armanisankara
JF-Expert Member
- Jul 15, 2011
- 283
- 49
Rais Jakaya Kikwete, amemteua Winfrida Beatrice Korosso, kuwa Katibu wa Tume ya Kurekebisha Sheria nchini.
Taarifa iliyotolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, ilisema uteuzi huo ulianza Agosti 14, mwaka huu.
Kabla ya uteuzi wake, Korosso alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Mkurugenzi wa Mashitaka katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam.
CHANZO: NIPASHE
Taarifa iliyotolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, ilisema uteuzi huo ulianza Agosti 14, mwaka huu.
Kabla ya uteuzi wake, Korosso alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Mkurugenzi wa Mashitaka katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam.
CHANZO: NIPASHE