njiwa
JF-Expert Member
- Apr 16, 2009
- 12,369
- 5,514
Wandugu,
Kama kuna jambo ambalo huwa linanishangaza ni hili la wazee wa Dar es Salaam. Katika nyakati zote ambazo mtawala wa nchi hii Dr. Dr. Dr. (Heshima-UDOM, UTURUKI, UDSM) alidai anaongea na wazee, nilichodhuhudia ni uwepo wa akina dada wa 'mipasho' waliosiliba midomo yao na rangi wakishangilia kwa sauti ileile inayotolewa kwenye taarabu. Mbaya zaidi wengi wao huwa wanakuwa kwenye lindi la usingizi wakati mtawala na msomi wa PhD ya heshima akiendelea kutoa hotuba yake. Wakati mwingine huwa inakuwa kama mchezo wa kuigiza hivi.
Jambo jingine ambalo huwa najiuliza ni je hao ni wazee wa Dar es Salaam au ni wana ccm wa Dar es Salaam tena kutoka Ilala na Temeke kwa wala ubwabwa na wanywa kahawa?
hapo kwenye Red unazungumzia PHD Ya nini..???
hapo kwenye black "wazee wa dar" wenyeji wa DSM hivi inakupa shida kufukiri wenyeji wazee wa dar ni watu wa pwani... sasa mbona unadhihaki mila na desturi zao... nawashangaa mnaposema kunywa kahawa barazani ni uswahili na kunywa ma wisky na pombe ndio uzungu ..... wawapi weye ...????
basi sisi watu wa pwani hatutaki huo uzungu wenu tuacheni na huu uswahili wetu .....
kumbuka TANU baadaye ikawa CCM harakati na mambo yote yalikuwa dar.... je wadhani wale wazee ambao walikuwa toka enzi hizo za tanu au wamelelewa na wazee wao ambao walikunywa maji ya TANU ulitaka waje na reaction gani ...! kwamba CCM ife.. give them a break
Mfano akienda moshi na kusema nataka kuongea na wazee wa moshi ofcoz utakuta mandhari tofauti na wazee wa dsm kutokana na mila za wale watu wa eneo lile... yaani hata mtoto wa primary school hawezi akaja na thread kama hii totaly wasted + crap!