Katika kutafakari nimegundua kikwete si dhaifu ila sisi watanzania Watanzania tunaporojo na wanafiki kwa mambo ya msingi. Ninamaanisha kilichotufanya tumchague Kikwete licha ya udhaifu alioonyesha awamu ya kwanza ninini? Leo madaktari wanagoma kwa ajili ya kuboresha huduma mahospitalini watanzania wanawalaumu, baadala ya kuandamana na kuishinikiza serikali ikae na madaktari wafikie muafaka tunalalamika tu. Rais katoa hotuba ya hovyo na kibabe watu wanaandamana kuunga mkono hotuba, wabunge wa CCM wanafurahia na kupongeza hotuba hiyo UNAFIKI! Walimu wanapanga kugoma wapo watu wanawabeza baadala ya kuwaunga mkono kwa kuishinikiza serikali itatue matatizo ya kijamii watanzania tunasubiri kuunga mkono hotuba ya Kikwete. Wanawapa wawekezaji Ardhi yetu, Wabunge wanapongeza UNAFIKI na kujipendekeza.Usalama waTaifa unafanya upuuzi wa kuteka watu bado tupo tunashangaa na wengine wanashangilia. Kwa ufupi CCM na kikwete wanatuenjoy kwani wanajua hakuna kitakachoendelea, wanaua, wanateka, wanakula nchi, wanaiba rasilimali huku wakitudhihaki! Mbunge anakazi gani muhimu kuliko mwalimu na daktari kiasi cha kulipwa pesa nying jamani,sheria wanazotunga ni za kuwalinda wao, Vinaundwa vyombo kwa ajili ya kupeana vyeo, ona TAKUKURU wanafanya nini rushwa imekuwa kitu halali. Hivi kunahitajika nguvu gani kuwakamata traffic wanaokularushwa barabarani jamani mbona watanzania tumekuwa wanyonge mno. Tunatakiwa tufanye kitu hali inakokwenda ni mbaya. Kikwete amejaa kiburi cha ajabu anaposhauriwa kukaa na madaktari anapuza kwa vile tu anajua watanzania ni dhaifu hawawezi kufanya lolote. EEE MUNGU TUNUSURU