwa kuwa huko EAC issue ni kwamba EAC inahitaji watu competent, so there's nothing wrong kwa Mwakyembe kupelekwa EAC na ndio maana kama umesoma Raia Mwema, hata wabunge wa EAC-Tanzania wamefurahia suala la Mwakyembe kupelekwa huko. Kwamba Mwakyembe kupelekwa EAC ni kumpoteza ni dhana ya hovyo. By the way, hata Sitta alikuwa ni right guy kuwa EAC... soma Raia Mwema ndipo utafahamu kwamba watu hawakurupuki wanapofanya maamuzi yao.If so, why not tangu mwanzo???!!!
Au manyang'au wamezaliwa 2015