Kwa nini kashindwa hata kumtaja jina Lowasa kama mmliki wa richmond , kwa nini hakusema live "richmond ni ya Lowasa" kama alivyosema Tundu Lisu kwamba richmond ni ya Kikwete?
Kama richmond ni ya Lowasa Dowans na symbion ni za nani?
Kama Lowasa ni mmiliki wa richmond kwa nini JK aliruhusu apewe mafao ya uwaziri mkuu mstaafu kwa miaka 8 na kwa nini baada ya kujiuzulu uwaziri mkuu JK alimpa usimamizi wa kazi za serikali kama ujenzi wa shule za kata, na kwa nini JK aliruhusu lowassa ashike uenyekiti wa kamati ya usalama wa bunge?
Kama richmond ni ya Lowasa na JK anafahamu kama anavyodai, kwa nini mpaka sasa hivi Lowasa anakatiza mikoani kuomba kura za uraisi badala ya kuwa jela?
Nasubiri siku jk atakapo mwaga ukweli wote wa escrow na hivyo kumfanya lowassa kuanguka kwa aibu ktk sanduku la kura.
kama ni kujiuzulu Kikwete anastahiki kutangaza mara moja amejiuzulu ,yaani kesho ajitokeze na kutangaza ,ni aibu kuendelea kuitwa Raisi wa nchi ,kwa sababu Raisi inakuwaje alalamike kwenye majukwaa kwamba fulani anefuatana na Lissu ndie fisadi linalohusika na Richmond ,
Na Lisu nae amemjibu Kiwete kwamba yeye ndie anaemiliki dili la richmond ,raisi ameshindwa tena ameshindwa katika dakika za mwisho.
Sijui tuitishe maandamano Nchi nzima kumutaka raisi ajiuzulu kwa kuwa anajibizana kwenye majukwaa baada ya kuchukua sheria.
Usibadili topic hapa....suala ni nani anahusika...ukitaka kuongelea suluhisho la ufisadi basi fungua thread nyingineHayo maswali uliyouliza majibu yake Ndiyo suluhisho la ufisadi?
Nchi Rais analialia, Mwananchi wa kawaida analialia!
Sasa JK alitaka Wananchi ndiyo wakamkamate muhusika wa Richmond?
kama ni kujiuzulu Kikwete anastahiki kutangaza mara moja amejiuzulu ,yaani kesho ajitokeze na kutangaza ,ni aibu kuendelea kuitwa Raisi wa nchi ,kwa sababu Raisi inakuwaje alalamike kwenye majukwaa kwamba fulani anefuatana na Lissu ndie fisadi linalohusika na Richmond ,
Na Lisu nae amemjibu Kiwete kwamba yeye ndie anaemiliki dili la richmond ,raisi ameshindwa tena ameshindwa katika dakika za mwisho.
Sijui tuitishe maandamano Nchi nzima kumutaka raisi ajiuzulu kwa kuwa anajibizana kwenye majukwaa baada ya kuchukua sheria.
Hapo sasa daaah acha tuNgoma inogile. Huku ubungo Kubenea nae kasema atawataja waliobeba hela stanbic.
Wewe huna akili kweli ndugu yangu, unadhani RAIS ni kama baba yako? unaonekana hata shule hujaenda maana unakurupuka tu kama unaenda kupokea chakula cha njaa, kwani alichoksea yeye kumtaja ni nini? Lisu yeye kawakumbatia na sasa anajifanya kuwasafisha hao mapapa, kwanza amekuwa mtu wa kukurupuka ovyo, hajui kujipanga, anajibu kwa jazba, alikuwa wapi muda wote mpaka aanze kuiga usemi wa JK? MMEKWISHA MWAKA HUU HAMAPATI KUINGIA iKULU NG'OOO MIAKA LAKI 8
Tumuite Julius Malema wa EFF aje atusaidie kumwita JK kuwa ni the most criminal person in the world