Miongoni mwa makosa makubwa sana aliyofanya Jakaya Kikwete katika urais wake ni kitendo cha kumruhusu Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, kwenda mahakamani kutoa ushahidi. Mkapa alitoa ushahidi dhidi ya Serikali katika kesi inayomkabili Profesa Mahalu. Nyerere ameshafariki dunia, Mwinyi hana maneno na mtu hata akipita mitaani. Mkapa tayari ameshafika mahakamani kutoa ushahiditena dhidi ya Serikali ile ile inayomshitaki Mahalu. Kitakachofuata sasa ni kuwa Kikwete naye atakwenda mahakamani kama Mkapa alivyokwenda, lakini siyo kutoa ushahidi kama alivyotoa Mkapa, bali kushitakiwa. Hayo ni maono yangu.